CONTROLA
JF-Expert Member
- Sep 15, 2019
- 6,939
- 22,989
Nilikuwa sina mpango hata wa kuandika Hii thread lakini naiandika kwa ufupi sana baada ya kupita instagram na kukutana na clip hatari za wahuni wakiwa wanahamishwa gereza huko El salvador
Kuhamishwa kwao,mikao yao yani imenikumbusha Moment hatari sana nilizowahi pitia miaka ya zamani hiyo
Gusa Link hapa chini uone watu wanavyokimbizwa mchaka mchaka
Magereza ni sehemu ambayo hakuna haki kinachofanywa kwa hao raia ndio kinachofanywa na magereza mengi nchi karibia zote sema ni siri zao hawa tu ndio wameamua kutuonyesha.
na hii imeonyeshwa ili walioko uraiani El salvador wale makundi ya wahuni wabadilike au wahame nchi maana wameonyeshwa namna kinavyonukishwa kwa wenzao.
Ukitazama hizo video utaona Baadhi ya mambo yafuatayo
KUKIMBIA
Huu ni utaratbu uliowekwa na magereza makusudi kabisa ili mfungwa asiweze au asipate muda wa kuangalia pembeni kujua gereza limejengwaje limekaaje,yani ni mchaka mchaka
KUANGALIA CHINI
Askari nao walizingatia usalama wao,hivyo unapoambiwa head down yani kichwa chini maana yake ni marufuku kumuangalia askari usoni maana huchelewi kumkariri halafu wahuni wenzako wakija ukawasimulia askari yukoje wao wakamjua wakaenda kufanya kazi ya roho mbaya huko nnje,hivyo walizingatia hilo
JINSI YA KUJIPANGA na KUKAA CHINI
Hii ni njia ambayo inatumika ili kurahisisha hesabu wakati mnahesabiwa kwahiyo kukaa chini magereza ni kauli mbiu sio ombi,na sio tu wakati wa kuhesabiwa ila ukiwa jela Kukaa chini ni 1 ya sheria, Ukiinuka ni either unaenda chooni au kuchukua chakula AU umeitwa Admission,ila huwezi kuwa ndani ya eneo la magereza halafu eti unasimama simama, huna cha kufanya tafuta sehemu kaa chini pigeni story na wenzio,ukikutwa umesimama "unalo".
KUNYOA KIPARA
Magereza kunyoa Kipara ni amri,ukienda na rasta zitadondoshwa ukienda na kipilipili watakusaidia kukishusha chini, na usifikiri kuna saloon magereza,ni Amri tu inatolewa ikifika MUDA wa kuingia kulala uwe HUNA nywele hata 1, sasa utanyolea wembe, utanyofoa nywele, utajua mwenyewe haiwahusu.
Uzuri ni kwamba jela wema hawakosekani atakuepo mmoja atakupa wembe wake utanyolea. Ndio mana nasema kila siku kama unampenda mtu wako cheza michezo yote ila usimpeleke Jela maana anaweza kwenda kuchukua ugonjwa ambao kama si wewe kumpeleka jela asingeupata.
KIFUA WAZI,KUWA WAZI JUU
Hii ni njia mojawapo ya usalama kwa wafungwa wenyewe na askari,hii imewekwa makusudi ili usiweze kuficha kitu ndani ya shati,kwahiyo ukishuka tu kwenye gari kutoka mahakamani kabla hujaingia magereza Shati unatoa, mkiingia ndani kabla hamjaingia kulala shati mnatoa yani nadahani walitamani wafungwa washinde bila mashati sema ndo hivyo tena kuna haki za binadamu.
KUKAA KARIBU KARIBU
Sio kwamba hamna nafasi ila JELA wanachofanya ni kukunyima uhuru,na hii wanaifanya makusudi ili hata ukitaka kufanya jambo utamgusa mwenzako na mtashtukiwa,maana mtatikisika kama ulitaka fanya chochote kitashtukiwa.
kwahiyo hata kama itokee gereza zima wamalize kifungo mbaki wafungwa 10 na vyumba vya kulala vipo 20,mtahukuliwa 10 mliobaki mtatafutiwa chumba kidogo chakuingia watu 8 mtawekwa nyie 10 ilitu mbanane,sheria yao iwe imekamilika,na hiii sio kwenye kukaa tu hiyo hadi kwenye kulala yani mbanano ndio kauli mbiu ya GEREZA LOLOTE.
Kwa ufupi hayo ni baadhi ya mambo na taratbu za Magereza,narudia kusema Furahia na thamini sana uhuru ulio nao maana ni zawadi kubwa sana Uliyo nayo ambayo yawezekana hujaijua.
usije ukakubali awae yeyote akakupokonya zawadi ya uhuru wako ni heri ulale njaa,utembee peku,ukose pakulala lakini uwe huru kwenda na kufanya lolote. Magereza ni DUNIA nyingine kabisa tofauti na hii tuliyopo sasa.
Nimewakumbusha wote ambao labda mmejisahau, epuka vitendo visasi vitakavyokusababishia ukapokonywa zawadi kubwa kuliko PESA na MAJUMBA na UFAHARI wowote ule kama UHURU.
UHURU hauna cha kulinganishwa nacho,Uhuru ni zawadi itunze ithamini na iheshimu.
