Fununu: Lema kuirithi mikoba ya Mbowe!

Fununu: Lema kuirithi mikoba ya Mbowe!

HAMY-D
Kila nikisoma thread zako naona zote ni comic. Na zote zinapata traffic ya kutosha. Wazo, najua wewe ni fisadi au unalishwa na mafisadi lakini unaonaje ukaachana na ufisadi halafu ukafungua blog yako. Utapata watu wa kutosha kutengeneza hela kwa jasho lako. Mimi binafsi nitakusaidia ku-set blog.

Una ujuzi mkubwa sana wa kutunga fiction.
 
Last edited by a moderator:
Mbona mimi nimezaliwa Kilimanjaro na ni Mrangi,mbona ccm mnawachukia sana wachaga?

CCM haiwachukii wachagga ila ni unafiki!
Ingaliwachukia wachagga Dr. Mathayo David, Anne Kilango, Aggrey Mwanri, Cyril Chami wasingalikuwa wabunge kupitia CCM
Ili uwe mwa CCM mzuri, unatakiwa kufuzu kwa kiwango cha juu elimu ya UNAFIKI kama HAMY-D
 
Inawezekana hata katika familia yake huyu Jamaa anaishi kwa fununu.Hii ni hatari sana
 
Acha kumkosea Subhana kwa kumhusisha na unafiki wenuu na uchumia tumbooo... Unaongeaa vitu bilaa dataa na unaropoka kwa kutumia sauti kubwa bila kuwa na hojaaa..... Rudi kwenye statistics, moshii Vijijini ni jimbo ambalo asilia tisini ya wakazi wake ni Wachagga na linaongozwa na Cyrialis Chamii ambaye ni mbunge wa CCM je hawa wachagga waliokichagua chama tawala unawaambiaje?!!! Agrey Mwanri ni mbunge wa CCM Siha je unawaambiaje wachaga waliomchaguaa kupitia CCM.. Rombo ilikuwa ni ngome ya CCM na haijawahi kuongozwa na upinzani hadi pale CCM walipojaribu kumbeba fisadi Mramba ndio jimbo hili likaangukia upinzani, je salam zako kwa uzalendo wa watu wa Wachagga wa Rombo kwa CCM kwa miaka yote hiyo unaukebehii?!!!.. Majimbo ya uchaguzi Mkoa wa Kilimanjaro yapo takribani Nane ila ni majimbo ya Hai (Mbowe - CDM), Rombo (Selasini - CDM), Moshi mjini (Ndesamburo- CDM) na Vunjo (Mrema-TLP) ndio yapo chini ya upinzani mengine manne yao CCM.. Je kwa uwiano huu nani mwenye nguvu zaidi kisiasa... (CCM 4, CDM-3, TLP 1)?!!!

