Future ya CCM baada ya Lowassa kung'oka

Future ya CCM baada ya Lowassa kung'oka

Pesa mbaya sana.
Hata mataifa makubwa duniani yanaitwa hivyo sababu yana pesa nyingi, na si sababu ya ukubwa wa eneo la nchi au idadi ya watu. Inge kuwa sababu ya ukubwa wa eneo lake hata Kongo inge itwa taifa kubwa.
 
Mkuu ni swala la muda tu. Just wait and see, chadema walikuwa namba moja kusema mamvi ni fisadi leo wanamkaribisha kwenye chama Chao, wanataka kutuambia nini? Leo kawa msafi wamemuosha kwa sabuni gani? Au alikuwa fisadi alipokuwa ndani ya ccm ila chadema kawa malaika? Kweli siasa mchezo mchafu walikuwa mstari wa mbele kumpaka matope leo wanampaka wanja. Chadema wanamaswali ya kujibu kuhusu usafi wa lowasa.

Kuna jibu wamelimeza wanasema ''MFUMO''
 
kwan yesu alikuwa na wafuasi wangapi lakin wakati anaenda kusulubiwa msarabani nani alimfata? lowassa alikuwa na wafwasi wengi kpnd yupo ccm bt akitoka ccm atakwenda peke yake myb na mke wake kwa maana imeandikwa kuwa mke au mme atawaacha wazaz wake na kuambatana na mumewe wakawe mwili mmoja

Well said "The great"
 
Siasa ni mchezo wa kufarahisha sana, lakini tahadhari ya kawaida katika maisha ya kila siku, Tukio moja halihitimishi mchakato! Hizi ni hatua za awali tu, kila mwanasiasa anaefahamu mchezo wa siasa vizuri, mwanzo una umuhimu mkubwa! Lakini ni mapema mno kutangaza ushindi!! Siasa ni kama mchezo wa mpira, Mwamuzi huwa ni zile dakika 90 za mchezo!!

Alihama Mrema kwa mbwembwe nyingi! Kwenye uchaguzi Chalii!
Fanyeni ushabiki, kajiandikisheni, na muhimu mkapige kura muda ukifika!!!

Wakati wa Mrema sio sasa!!!! Watanzania wa leo sio wale ni wengine kabisaa
 
Kilichofanywa na ccm ni kuonesha kuwa chama hicho ni makini kinaangalia maslah ya wengi kuliko mtu. Kwa upande wa chadema hakuna hiki kitu ndio maana mbowe anafanya mambo anavyotaka. Uamuzi wa Mbowe kumruhusu EL kujiunga Chadema ni uamuzi wa Mbowe na sio Wanachadema.

Ila kwa kuwa Chadema inaendeshwa kisultani, Wanachadema wameaminishwa uongo kuwa ukweli. Na hapa ndipo tunakosa kuleta mabadiliko kwa sababu ya uzembe wa viongozi wa upinzani.

Mbona unalialiaaaa......kwani wewe umejipangaje!!!!!!?
 

Nimeipenda falsafa yako,nikukumbushe ukweli huu, kuwa wanasiasa Hawana kitu kinachoitwa AIBU! lakini Kwa maoni yangu inawezekana kinachotafutwa ni zaidi ya heshima! Ni utumishi katika taasisi ya Urais! Siku zote, mafanikio ya taasisi hii ya urais yanategemea mfumo unaotawala kipindi hicho! Naamini uwanja wa CCM unatofautiana na ule wa CDM!! Aibu inaweza isimpate!

umenena kweli kabisa
 
Unaota ndoto za mchana, CCM chama dola, Lowassa wenu mtaumbuka tu.

Masuala ya chama dola kwa UKAWA ya leo c rahisi kama unavyo fikiri ndugu yangu sasa lazima chama kikuu cha upinzani mwakan kiwe CCM
 
juzi nilimsikia makonda akijisifu kuwa tumemkata, na kusema tayari amejiandikisha iliaendeleze kukata watu kwenye box la kupigia kula. aliongea haya kwenye redio moja wakati wakimuhoji kuhusu maji taka kinondoni.

my take;
je sasa hivi ccm itakuja na sera gani, sera ya atakatwa, kakatwa na tumemkata imeisha x-pair, maana jina lake el limezidi kushamiri na kuchukua kurasa za mbele kwenye vyombo vya habari toka mumkate, na jana chati yake ime sky rocket gafla na hii mpaka october
 
Nape ajiande kwenda kulima viazi vitamu na alivyotepetea kaa toto lilivyolelewa na bibi,basi,akishindwa kulima atakuwa mpuliza moto jikoni.
 
CCM itabaki imara daima. Kete ya ufisadi ndio ilikuwa inaipaisha ukawa aka cdm na upinzani kwa ujumla. Kwasasa Kete yao itakuwa ipi? Hawana.
 
Mimi nahurumia gas yetu iliyokuwa inaviziwa na akina mengi na rostam
 
CCM itabaki imara daima. Kete ya ufisadi ndio ilikuwa inaipaisha ukawa aka cdm na upinzani kwa ujumla. Kwasasa Kete yao itakuwa ipi? Hawana.
escrow mikayaba mibovu kutokilopwa kwa mirabaha na ukwepaji wa kodi JK analo mwaka huu
 
Back
Top Bottom