#WASIKUZOEEElakini
Isikieni Magereza/JELA kwenye mitandao tu na kwenye media ila Usiombe wala usijaribu kunusa hayo maeneo.
Kuhamishwa kwao,mikao yao yani imenikumbusha Moment hatari sana nilizowahi pitia miaka ya zamani hiyo
Gusa Link hapa chini uone watu wanavyokimbizwa mchaka mchaka
Magereza ni sehemu ambayo hakuna haki kinachofanywa kwa hao raia ndio kinachofanywa na magereza mengi nchi karibia zote sema ni siri zao hawa tu ndio wameamua kutuonyesha.
na hii imeonyeshwa ili walioko uraiani El salvador wale makundi ya wahuni wabadilike au wahame nchi maana wameonyeshwa namna kinavyonukishwa kwa wenzao.
Ukitazama hizo video utaona Baadhi ya mambo yafuatayo
KUKIMBIA
Huu ni utaratbu uliowekwa na magereza makusudi kabisa ili mfungwa asiweze au asipate muda wa kuangalia pembeni kujua gereza limejengwaje limekaaje,yani ni mchaka mchaka
KUANGALIA CHINI
Askari nao walizingatia usalama wao,hivyo unapoambiwa head down yani kichwa chini maana yake ni marufuku kumuangalia askari usoni maana huchelewi kumkariri halafu wahuni wenzako wakija ukawasimulia askari yukoje wao wakamjua wakaenda kufanya kazi ya roho mbaya huko nnje,hivyo walizingatia hilo
JINSI YA KUJIPANGA na KUKAA CHINI
Hii ni njia ambayo inatumika ili kurahisisha hesabu wakati mnahesabiwa kwahiyo kukaa chini magereza ni kauli mbiu sio ombi,na sio tu wakati wa kuhesabiwa ila ukiwa jela Kukaa chini ni 1 ya sheria, Ukiinuka ni either unaenda chooni au kuchukua chakula AU umeitwa Admission,ila huwezi kuwa ndani ya eneo la magereza halafu eti unasimama simama, huna cha kufanya tafuta sehemu kaa chini pigeni story na wenzio,ukikutwa umesimama "unalo".
KUNYOA KIPARA
Magereza kunyoa Kipara ni amri,ukienda na rasta zitadondoshwa ukienda na kipilipili watakusaidia kukishusha chini, na usifikiri kuna saloon magereza,ni Amri tu inatolewa ikifika MUDA wa kuingia kulala uwe HUNA nywele hata 1, sasa utanyolea wembe, utanyofoa nywele, utajua mwenyewe haiwahusu.
Uzuri ni kwamba jela wema hawakosekani atakuepo mmoja atakupa wembe wake utanyolea. Ndio mana nasema kila siku kama unampenda mtu wako cheza michezo yote ila usimpeleke Jela maana anaweza kwenda kuchukua ugonjwa ambao kama si wewe kumpeleka jela asingeupata.
KIFUA WAZI,KUWA WAZI JUU
Hii ni njia mojawapo ya usalama kwa wafungwa wenyewe na askari,hii imewekwa makusudi ili usiweze kuficha kitu ndani ya shati,kwahiyo ukishuka tu kwenye gari kutoka mahakamani kabla hujaingia magereza Shati unatoa, mkiingia ndani kabla hamjaingia kulala shati mnatoa yani nadahani walitamani wafungwa washinde bila mashati sema ndo hivyo tena kuna haki za binadamu.
KUKAA KARIBU KARIBU
Sio kwamba hamna nafasi ila JELA wanachofanya ni kukunyima uhuru,na hii wanaifanya makusudi ili hata ukitaka kufanya jambo utamgusa mwenzako na mtashtukiwa,maana mtatikisika kama ulitaka fanya chochote kitashtukiwa.
kwahiyo hata kama itokee gereza zima wamalize kifungo mbaki wafungwa 10 na vyumba vya kulala vipo 20,mtahukuliwa 10 mliobaki mtatafutiwa chumba kidogo chakuingia watu 8 mtawekwa nyie 10 ilitu mbanane,sheria yao iwe imekamilika,na hiii sio kwenye kukaa tu hiyo hadi kwenye kulala yani mbanano ndio kauli mbiu ya GEREZA LOLOTE.
Kwa ufupi hayo ni baadhi ya mambo na taratbu za Magereza,narudia kusema Furahia na thamini sana uhuru ulio nao maana ni zawadi kubwa sana Uliyo nayo ambayo yawezekana hujaijua.
usije ukakubali awae yeyote akakupokonya zawadi ya uhuru wako ni heri ulale njaa,utembee peku,ukose pakulala lakini uwe huru kwenda na kufanya lolote. Magereza ni DUNIA nyingine kabisa tofauti na hii tuliyopo sasa.
Nimewakumbusha wote ambao labda mmejisahau, epuka vitendo visasi vitakavyokusababishia ukapokonywa zawadi kubwa kuliko PESA na MAJUMBA na UFAHARI wowote ule kama UHURU.
UHURU hauna cha kulinganishwa nacho,Uhuru ni zawadi itunze ithamini na iheshimu.
#WASIKUZOEEElakini
Isikieni Magereza/JELA kwenye mitandao tu na kwenye media ila Usiombe wala usijaribu kunusa hayo maeneo.