Parapanda
Member
- May 30, 2010
- 39
- 4
Jana nimesoma habari kwenye gazeti la Nipashe kuwa, walinzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili walilizuia lori lililokuwa limebeba maiti wengi kutoka nyumba ya maiti hospitalini hapo, baada ya kutilia shaka uondoshwaji wa maiti hao. Sehemu ya habari hiyo ni hii
"lilikuwa limebeba maiti 10 ambazo zilikuwa zinaondolewa hospitalini wakati wa usiku na bila wao kuwa na taarifa.
Maiti hizo zilizuiliwa kwa muda wa saa kadhaa mpaka polisi walipoitwa kuthibitisha ukweli wake................"
"Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alisema kuwa suala hilo ni la kiutawala linaloihusu Hospitali ya Muhimbili na kwamba wao hawawezi kulitolea taarifa bali wenye mamlaka hiyo ni uongozi wa hospitali hiyo"
"Ofisa Habari wa Hospitali ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha, aliliambia NIPASHE kuwa maiti hizo zilikuwa zinapelekwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) kilichoko mkoani Dodoma".
"Aligaesha alisema kuna utaratibu ambao huwa unafanyika kwani vyuo vya tiba huomba maiti kwa ajili ya kufundishia wanafunzi wao"
"Alisema maiti ambazo huwa zinatolewa ni zile ambazo zimekaa katika chumba cha kuhifadhia maiti zaidi ya siku 14, baada ya ndugu kushindwa kujitokeza"
Na ikishafikia hapo maiti haina ndugu na imekaa zaidi ya siku hizo huzikwa na Manispaa kwa kushirikiana na polisi, alisema Aligaesha.
Naomba wenzangu mnaofahamu mnielimishe kuhusiana na jambo hilo ambalo mimi limenikera, na sioni kama ni haki kutoa maiti kwa ajili ya kujifunzia (Cadaver) kwa kigezo tu cha wanandugu kutokujitokeza kumchukua maiti yule! Najisikia vibaya kwa sababu NI HAKIKA kuwa hata mimi nitakuwa maiti wakati wangu ukifika, hata wewe.
Huo ndio utaratibu au mfumo kwa ajili ya kupata maiti kwa ajili ya wanafunzi wa tiba kujifunzia? Nijuavyo mimi, maiti za kujifunzia huwa zinatokana na ridhaa ya mtu awapo hai kutoa tamko la kukubali kuwa, atakapokufa, kiungo au viungo fulani katika maiti yake vitumike kwa manufaa ya walio hai.Kwenye nchi zingine watu wa namna hii, ridhaa yao hiyo huwa imeonyeshwa kwenye vitambulisho vyao kama Leseni ya udereva kuwa ni "Organ Donor"; ili mauti yatakapomkuta popote, mamlaka zinazohusika zifahamu kuwa alishatoa ridhaa ya namna hiyo.
Mwanadamu anastahili heshima; na hata maiti yake pia inastahili heshima vilevile. Naamini ni kinyume cha haki za binaadamu kutumia maiti yake au viungo vya maiti huyo bila ridhaa yake ambayo huitoa akiwa hai. Sipingi mafunzo ya tiba; ni mafunzo muhimu kwa ustawi mwa mwanadamu, lakini haki na heshima ya mwanadamu iheshimiwe awapo hai hata awapo maiti.
"lilikuwa limebeba maiti 10 ambazo zilikuwa zinaondolewa hospitalini wakati wa usiku na bila wao kuwa na taarifa.
Maiti hizo zilizuiliwa kwa muda wa saa kadhaa mpaka polisi walipoitwa kuthibitisha ukweli wake................"
"Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alisema kuwa suala hilo ni la kiutawala linaloihusu Hospitali ya Muhimbili na kwamba wao hawawezi kulitolea taarifa bali wenye mamlaka hiyo ni uongozi wa hospitali hiyo"
"Ofisa Habari wa Hospitali ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha, aliliambia NIPASHE kuwa maiti hizo zilikuwa zinapelekwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) kilichoko mkoani Dodoma".
"Aligaesha alisema kuna utaratibu ambao huwa unafanyika kwani vyuo vya tiba huomba maiti kwa ajili ya kufundishia wanafunzi wao"
"Alisema maiti ambazo huwa zinatolewa ni zile ambazo zimekaa katika chumba cha kuhifadhia maiti zaidi ya siku 14, baada ya ndugu kushindwa kujitokeza"
Na ikishafikia hapo maiti haina ndugu na imekaa zaidi ya siku hizo huzikwa na Manispaa kwa kushirikiana na polisi, alisema Aligaesha.
Naomba wenzangu mnaofahamu mnielimishe kuhusiana na jambo hilo ambalo mimi limenikera, na sioni kama ni haki kutoa maiti kwa ajili ya kujifunzia (Cadaver) kwa kigezo tu cha wanandugu kutokujitokeza kumchukua maiti yule! Najisikia vibaya kwa sababu NI HAKIKA kuwa hata mimi nitakuwa maiti wakati wangu ukifika, hata wewe.
Huo ndio utaratibu au mfumo kwa ajili ya kupata maiti kwa ajili ya wanafunzi wa tiba kujifunzia? Nijuavyo mimi, maiti za kujifunzia huwa zinatokana na ridhaa ya mtu awapo hai kutoa tamko la kukubali kuwa, atakapokufa, kiungo au viungo fulani katika maiti yake vitumike kwa manufaa ya walio hai.Kwenye nchi zingine watu wa namna hii, ridhaa yao hiyo huwa imeonyeshwa kwenye vitambulisho vyao kama Leseni ya udereva kuwa ni "Organ Donor"; ili mauti yatakapomkuta popote, mamlaka zinazohusika zifahamu kuwa alishatoa ridhaa ya namna hiyo.
Mwanadamu anastahili heshima; na hata maiti yake pia inastahili heshima vilevile. Naamini ni kinyume cha haki za binaadamu kutumia maiti yake au viungo vya maiti huyo bila ridhaa yake ambayo huitoa akiwa hai. Sipingi mafunzo ya tiba; ni mafunzo muhimu kwa ustawi mwa mwanadamu, lakini haki na heshima ya mwanadamu iheshimiwe awapo hai hata awapo maiti.