Rusi tena kwenye takwimu tujirishishe wabunge wa chadema wametoka mikoa mbalimbali ya tanzania kutoka Kigoma kupitia Singida mpaka Dar. Kutoka Mwanza Shinyanga, Mbeya, Mbozi mpaka Sumbawanga., kutoka Mara, Kilimanjaro Arusha mpaka Iringa.. na madiwani ndio wametapakaa zaidi karibuni mikooa yotee.. Vyama vingi vya upinzani vina uwezo mdogo kifedha hivyo vinakosa uwezo wa kuendesha upinzani nchi nzima hivyo huwekeza nguvu zake zaidi pale vilipo na uhakika wa kushindaa lakini haimaanishi kwamba hivi ni vyama vya kikabila hapana.. hivi vipo kwa mujibu wa sheria na ni taasisi kama taasisi nyingine. Kurundikana kwa watu wa nasaba moja kwenye chama si jambo la ajabu maana hata CCM amacho ni chama Kikongwe wamejaa wengi na familia zao na haijawahi kuwa nongwa... Nenda hata katika moafisi mengi utakuta halamsahauri ya Kyela wamejaa wanyakyusa je huu ni ukabila!!? Halmashauri ya Kigoma wamejaa wahaa je huu ni ukabila?!! Halmashauri ya Muleba wamejaa wasukuma je huu ni ukabila?!!!
Tujiulize viongozi na wakuuu wa vyama wanapatikana kwa kuchaguliwa, je swali ulitaka nani awe mwenyekiti na kama angekuwa ni ------ weewe usingekuwa na shida na kabila lakee??? Je ambao sio wakere unawaambiaje wao ni wajinga kuongozwa na ------?!!! Unaweza kuwa na wenyekiti wa ngapi wa CCM ili awakilishe makabiala yote na dini zote!?
Wabunge hupatikana kwanza kwa juhudi binafsi za mgombea, uwezo wakee na kukubalika katika sehemu anayogombea na mwisho kuchaguliwa na wapiga kuraa?!!! Sasa kama Mtwara au Tanga hakuna mgombea ubunge kupitia CCM aliyejijenga na akasimama na kushinda hilo kosa linakuwaje liwe ni tatizo kwa yule aliyeshinda kupitia chama hicho huko Moshi au Arusha?!!! Mbowe au Lema ndiye aliyekukosesha wewe fursa ya kugombea na kushinda ubunge kupitia chadema kupitia CDM huko Ludewa au Rufiji?!!! Hao wambunge wanotoka mikoa mingine unawaambiaje, walishinda kwa sababu wao ni wachaggaa?!!! Wakina ZItoo, Sugu, Msigwa, Shibuda, Machemli, Said Harfi hawa wanatoka kilimanjarooo.??
Enzi za Nyerere viongozi walichaguliwa kwa utendaji wao na si ajabu ilitokea kwa bahati nzuri au mbaya unakuta kuna ratio kubwa ya waislam au wakristo katika baadhi ya ofisi je huu ulikuwa udinii??!!! Je ni kwanini sasa kila kituu tunachokiangalia tunakitizama kwa miwani za udini, ukabila na uchama?!!!
Bahati mbaya viongozi wengi wa CCM wameingia kwenye siasa hizi za maji taka, na wamesahau misngi iliyowekwa na Mwl. Nyerere. Kila mnapozidiwa hoja mnatafuta majibu mepesi kwa kuangalia udini, ukabila na uchama.. Mnasahau kabisa hii nchiii ni ya watanzania na hizo haki nyingine zinakuja baadaye

Kumtetea HAMY-D lazima na wewe uwe na sifa hizi tatu moja lazima unaamini katika chama kushika hatamu na hakuna chama kingine zaidi ya CCM. Pili mfumo Ukiristo ndio cha matatizo yako na hakuna dini nyingine zaidi ya dini yakoo.. Tatu watu wote wa kaskazini especially wachagga ni chanzo cha matatizo yote na hawastahini kupewa nafasi yeyote ile katika nchiii.. Hii ndio misingi ya hoja za HAMY-D hawezi kucheza mbali na hapaaaa atabadilisha sura lakini upeo wake huishia hapa hapa... Na watu wa aina hiii mpo wengi tuuu ambao kila tatizo mnaweza kulitatua kwa kuangali pande tatu UKIRISTO, UCHAGGA, NA UPINZANI (CHADEMA)...
Ili tuendelee tunahitaji vitu vinne watu, ardhi, siasa safii na uongozii boraaa.. Nyie mnaa tumiaa kauli hii, ''ili tuendelee tunahitaji, Wenzetuu (mafisadi) na sio waxchagga, ardhii, siasa chafuu na bora viongoziii...''

WEWE NA HUYO HAMY-D NI WANAFIKI NA WABAGUZI WAKABILA NA WADINI

poa tu lakini habari ndio hiyo.Chadema ni chama cha wachaga kwa jinsi kinavyoendeshwa.Mwaka 2005 karibu 100% ya wabunge viti maalum walikuwa wachaga,baada ya kelele ndio 2010 wakachomekachomeka vyasaka,hili liko wazi ndugu usibishe.takwimu zako ziko sawa lakini kwa hili kubisha ni unafiki.zitto licha ya kukipa umaarufu chama anaonekana kama kinyesi tu huku makanjanja akina lema wanaoneka mashujaa,aibu kwel
 
WanaJF!

