Future ya CCM baada ya Lowassa kung'oka

Future ya CCM baada ya Lowassa kung'oka

ndoto gani hizo za mchana

Mkuu ni swala la muda tu. Just wait and see, chadema walikuwa namba moja kusema mamvi ni fisadi leo wanamkaribisha kwenye chama Chao, wanataka kutuambia nini? Leo kawa msafi wamemuosha kwa sabuni gani? Au alikuwa fisadi alipokuwa ndani ya ccm ila chadema kawa malaika? Kweli siasa mchezo mchafu walikuwa mstari wa mbele kumpaka matope leo wanampaka wanja. Chadema wanamaswali ya kujibu kuhusu usafi wa lowasa.
 
Hii ni fursa adimu na nadra sana kutokea in a life time,ni fursa ya kuiondoa ccm madarakani.
 
Mipango na mawazo ya Mungu sio kama ya wanadamu,ifike mahali tuangalie utaifa kwanza ccm wameichezea nchi hii sana acha wameguke akili iwakae sawa.
 
kwan yesu alikuwa na wafuasi wangapi lakin wakati anaenda kusulubiwa msarabani nani alimfata? lowassa alikuwa na wafwasi wengi kpnd yupo ccm bt akitoka ccm atakwenda peke yake myb na mke wake kwa maana imeandikwa kuwa mke au mme atawaacha wazaz wake na kuambatana na mumewe wakawe mwili mmoja
 
Nikuwa chama cha upinzani. Ninasikitika tuu kuwa kama kitakuwa na wabunge kama Asumpta au Kibajaji basi tutakuwa na wapinzani wa hovyo sana.

hehehehe kibajaji tena atakuwa upinzani,manake ccm isubiri miaka 2000 ndio ije kushika dola
 
Mipango na mawazo ya Mungu sio kama ya wanadamu,ifike mahali tuangalie utaifa kwanza ccm wameichezea nchi hii sana acha wameguke akili iwakae sawa.

mkuu Vonix umezungumza kwa jazba sana,anyway huo ndio uzalendo
 
Last edited by a moderator:
Ccm hawakuwa na evidence yoyote kuwa lowasa ni fisad.wamkamate tu kwa sasa si hana tena immunity!!!!!!
 
Siasa ni mchezo wa kufarahisha sana, lakini tahadhari ya kawaida katika maisha ya kila siku, Tukio moja halihitimishi mchakato! Hizi ni hatua za awali tu, kila mwanasiasa anaefahamu mchezo wa siasa vizuri, mwanzo una umuhimu mkubwa! Lakini ni mapema mno kutangaza ushindi!! Siasa ni kama mchezo wa mpira, Mwamuzi huwa ni zile dakika 90 za mchezo!!

Alihama Mrema kwa mbwembwe nyingi! Kwenye uchaguzi Chalii!
Fanyeni ushabiki, kajiandikisheni, na muhimu mkapige kura muda ukifika!!!
 
kwan yesu alikuwa na wafuasi wangapi lakin wakati anaenda kusulubiwa msarabani nani alimfata? lowassa alikuwa na wafwasi wengi kpnd yupo ccm bt akitoka ccm atakwenda peke yake myb na mke wake kwa maana imeandikwa kuwa mke au mme atawaacha wazaz wake na kuambatana na mumewe wakawe mwili mmoja

Ni bora ukaweka akiba maneno yako! Siasa haina adabu, inaweza kukuumbua kesho! Umewasikia wanasiasa wakivikana vyama vyao vya zamani kwa kudai si baba wala mama ambaye hawezi kukanwa! Ungengoja baada ya oktoba ndo useme hayo!
 
Kilichofanywa na ccm ni kuonesha kuwa chama hicho ni makini kinaangalia maslah ya wengi kuliko mtu. Kwa upande wa chadema hakuna hiki kitu ndio maana mbowe anafanya mambo anavyotaka. Uamuzi wa Mbowe kumruhusu EL kujiunga Chadema ni uamuzi wa Mbowe na sio Wanachadema.

Ila kwa kuwa Chadema inaendeshwa kisultani, Wanachadema wameaminishwa uongo kuwa ukweli. Na hapa ndipo tunakosa kuleta mabadiliko kwa sababu ya uzembe wa viongozi wa upinzani.

Mtawaya waya sanaaaaaa UKAWA ileeeeeeeee magogoni! Karibu kamanda Lowassa
 
Lowasa anaitafuta heshima kwa gharama kubwa atapata aibu kwa bei nafuu.

Nimeipenda falsafa yako,nikukumbushe ukweli huu, kuwa wanasiasa Hawana kitu kinachoitwa AIBU! lakini Kwa maoni yangu inawezekana kinachotafutwa ni zaidi ya heshima! Ni utumishi katika taasisi ya Urais! Siku zote, mafanikio ya taasisi hii ya urais yanategemea mfumo unaotawala kipindi hicho! Naamini uwanja wa CCM unatofautiana na ule wa CDM!! Aibu inaweza isimpate!
 
Back
Top Bottom