Future ya CCM baada ya Lowassa kung'oka

Future ya CCM baada ya Lowassa kung'oka

Kilichofanywa na ccm ni kuonesha kuwa chama hicho ni makini kinaangalia maslah ya wengi kuliko mtu. Kwa upande wa chadema hakuna hiki kitu ndio maana mbowe anafanya mambo anavyotaka. Uamuzi wa Mbowe kumruhusu EL kujiunga Chadema ni uamuzi wa Mbowe na sio Wanachadema.

Ila kwa kuwa Chadema inaendeshwa kisultani, Wanachadema wameaminishwa uongo kuwa ukweli. Na hapa ndipo tunakosa kuleta mabadiliko kwa sababu ya uzembe wa viongozi wa upinzani.

Ruksa kujifariji 😀
 
Kilichofanywa na ccm ni kuonesha kuwa chama hicho ni makini kinaangalia maslah ya wengi kuliko mtu. Kwa upande wa chadema hakuna hiki kitu ndio maana mbowe anafanya mambo anavyotaka. Uamuzi wa Mbowe kumruhusu EL kujiunga Chadema ni uamuzi wa Mbowe na sio Wanachadema.

Ila kwa kuwa Chadema inaendeshwa kisultani, Wanachadema wameaminishwa uongo kuwa ukweli. Na hapa ndipo tunakosa kuleta mabadiliko kwa sababu ya uzembe wa viongozi wa upinzani.

Naamini kabjsa unaongea hili jambo kutoka kwenye kichwa chako tena kwa ufahamu wako mdogo. Kama hujui kitu just "shut up"
 
Mkuu ni swala la muda tu. Just wait and see, chadema walikuwa namba moja kusema mamvi ni fisadi leo wanamkaribisha kwenye chama Chao, wanataka kutuambia nini? Leo kawa msafi wamemuosha kwa sabuni gani? Au alikuwa fisadi alipokuwa ndani ya ccm ila chadema kawa malaika? Kweli siasa mchezo mchafu walikuwa mstari wa mbele kumpaka matope leo wanampaka wanja. Chadema wanamaswali ya kujibu kuhusu usafi wa lowasa.

Hakuna mwana ccm alie furahi kwa maamuzi ya lowassa kuwatosa na tulitarajia hilo.

bakini na mchama wenu mfu huo,tukutane oktoba 25.
 
Wakuu,

Ni dhahiri kabisa future ya CCM ndio imefika ukingoni baada ya Lowassa kung'oka CCM, pia kama tunavyojua kundi la wafuasi wake kumfuata.

Hapa tujikumbushe nyuma kidogo, baada ya Lowassa kukatwa jina ndio makundi makubwa ya wanachama wa CCM walipopinga kukatwa kwake huku wakiimba nyimbo mbalimbali za kumnadi Lowassa.

Sasa Lowassa amehama CCM na washirika wake ambao ndio wengi zaidi kuliko mwanaCCM yeyote kuamua kumfuata UKAWA.

Je, CCM itaweza kuendelea bila kundi hili kubwa kabisa kuwepo? Je, watakaobaki CCM watakuwa na mvuto katika jamii?

My take:
UKAWA isije kugeuka up coming CCM baada ya wanaCCM wengi kuomba kujiunga UKAWA.

Uko sawa mkuu
 
CCM itabaki imara daima. Kete ya ufisadi ndio ilikuwa inaipaisha ukawa aka cdm na upinzani kwa ujumla. Kwasasa Kete yao itakuwa ipi? Hawana.

Wameambiwa kama wanaushahidi wapeleke mahakamani ila kama hawana wafunge vinywa.


habari yao imeisha.
 
Wakuu,

Ni dhahiri kabisa future ya CCM ndio imefika ukingoni baada ya Lowassa kung'oka CCM, pia kama tunavyojua kundi la wafuasi wake kumfuata.

Hapa tujikumbushe nyuma kidogo, baada ya Lowassa kukatwa jina ndio makundi makubwa ya wanachama wa CCM walipopinga kukatwa kwake huku wakiimba nyimbo mbalimbali za kumnadi Lowassa.

Sasa Lowassa amehama CCM na washirika wake ambao ndio wengi zaidi kuliko mwanaCCM yeyote kuamua kumfuata UKAWA.

Je, CCM itaweza kuendelea bila kundi hili kubwa kabisa kuwepo? Je, watakaobaki CCM watakuwa na mvuto katika jamii?

