Wana JF poleni na majukumu.
Nina rafiki yangu wa karibu sana, ana mke na Mtoto 1 Yuko STD 5 boarding, Shemeji yangu Mashallah amejaaliwa sector zote, hawajajaaliwa kupata Mtoto mwingine, tatizo limejitokeza jumamosi iliyopita, rafiki yangu hata tabia ya kushika simu ya mke wake, siku hiyo jamaa alikuwa sebuleni na shemeji Yuko jikoni japo simu ameacha sebuleni, mara msg whatssap ikaingia jamaa akajikuta anaichukua simu na kufungua msg, kwa jina na Husna japo picha ya prifile niya kiume, ''honey nimeku miss kama Jana hatukuwa pamoja, njoo basi Hunters tupate wine niko alone, jamaa yangu akaishiwa nguvu, ila akaijibu! '' Nakuja sweetheart' muda huo huo akamwambia mke wake watoke kuna emergency,wakatoka mpaka block 40, akachukua vijana 3, wakati huo alikuwa ameshanitaarifu, ndiyo wakaenda Hunters, kufika jamaa akamwambia mke wake atangulie ndani wanamaongezi, alipoingia ndani kutafuta pa kukaa, jamaa akamuona akawa anamuita '' honey niko hapa njoo'' jamaa nao wakawa wamefika, ikawa ugonvi kumpiga jamaa, ila nikawa nimefika nikaamulia japo jamaa alikuwa kaumizwa kidogo, ktk kumhoji jamaa alionekana hana makosa maana aliambiwa hajaolewa, mke alikiri kumwambia hivyo, ala anaomba msamaha, unamshauri vipi ndugu yangu?