From Zanzibar: Kura za Maoni Shwari!

From Zanzibar: Kura za Maoni Shwari!

Samahani wakuu zangu nimeingia katikati pasipo kufuatilia mwanzo wa hizi kura za maoni..Ningependa kujua NDIYO inasimamia nini na HAPANA inasimamia nini..
Ukisema ndio,maana yake unaunga/unataka serikali ya umoja wa kitaifa kifupi SUK na ukisema hapana,maana yake atakayeshinda ktk uchaguzi mkuu ujao hata kwa kura kiduchu basi aunde serikali peke yake bila kumshirikisha mwenzaka a.k.a mpinzani wake.
 
Kuna mtu kanitumia sms hapa ananiambia NDIYO ni aslimial 80%
 
Bububu - Ndio: 4978 Hapana: 1622

M/Kwerekwe - Ndio: 3017 Hapana: 2174
Kikwajuni –Ndio: 3326 Hapana: 2131

M/kwerekwe ni jimbo alilokuwa akilishikilia waziri kiongozi Shamsi Vuai Nahodha wamepiga NDIYO.

Jimbo la Kikwajuni,limepiga NDIYO, ambalo saivi lipo katika kinyan'nganyiro kikali kwa kiti cha ubunge kwa tiketi ya CCM...ambalo pamoja na wengine yumo N/Katibu Mkuu wa CCM Z'bar, Saleh Ramadhan Ferouz, ambaye pia ameteuliwa hivi karibuni kuwa mjumbe wa BLW, yumo Hamad Yussuf Masauni, bosi wa zamani wa UVCCM ambaye ameshinikizwa na wazee na vijana wa jimbo agombee kumkomoa Ferouz anayedaiwa kumjengea zengwe la kutimuliwa UVCCM.
 
Kuna uelekeo huo, dakika chache zijazo Pasco atatujuza kilichojili
Thanks Invi, na wana JF wengine,
Usiku ulikwenda vizuri, night life ya ZnZ bombo, watoto wa kiTanga wanaharibu haswa usiku pale wanapo-pose kama Wanzanzibari kuvaa vinguo vya ajabu ajabu, wengine tushaizoea Zanzibar, ushungi hata kwenye mengineyo.

Tuache hayo, matokeo yanafuatia.
 
Kwahani na Amani wamepiga hapana. Mji Mkongwe 80% ndiyo
 
Maalim Seif na Feruzi wapo. Pemba yote wamepiga kura za ndio. Matokeo ya jumla kutolewa punde.
Matokeo yanaendelea kusomwa. Ukiniona kimya jua ni ndio. Nitayataja majimbo ya hapana. Chaani wamesema hapana
 
Matokeo ya majimbo ambayo hayakutangazwa jana yanatangazwa sasa na mwishoni matokeo ya jumla yatatolewa...inaendelea TBC sasa hivi
 
Matokeo ya Pemba yanaendelea kutolewa nI kura za ndio kwa kwenda mbele.
 
Matokeo ya Pemba yanaendelea kutolewa nI kura za ndio kwa kwenda mbele.
Asante sana Pasco, kwa hesabu za haraka haraka i can foretell....
NDIYO 68% (+/-3%)
HAPANA 32% (+/-3%)
 
Pemba wamejitokeza kwa wingi kuliko ZnZ. WakIsususa na Oktober , Seif rais. Ngome Ya CCM ya Kwahani wamesema ndiyo.
 
Pemba wamejitokeza kwa wingi kuliko ZnZ. WakIsususa na Oktober , Seif rais. Ngome Ya CCM ya Kwahani wamesema ndiyo.

Nakubaliana na wewe.

Hii kura ya maoni itainufaisha sana CUF kwenye uchaguzi ujao, maana wanaCCM kindakindaki watakuwa wamevunjwa moyo sana na suala hili na watapungukiwa na mori ya uchaguzi mkuu.
 
Imetangwazwa na tume ya uchaguzi zanzibar dakika chache zilizopita tbc
 
Back
Top Bottom