Fundi hata umbane vipi akitaka kukuibia atakuibia tuu

Hizi changamoto za kusumbuana na mafundi mnazitaka wenyewe client, Siku hizi kuna makampuni mengi tu class VII wanajenga hadi nyumba za viwili, kaa nao chini mpatane muingie mkataba, mkiendelea kujenga ki local hvo mtapigwa sana na nasema mtaendelea kupigwa tu!
Hata hawa wa makampuni ni wezi tu kiufupi hamnaga fundi asiekua mwizi muache unoko matajiri
 
Kuna jamaa yangu alikuwa kwenye ujenzi wa nyumba wake,jamaa kauzu sana mtu wa kufuatilia kila sent yake imetumikaje. Sasa akamwambia fundi amwandikie na kumpigia hesabu idadi za materials kama mbao na bati fundi alipomaliza jamaa akashika karatasi akamwambia fundi twende kununua vifaa. Fundi akamshawishi ili kuokoa gharama issue ya mabati waende Kiwandani kabisa. Jamaa akapokea wazo wakaenda Kiwanda kimoja kipo Nyerere Road,jamaa akatoa oda pale na kulipa kila kitu then wakapewa mzigo wakaondoka nao.

Sasa baadae fundi akafanya kazi yake akamaliza,sasa ikaja kuonekana kuwa kuna mabati yamepungua na jamaa akawa wakati ule hana hela,akaanza kujiuliza imekuwaje bati zipungue na hesabu ilikuwa sawa. Wakati huo fundi yupo mkoani kwenye kazi nyingine,jamaa ikabidi aende pale kiwandani kuulizia kulikoni,jamaa ndio wakamsanua kuwa fundi kakupiga,jamaa kupiga hesabu vizuri fundi alimpiga kama 2ml. Jamaa akachoka na hasira juu,kumbe pale kiwandani yule fundi anafahamika sana na anawapelekea wateja wengi sana,kwa hiyo ana signals zake anazowapa wale wafanyakazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hujasema alimuibiaje hapo kiwandani,kama walienda kununua bati mia ina maana walichukua bati pungufu?

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
 
Hawa jamaa dawa yao ni kujenga nao urafiki na kama ikiwezekana hata msosi wapikie😁hapo kiasi fulani utapunguza mipango ya upigaji,ukisema uwabane sana utapotea maana jamaa wana mbinu nyng za upigaji
hii mbinu maza angu huwa anaitumia sana,huwa analeta wafanya usafi wa mazingira kulima,kufyeka,kufagia ,kuchoma moto taka nk
sasa wakifika anawapa unga,mboga nk,matokeo yake jamaa hufanya kazi kwa weledi mno tena kwa gharama ndogo
 
Habarini wakuu,

Fundi yeyote ana taaluma ambayo wewe huna jifunze namna ya kuishi na fundi kupunguza chances za kukuibia

Fundi yeyote yule unapo mpa kazi mpe uhuru wa kuifanya ile kazi cha muhimu ni kuzingatia ubora wa kazi yako
Fundi asipokuibia hela ,atakuibia materials, asipo kuibia materials atakuibia Muda wako

Huwa naona watu wengi sana wanapoteza muda kufuatana na mafundi especially hawa wa buildings works km carpenter, painter,plumber, electrical & air condition technicians ...n.k
Lakini pamoja na kuwafuatilia hatua kwa hatua bado wanaendelea kuibiwa pasipo kujua ..kwakua lazima tukubali kuwa fundi yeyote amekuzid knowledge ya hiyo taaluma yake ..hvyo bhac ,iwe Kampuni ,Taasisi au Mtu binafsi ..unapokua na kazi yako ..focus zaidi kwenye ubora wa kazi na sio fundi um'bane vipi ili asikuibie

Nimeona mifano mingi sana ya watu wanaolalamika kila siku kuibiwa na mafundi lakini ukifuatilia kwa makini ni watu wanao wabana sana mafundi wakat wa kazi zao lakini ukweli ni kwamba kadri unavozidi kumbana fundi ndo unamuongezea nafasi ya kukuibia

Kwa upande wa hela fundi kukuibia anaweza akataja bei tofaut na bei elekezi..au kazi ambayo angeweza kuifanya kwa lisaa limoja anaweza akaifanya kwa masaa matano ili uone ni kazi complicated umpe hela nyingi

Kwa upande wa materials hapa ndo wanatupigaga sana hususani hv vitu vya spare iwe vyombo vya usafiri, vifaa vya umeme,bomba ,Ac nk hapa hata uwe unajua bei ya kila kitu anaweza akakudanganya kitu flani kimeharibika ni cha kubadilisha kwakua hujui chochote ukimpa hela tayari anakua ameshakupiga hata ukitaka recept za EFD zinanunuliwa..so sio big deals..

Kwa upande wa muda hapa mara nyingi n kwa mafundi walio ajiriwa kwenye makampuni au taasisi ambazo nature ya kazi zao ni za ku move kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine hapo watakua wanatumia muda wa ofisi kufanya kazi zao binafsi

Hebu kila mmoja aelezee mbinu anazozijua ambazo mafundi wanatumia kutuibia kila siku ili angalau tujifunze
Umeongea kweli tupu fundi unatakiwa umchukulie kama rafiki yako ukae nae unywe nae bia atakupna mshua hawezi kukupiga!
 
