FT: Ligi Kuu Bara: Mtibwa Sugar 0-1 Yanga : Uwanja wa Manungu : 31/12/2013

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Huu ni mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa Manungu Mkoani Morogoro, Mtibwa wakiwa wageni.

Mtibwaa.JPG

Kikosi cha Mtibwa Sugar
Yanga.jpg

Kikosi cha Yanga kwa ajili ya mchezo huo


Mchezo unatarajiwa kuanza muda wowote kuanzia sasa
Mchezo umeanza
3' Umeanza kwa kasi ndogo, Yanga wanamiliki mpira muda mwingi
5' Azizi Ki anapata nafasi, shuti linapaa juu ya lango
10' Yanga wamepata kona mbili lakini hawajazitumia vizuri
21' Bado hakuna goli, timu zinapeana zamu kumiliki mpira
26' Azizi Ki anafunga kwa shuti la faulo
Kipa wa Mtibwa ni kama alizubaa na mpira kumgonga kisha kuingia wavuni
30’ Mtibwa wanaendelea kujipanga taratibu
40’ Mtibwa wanafika langoni kwa Yanga lakini wanakosa umakini
42’ Shuti la Ismail linatoka nje ya lango la Yanga
44’ Mayele alamanusura awalize Mtibwa lakini wanawahi kuokoa
45’ Yanga wanapata faulo karibu nae neo lilelile alilofunga Azizi Ki
Faulo ibapigwa, kipa anadaka

MAPUMZIKO

Kipindi cha pili kimeanza

46’ Mayele anawapa kashkashi walinzi wa Mtibwa
48’ Yanga wanapata kona ya tatu lakini haizai matunda
52’ Krosi ya Moloko inatoka nje
62' Mtibwa Sugar wanapata nafasi nzuri shuti linapaa juu ya lango
72' Yanga wanapata kona, hii ni ya sita kwao, lakini inaokolewa
90' Mchezo umebalansi, timu zinapeana zamu kuuchezea mpira.
90' Zinaongezwa dakika 3 za nyongeza

Full Time
 
Back
Top Bottom