Future ya CCM baada ya Lowassa kung'oka

Future ya CCM baada ya Lowassa kung'oka

Ccm haijawahi kusema el ni msafi refer op magamba. Mkuu labda nikuulize na wewe sasa na huyo mwenyekiti wako leo ndio mnaona lowassa sio fisadi?

Lowasa angekuwa fisadi ni kwanini kwa muda wa miaka8 baada ya kujiuzuru kutoka nafasi ya pm hadi mwaka huu ccm walishindwa kumshitaki?hiyo inaonyesha kuwa lowasa ni msafi kabisa
 
kikwete yupo Australia anatafutia watoto wake business partiners anajali nini yule mtu bwana

Hivi mmeshasahau kampuni lao lililochota mapesa ya Escrow kule benki ya stanbic limesajiliwa Australia? Sijui lile kampuni linaitwa PP nini sijui!!
 
Wakuu,

Ni dhahiri kabisa future ya CCM ndio imefika ukingoni baada ya Lowassa kung'oka CCM, pia kama tunavyojua kundi la wafuasi wake kumfuata.

Hapa tujikumbushe nyuma kidogo, baada ya Lowassa kukatwa jina ndio makundi makubwa ya wanachama wa CCM walipopinga kukatwa kwake huku wakiimba nyimbo mbalimbali za kumnadi Lowassa.

Sasa Lowassa amehama CCM na washirika wake ambao ndio wengi zaidi kuliko mwanaCCM yeyote kuamua kumfuata UKAWA.

Je, CCM itaweza kuendelea bila kundi hili kubwa kabisa kuwepo? Je, watakaobaki CCM watakuwa na mvuto katika jamii?

My take:
UKAWA isije kugeuka up coming CCM baada ya wanaCCM wengi kuomba kujiunga UKAWA.
Hivi Lowassa ni nani hasa eti kutoka kwake kuitikise CCM? Mafisadi wenzake wafanyabiashara wamebaki midomo wazi hii Nchi UKAWA kukamata dola kutegemea mtaji wa mafisadi mmebugi step. Mkwe wake Sioi Sumari mume wa Pamela Lowassa Yupo Arumeru busy ana kampeni aingie bungeni kwa tiketi ya CCM. Bashe Yuko Nzega busy CCM anausaka ubunge. Sophia Simba bado Mwenyekiti wa UWT aende CDM ili akawe nani ? BAVICHA halima atampisha? Nasema hivi main objective ya mwanasiasa ni kushika madaraka na kukamata dola. Hakuna Mwanasiasa Mjinga atakayetoka CCM bila uhakika wa kukamata madaraka. CCM wajanja walisogeza mchakato ili kuubabanisha na mchakato wauchaguzi wa NEC ili kuwadhibiti wanasiasa uchwara. Atanunua wale wa buku 15 wanachama wachache waliopoteza mvuto, wanaotoka KASKAZINI kwa kuwa ni mkabila. Wengine kina Sioi, Sofia, Bhashe wamebaki wakibwagwa kwenye mchakato ndio watakimbia kama mamvi lakini wakipita wanabaki kushika madaraka. Mamvi umekwisha kisiasa we peleka ubabe na mambo yako ya kulazimisha kwa nguvu ya pesa wachaga watakumaliza .
 
Hivi mmeshasahau kampuni lao lililochota mapesa ya Escrow kule benki ya stanbic limesajiliwa Australia? Sijui lile kampuni linaitwa PP nini sijui!!

Ngoja tumuulize lizaboni lazima ataijua hiyo kampuni
 
Ccm haijawahi kusema el ni msafi refer op magamba. Mkuu labda nikuulize na wewe sasa na huyo mwenyekiti wako leo ndio mnaona lowassa sio fisadi?