Unaweza kumbana na asiibe,Mimi nilikuwa na Jenga,mafundi hasahasa huiba cement,Mimi nilinunua idadi ya cement aliyosema Kisha Ile mifuko ya cement niliiwekea alama ndogo Sana ya sili,ni ndogo Sana na nikimuomba fundi anihifadhie mifuko yote atakayo itumia,Nina kazi nayo muhimu,nikiporudi nilikuta Kati ya mifuko mitupu aliyoniwekea mitatu haikuwa yangu,means alichukua mifuko mitupu mingine akaniwekea akasepa na na cement mifuko 3 nilimuomba tu fundi naomba cement yangu,na kweli alirudisha

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Utaibiwa tu hata ufanyeje.

Nina WORKSHOP ya fabrication ya vyuma na Welding in general

Sasa wale madogo wako pale mbinu zao zote za upigaji nimeshazijua, mfano mteja anataka atengenezewe kitu, atatengenezewa QUOTATION ya vyuma vizito kwa thickness za milimita, lakini linapokuja suala la kufabricate unatengenezewa chuma chepesi, kama ilitakiwa itumike Round pipe ya mm2 inchi moja na nusu inayouzwa elf 55, utatengenezewa ya mm1 inayouzwa elfu 35, hiyo 20 ya kila pipe kama ziko kumi 200,000 ishaibwa.

Kama mteja ni king'ang'anizi wa kuongozana Hardware anapigwa kwa MEASURING TAPE, yaani hapa material yanazidishwa kwenye QUOTATION, idadi iliyozidi inarudishwa hardware kwa bei pungufu, ukileta mtu wa kusimamia Chuma zinakatwakatwa zitauzwa kama offcuts. ukitaka ufanyiwe kazi site kwako bei inaongezeka.

Sasa kuna soo walilifanya mpaka jamaa (Mteja) akakoma, jamaa alikuwa anakuja anawachukua WORKSHOP wakapime kazi, alafu kazi anapewa fundi mwingine sababu ya bei ya hao madogo, jamaa alirudi kwa staili ile kama mara tatu, kila wakipima kazi,kazi anapewa fundi mwingine. Siku akaja akawachukua hadi site alikuwa anajenga guest, madogo wakapima grills(madirisha) wakaandika vipimo vyao in vice-versa kwa makusudi kabisa, urefu ukawa ndo upana na upana ukawa ndo urefu,wakampa vipimo, akasema atakuja kuwachukua workshop wakafanye ile kazi kumbe anaenda kumpa fundi wake vile vipimo achome zile grills. fundi wake akachoma zile dirisha kwa vipimo alivyopewa. kwenda kuzifitisha ikawa kizaazaa, dirisha hazifiti, jamaa alikoma kwa ujuaji wake.

NB:Kumtoa fundi ofisini kuna bei yake



Sent using Jamii Forums mobile app
 
HATA SIKU MOJA USIENDE DUKA ANALOKUPELEKA FUNDI KUNUNUA MATERIAL KULE ASHAPATANA NA MWENYE DUKA KUNA HELA YAKE HAPO MZIGO WA MIL 2 FUNDI KUNA LAKI 3 AU TANO YAKE HAPO MIMI KWENYE UJENZI WA NYUMBA YANGU KILA KITU NILINUNUA MIMI KWA MFANO NONDO MM 12 ZINAHITAJIKA LABDA 100 NAENDAMWENYEWE KWA MRUSI KAMAKA NAPAKIA MZIGO NAWEKA STOO SIKU YA KAZI FUNDI ANAHITAJI NONDO NAMAPA SITOKI SITE NAHAKIKISHA ZOTE ZIMEKATWA ZINATUMIKA UKIANZA UJENZI SHINDA STE KAMA NI MFANYAKAZI CHUKUA LIKIZO KUNA FUNDI MMOJA ALIPELEKA KUNUNUA JERETA KUME KASHAPIGA SIMU JENERETA LLA MIL 2 FUNDI KASEMA NIAMBIWE MIL 3 KUFIKA DUKN MWENYE DUKA NAMFAHAMU NIKAZUGA KAMA HATUJUANI FUNDI MIMATE INAMTOKA KUNISHAWISHI JAMAA KANITUMIA SMS NJOO KESHO ACHANA NA FUNDI WAKO ANAKUPIGA MZIGO SIO BI HIYO
Hakuna.ujanja siumewasikia wanazengo asipokuibia atakutia hasara
 
Lakini huu ni uhuni, mafundi waache hizi za upigaji wa kijinga, yeye anapotaka kupiga pesa ya bosi wake hajui kamba mwenzake ame-hustle kiasi gani kuipata hiyo pesa.

Halafu hiyo kazi unayofanya unalipwa wizi wa nini tena. Ndo maana mafundi njaa njaa hawa hawana maisha ya maana japo wanafanya kazi za pesa nyingi.
Mkuu kazi yamilioni unataka kwa laki
 
Hizi changamoto za kusumbuana na mafundi mnazitaka wenyewe client, Siku hizi kuna makampuni mengi tu class VII wanajenga hadi nyumba za viwili, kaa nao chini mpatane muingie mkataba, mkiendelea kujenga ki local hvo mtapigwa sana na nasema mtaendelea kupigwa tu!
Hawa tena ndio wanakufumua kishenzi maana wako kibiashara zaidi
 
Back
Top Bottom