Ni wazi kuwa wananchi na hasa wapenzi wa CHADEMA wangependa kujua ni nani kati ya viongozi waliopo mwenye nafasi kubwa ya kuongoza chama hicho kwenye nafasi ya uenyekiti katika ngazi ya taifa.

Ni ukweli kuwa CHADEMA kwa sasa ni chama kikubwa cha siasa nchini, hivyo kwa hadhi hiyo uchaguzi wake ni lazima uwe na hamasa kulinganisha na chaguzi za vyama vingine, hivyo ni haki kwa wananchi kuwa na shahuku na uchaguzi wa CHADEMA.

Katika penya penya zangu na uchunguzi mkubwa nilioufanya kwenye chama hicho, nimegundua kuwa ndani ya CHADEMA kwa sasa ni bwana Godbless Lema ndiye mwenye nguvu na nafasi kubwa ya kuwa mwenyekiti wa CHADEMA taifa.

Itakumbukwa kuwa Godbless Lema ni mbunge wa Arusha mjini, na pia mzaliwa wa Kilimanjaro na ina semekana ana ujamaa na bwana Mbowe, hivyo kwa maelezo haya ni wazi kuwa ametimiza vigezo vikuu vya kuwa mwenyekiti wa CHADEMA taifa.

Aidha, ndugu Lema kwa sasa anapigiwa 'promo' na mwenyekiti wa sasa, bwana Mbowe, kwa kuhakikisha ana ambatana nae kwenye mikutano mikubwa kwa midogo ya CHADEMA, na pia bwana Mbowe bila kificho uwa ana msifu Lema kuwa ndiye 'jembe' la CHADEMA.

Lakini vilele ningependa ieleweke kwamba, katika mchakato wa kumpata mwenyekiti au kiongozi mwingine yeyote ndani ya CHADEMA kwenye ngazi ya taifa, vigezo vifuatavyo sio vya muhimu sana;

i) ELIMU, angalau mwombaji awe na elimu ya kidato cha nne, nadhani hii bwana Lema atamudu.

ii) UZOEFU, ni CHADEMA pekee ambayo utoa nafasi kwa mtu kuwa kiongozi pasipo kukitumikia chama kwa kipindi cha angalau miaka mitatu.

iii) MAADILI, hili halizingatiwi kabisa, na imeonekana likiwekwa kama kigezo cha kupata kiongozi ndani ya CHADEMA ni wengi watakosa nafasi.

Hivyo basi, ni wazi kuwa kama sifa tajwa hapo juu zimepuuzwa na CHADEMA katika mchakato wa kumpata mwenyekiti wa chama hicho, ni ukweli usio pingika kuwa Godbless Lema ana andaliwa kuirithi mikoba ya Mbowe.

Hahahahahahahaha Hamy umenivunja sana mbavu. Yaani kiki chama wanaachiana wavuta bangi tu wakiongoze.

Hhahahahahahahahaah
 
Hamy- D,
Mara zote ninaposoma post zako huwa nakuhurumia sana kwani kazi uliyopewa ya kuidhoofisha Chadema ni ngumu sana kwako, unatumia muda mwingi kushawishi watu wa humu JF wakati chadema wao wanakula vichwa vya wapiga kura huko vijijini, plse change your tactics!
 
Vipi kijana wa hayati mwl Nyerere upo?

Nadhani kwa jinsi CHADEMA wanavyo recruit viongozi wao hata wewe unaonyesha una sifa za kuwa kiongozi ndani ya CHADEMA.

Kuna hii ishu ya kusimamia uongo mpaka uonekane ukweli; nadhani kwa jinsi ulipotosha watu humu kuwa wewe ni kijana wa hayati mwl Nyerere na baadhi wakaamini, basi wewe ni tunu ndani ya CHADEMA.

Lini CHADEMA wame recruit viongozi....? Hivi karibuni CHADEMA walitangaza nafasi za kazi majimboni,naomba ujaribu kuzifuatilia then uone kama uhalisia wake una reflect what you chose to see.
 
Nani kakuambai kuwa CDM wanrithishana uongozi kama nyie magamba mfanyavyo? mfano: utakuta mtu kidingi kinoma (kidevu kimejaa ukurutu/ukoko wa bagia) eti mnantuambia katibu wa "youngs" wa chama ..mmmhhh..damn ,...cdm katiba ya wanachama ndo " the hub of decision". nadhani utakuwa umepata somo japo kidogo.
 