My take:
UKAWA isije kugeuka up coming CCM baada ya wanaCCM wengi kuomba kujiunga UKAWA.

Kabla ya kuandika au kusema chochote jaribu kujiuliza yafuatayo:

1: Kuna viongozi wangapi wakubwa wa CCM walistaafu au kuacha siasa ndani ya CCM na chama chao kiliendelea kuwa na nguvu mpaka leo??


2: Kuna viongozi wangapi wakubwa wa Serikali na chama walistaafu au kuacha siasa ndani ya chama chao cha CCM na chama chao kiliendelea kuwa na nguvu??


Alafu Ukiona mtu anajua formation zote za michezo na madhara yake na huyo mtu akaendelea kufanya atakavyo basi ujue yafuatayo;

1: Anazeeka Vibaya.


2: Pesa inamdanganya.


3: Ana washauri wabaya.


4: Anajiona ana nguvu wakati hana.


5: Anayo kinga fulani anayotegemea ambayo wakati huo huo uenda ika-expire wakati wowote na yeye hajui hilo.


6: Au huko UKAWA yupo kazini.


Wale wote waliokuwa wakiimba na kupiga kelele wakati akiwa ndani ya CCM wooote wale wana njaa tu na walikuwa wakiimba huku wakiangalia matumbo yao na ahadi kedekede walizopewa na kamwe hawawezi kufanya maamuzi ya kijinga ya kuhama chama. Wakihama basi watakuwa wachache.


Lowassa ni mwanachama wa kawaida kama wanachama wengine na hana madhara yoyote ndani ya CCM kama mnavyodhani sema tu ni pesa zake tu alizonazo na vyombo vya habari alivyovinunua. Kama huko UKAWA hayupo Kazini basi namuonea uruma sana kwa maana atakuwa amejiaribia maana pesa alizonazo ni kama vifaranga vya kuku na wakati wowote uenda kunguru akaja kuvichukua vyote akabaki hana kitu.


CCM ni chama chenye uzoefu mkubwa na miaka mingi msitegemee ata siku moja kwamba hawakufanya mahesabu ya madhara atakayoleta Lowassa kuhama chama cha CCM na kumbuka CCM wana advantage kubwa nyuma yao ambayo itakayowasaidia kufanya hayo mahesabu vizuri na kupata ushindi mkubwa au kumpunguza Lowassa nguvu.


Vile vile, Kwa upande wa Chadema au UKAWA, hawa ni wakuogopa kuliko chama au kitu chochote kingine, kwanini nasema hivyo? Kama juzi au jana walizungumza vibaya juu ya Lowassa kwa ushahidi leo wakimzungumzia mazuri basi napata shida kufikiria siku wakichukua nchi maamuzi yao yatakuwaje na wataendeshaje nchi kama sio kuwa Mafisadi wakubwa zaidi. Sasa najua na kuona ni jinsi gani Yesu / Issa alivyo uzwa kwa ajiri ya Pesa na Sasa ndio naona ni jinsi gani Upinzani ndani ya Tanzania ulivyokufa rasmi.


Haya ni maoni yangu tu na wala mimi SIO mwanachama wa chama chochote kile ila ukilinganisha maamuzi yaliyofanywa na UKAWA pamoja CCM (kumkubari Lowassa na mwingine kumkataa) basi kwa mtazamo wangu CCM itaendelea kutawala miaka mingi ijayo hapa Tanzania.
 
Hakuna mwana ccm alie furahi kwa maamuzi ya lowassa kuwatosa na tulitarajia hilo.

bakini na mchama wenu mfu huo,tukutane oktoba 25.

Wala sio wana ccm mana waukwel wanafurah kujenga chama kwa kufata kanuni...wahame wote waende kokote alaf chama kianze upya na watu wapya-kifup wenye kashfa wote watoke wabakie majembe,mfumo utachange tu mana wapindishaji wapo upande wa pili alaf kaz iendelee,hakuna haja ya kulumbana sana kwa swala ambalo kila mtu anaamin mtazamo wake.
 
akili,majina,tabia,hisia ,hulka huwa vinabaki constant...alafu chama ni variable. cdm ikipokea wote kutoka ccm eti ni mtaji ,sidhan kama itatoa picha nzuri. screening ifanyike ili kulinda heshma ya chama
 
Back
Top Bottom