mdida
JF-Expert Member
- Jul 14, 2011
- 1,607
- 777
Kusema kweli nina rafiki yangu yupo njia panda, mpenzi wake amekasirika sana wala hataki kumuelewa, imekaa hivi kuna jamaa mmoja alikuwa akimtokea huyo rafiki yangu mwenyewe anavyosema, akamwambia Yule jamaa kuwa na mpenzi wake so hamtaki, Yule jamaa akasema basi awe rafiki yake tu coz nayeye ana mtu wake, basi akawa anamtumia huyu dada sms. Siku ya siku ndo akatuma hiyo ya G9T Dear mwaaa!!! Mpenzi wake akasikia sms ikingia ile kuchukua cm akakutana na mwaaa sasa mambo yameharibika, ameshamwelewesha sana lakini hamwelewi, Ila dada wa watu anasema Yule jamaa alimkataza na akaelewa sasa sijui ilikuaje akamtumia sms ya vile. Wanajamvi hebu saidia hapa jinsi gani shemeji yangu aambiwaje ili aamini.