Hakuna cha kuangaika na CHADEMA, mimi kama mpenda amani sina budi kufatilia chaguzi za ndani za CHADEMA kwa lengo la kujua ni nani atakae kuwa mwenyekiti, huyu wa sasa zaidi ya kusababisha mauaji na uvunjifu wa amani kwa kiasi kikubwa hapa nchi, hakuna la maana alilofanya. Je, mkimpa Lema itakuwaje?

Unaposema amesababisha mauaji na serikali haijamchukulia hatua yeyote....ni kumdhalilisha Rais na mawaziri wake wote kuwa ni dhaifu....mtu anaweza kuharibu na kupoteza uhai wa watu bila kuchukuliwa hatua yeyote....ni sawa na kusema tuna serikali legelege na Rais dhaifu.
 
Daaaaah
Nimeishia kusoma taarabu za Yericko, Hamy-D na Mwanadiwani.
CCM na CDM ni kama ulimi na mimate
 
Hamy- D,
Mara zote ninaposoma post zako huwa nakuhurumia sana kwani kazi uliyopewa ya kuidhoofisha Chadema ni ngumu sana kwako, unatumia muda mwingi kushawishi watu wa humu JF wakati chadema wao wanakula vichwa vya wapiga kura huko vijijini, plse change your tactics!

CCM hawajawahi kufikiria kubadilisha tactics hata siku moja. Old dog, old tricks.
Zero efficiency. Kulinda halindi wala kushambulia hashambulii tena. Amebaki kubweka tu
 
fallacy arguement from narrow and simple minded.
 
Hakuna cha kuangaika na CHADEMA, mimi kama mpenda amani sina budi kufatilia chaguzi za ndani za CHADEMA kwa lengo la kujua ni nani atakae kuwa mwenyekiti, huyu wa sasa zaidi ya kusababisha mauaji na uvunjifu wa amani kwa kiasi kikubwa hapa nchi, hakuna la maana alilofanya. Je, mkimpa Lema itakuwaje?
Hebu jaribu kueleweka, vinginevyo unahitaji kupimwa akili. Unasema: "Hakuna cha kuangaika na CHADEMA", lakini ndiyo kwanza unahangaika. Kila ukianzisha uzi wako unahangaika tu na Chadema. Unadai: Mbowe "hakuna la maana alilofanya", lakini unakiri kuwa Chadema ni chama kikubwa.

Kama hakuna alilolifanya, chama kimekuwaje kikubwa kama mwenyekiti wake hakushiriki au kushirikisha wengine ndipo chama kikawa kikubwa? Mbowe amesababisha "...mauaji na uvunjifu wa amani." Aliwezaje kufanya hivyo katika serikali SIKIVU na MAKINI kama ya CCM? Au huko ni kukiri kuwa serikali ya CCM ni dhaifu ndiyo maana Mbowe anafanikiwa kusababisha "mauaji na uvunjifu wa amani"? Mwisho unauliza: "Je, mkimpa Lema itakuwaje?" Hapa ndipo patamu zaidi na ndipo panapokutisha zaidi kwa sababu Lema siyo mwoga. Ukitaka kujua hivyo kamuulize Magessa Mulongo kule Arusha atakupa jibu. Lakini jawabu langu kwa swali lako la mwisho ni rahisi sana. Kama Lema akiwa mwenyekiti wa CHADEMA, Tanzania nzima itajitambua kama Arusha walivyojitambua. Period. Na ndipo utakaposikia si 4-0 tena, bali TSUNAMI la nchi. Dada HAMY-D najua wewe hutanielewa kwa sababu kwanza huna uwezo wa kuelewa na hata kama ungekuwa nao, hauko tayari kuelewa. Akili iliyopumbaa ndivyo ilivyo.
 
Ni kweli Lema anaaminika sana miongoni wa wote, si unaona yeye ndiye anayepewa kazi ya kubeba SADO za kukusanyia sadaka mikutanoni.
 
Back
Top Bottom