Kukanusha ndio falsafa ya ccm
 
Kazi ya chama cha siasa wakati wa uchaguzi ni kupiga propaganda ya kushawishi wananchi wawapigie kura ili washike dola. Ushawishi ni wa nini watakifanya kwa faida ya Nchi kupitia ilani ya uchaguzi ya miaka 5. Mwaka huu ukawa itatumia muda wake kushawishi Wananchi kumkubali Lowasa na kuwa ni msafi. Watatumia Jik, majivu, steel wool, mchanga etc ili asafishike. Wenzao wanashukuru gume gume limejivua gamba lenyewe. Hicho ndicho walichokitaka. Mbowe alisema Lowasa ni dhaifu hakukosea. Akisakamwa ataachia ngazi ya kugombea urais Siku 3 kabla ya uchaguzi na kudai wanamsakama sababu ya ugombea urais. Urais sio rahisi hamjiulizi kwanini Huyu mtu hatakiwi tangu 1995?
 
Tunaweza kuudanganya umma kuwa chama kipo imara na kitashinda lakini ukweli tunaujua. Mambo si shwari. Tunajikaza kisabuni kwa kurubuni tu. Mchakato wa Dodoma umetujeruhi. Si Lowassa pekee asiyeridhika. Wapo wengi ingawa wenyewe wameamua kunyamaza.

Dodoma imetuacha vipande vipande kama kunde au kande. Dodoma hatujatoka wale. Hadi sasa,CCM imepoteza Wabunge na Madiwani kadhaa. Imepoteza focus na nafasi ya kula nanasi. Kujidai. CCM imefikia kutokwa povu la nguvu mbele ya waandishi. Ya jana ni tosha kuthibitisha.

Ingawa mapengo yatajazwa,lakiní si mwaka huu. Too late to do it now. Ninawajua makada waliojiapiza kupigia kura upinzani ili wapate amani. Walitamani upinzani uanzie chamani. Ukweli ni kwamba,CCM haiko tulivu wala kuwa na wavumilivu. Imejaa wenye nia ovu na wivu. Kumechafuka!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

mkuu ndio kusema hata wewe umeridhia ukawa kuchukua nchi
 
Wakuu,

Ni dhahiri kabisa future ya CCM ndio imefika ukingoni baada ya Lowassa kung'oka CCM, pia kama tunavyojua kundi la wafuasi wake kumfuata.

Hapa tujikumbushe nyuma kidogo, baada ya Lowassa kukatwa jina ndio makundi makubwa ya wanachama wa CCM walipopinga kukatwa kwake huku wakiimba nyimbo mbalimbali za kumnadi Lowassa.

Sasa Lowassa amehama CCM na washirika wake ambao ndio wengi zaidi kuliko mwanaCCM yeyote kuamua kumfuata UKAWA.

Je, CCM itaweza kuendelea bila kundi hili kubwa kabisa kuwepo? Je, watakaobaki CCM watakuwa na mvuto katika jamii?

My take:
UKAWA isije kugeuka up coming CCM baada ya wanaCCM wengi kuomba kujiunga UKAWA.

Hata wakati lowasa yuko CCM haikuwai kushinda kihalali wenyewe wanajua
 
uchu wa madaraka ndo umempeleka huko chadema. Chadema ni chama makini hawawez kumfuata bali kajipeleka na sio kwa wamachama wote bali amemtumia mbowe ambaye ni rahisi kununulika

kwahiyo unakili EL ameinunua CDM
 
kwahiyo unakili EL ameinunua CDM

Hilo lipo wazi. Na uamuz wa Lowasa kuruhusiwa chadema haujapangwa na wanachadema wengi ila ni maamuz ya Mbowe. Mimj kama mwanachadema nakubaliana nasera ya kulichukua dola ila sio kwa candidate kama Lowasa. Mbowe ametuuza
 
ccm mus be very carefull especially when throwing stones to ENL otherwise it will be very tough on them in OCTOBER
 
Hilo lipo wazi. Na uamuz wa Lowasa kuruhusiwa chadema haujapangwa na wanachadema wengi ila ni maamuz ya Mbowe. Mimj kama mwanachadema nakubaliana nasera ya kulichukua dola ila sio kwa candidate kama Lowasa. Mbowe ametuuza

WEKKI wewe ni ccm unajulikana kitambo,hebu toka apa
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom