From Zanzibar: Kura za Maoni Shwari!

From Zanzibar: Kura za Maoni Shwari!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
58,894
Reaction score
132,244
Zoezi la upigaji kura za maoni Zanzibar limeanza asubuhi hii kwa utulivu na amani hali inayotafsiriwa kama kiashiria cha Uchaguzi huru na wa haki mwezi October.

Niko hapa visiwa vya marashi ya Karafuu kuwajulisheni kinachojiri.

Karibuni.
Up Date 1.
Matokeo ya Majimbo matano ya Zanzibar, 4 wamesema ndiyo, moja limesema hapana.
 
Lakini naona kama mapema. hebu tuvute subira kwanza alafu toene.
Mungu ajaalie zoezi liishe kwa amani.
 
Pasco binafsi ningependa zaidi kusikia habari za maeneo ya kaskazini Unguja,,,hasa hasa Donge,, Mkwajuni na Chaani,,hali halisi ikoje huko??
 
Na jee kuna mawakala wa vyama katika vituo vya kura??
 
D u kumbe nimesahau tarehe ya leo, aise haya majukumu yanaweza ua mtu, we Malaria sugu, um ekuwa mwandishi cku hizi na umeacha kazi yako ya ukada?
 
Asante Pasco tupe habari. Malaria sugu acha kumwalibia pasco thread yake, huwa tukishakuona wewe kila kitu kinaonekana kama mzaha hivi
 
uongozi wa kikwete hauna rafu na wala jwtz na police kutika bara hawatapelekwa kuua watu zanzibar. ni hivyo hivyo tunatarajia uchaguzi ujao wa bara na visiwani. Big up JK kwa uvumilivu ambao haujawahi tokea Tz.
 
Sisi wengine tupo mbali hivyo hakuna aliyeko Pemba angalau akatupa ya huko?
 
Zoezi la upigaji kura limemalizika, zoezi la kuhesabu kura pia limemalizika, kinachoendelea sasa ni zoezi la kujumlisha matokeo ya vituo mbalimbali.
Mpaka sasa, kura za ndio zinaongoza, kwa hapa Zanzibar, ndio na hapana zimegawana majimbo, Jimbo la Shamhuma, wamepiga kura za hapana.
Kuanzia saa 2 usiku, nitajisogeza eneo la Bwawani Hotel, ambapo ZEK imefungua kituo cha kupokea matokea, na kama hakuna zengwe, nitawaletea matokeo ya jimbo kwa jimbo.

Nimesema kura za ndio ndio zinaongoza, kama hali hii ni Zanzibar, tunaasume Pemba yote ni ndiyo, hivyo matokeo ya mwisho ni ndio, kinachosubiriwa ni kutangazwa tuu.
 
Asante Pasco tupe habari. Malaria sugu acha kumwalibia pasco thread yake, huwa tukishakuona wewe kila kitu kinaonekana kama mzaha hivi
Shalom, ukishaanzisha thread hapa JF, inakuwa ni ya wote, hakuna thread ya mtu, hivyo mwache MS naye atupe yale ya upande wake.
Malaria Sugu, endeleza.
 
Na jee kuna mawakala wa vyama katika vituo vya kura??

Mshirazi, kura za maoni hazina mawakala wa vyama, ila kuna waangalizi mbalimbali, kuanzia wa kimataifa, kitaifa, mashirika kama TAMCO na waangalizi wa vyama. Chama cha CUF kimeweka waangalizi karibu kila kituo, sikubahatika kuona waangalizi wa CCM.
 
Pasco binafsi ningependa zaidi kusikia habari za maeneo ya kaskazini Unguja,,,hasa hasa Donge,, Mkwajuni na Chaani,,hali halisi ikoje huko??
Mshirazi, hali ni ya utulivu wa hali ya juu, Wilaya ya Kaskazini Unguja huku kwa Shamhuna ndiko nilikobahatika kupita hapa na pale. Hili nin eneo la manazi wa CCM, sikuamini niliposhuhudia kura za hapana nyingi kuliko za ndio.
Nimekubali kweli Wanzanzibari ni kiboko! yaani watu wa misimamo isiyoyumba, siamini baada ya kampeni yote ya Karume kuhamasisha kura ya Ndio, bado kuna majimbo yamepiga kura ya Hapana!.
 
Pasco, utulivu ulio kutana nao hautokani wapiga kura kujitokeza kwa uchache? nafikili kuna jumla ya watu laki nne waliojiandikisha kupiga kura leo. Je hawa wote wametimiza lengo la kipiga kura?
 
Mshirazi, hali ni ya utulivu wa hali ya juu, Wilaya ya Kaskazini Unguja huku kwa Shamhuna ndiko nilikobahatika kupita hapa na pale. Hili nin eneo la manazi wa CCM, sikuamini niliposhuhudia kura za hapana nyingi kuliko za ndio.
Nimekubali kweli Wanzanzibari ni kiboko! yaani watu wa misimamo isiyoyumba, siamini baada ya kampeni yote ya Karume kuhamasisha kura ya Ndio, bado kuna majimbo yamepiga kura ya Hapana!.

Tatizo lililopo hapa si watu kuwa na msimamo bali ni jinsi kampeni zilivyofanyika. Hakukuwa na hamasa ya kura ya ndiyo. Na usishangae kura hii ika-fail. Vile vipeperushi vya kuwataka watu wapige kura ya hapana vilitolewa na nani?. Kwa sababu hata Karume naye moyoni mwake hahitaji kura ya Ndiyo, kila mara amekuwa akisikika kuwa watu kwa wingi "wajitokeze wakapige kura" badala ya kusema " wajitokeze kwa wingi wakapige kura ya Ndiyo"
 
ndiyo na hapana yote ni majibu sahihi ktk demokrasia. Tatizo huwa ni uwingi :shock:
 
Pasco, utulivu ulio kutana nao hautokani wapiga kura kujitokeza kwa uchache? nafikili kuna jumla ya watu laki nne waliojiandikisha kupiga kura leo. Je hawa wote wametimiza lengo la kipiga kura?
Kibunango, ni kweli kuna uwezekano huu utulivu pia umechangiwa na uchache wa waliojitokeza, lakini pia ukumbuke huu ni uchaguzi usio na ushindani, wana CCM hawakujitokeza kwa wingi kutokana na kukatishwa tamaa na muafaka.

Nimejifunza kuwa zile siasa za shari, chuki, jazba, visa na mikasa, ni sehemu za order of the day kwa siasa za Zanzibar. Hivyo maridhiano kwao ni kama kuwakatisha tamaa.

Just imagine unasubiria boxim match ya Tyson na Holifield pale pale MGM, jamaa wanapanda ulingoni, halafu wanaamua kutopigana tena, wanashikana mikono mnatangaziwa pesa zenu mtarudishiwa!, amini usiami kuna watu watakasirika hata kurudishiwa pesa watasusa. ndivyo walivyosusa hao Wa CCM damu hapa ZnZ.
 
CCM wanajificha maana hata mwangalizi hakuna ,lile kundi la akina Shamhuna ni kundi likijidai tu na wakijificha chini ya mwevuli wa CCM lakini hamna kitu walikuwa na malengo yao na si kuendesha nchi ,wamepigwa na chini ,hata huku Bara mnajua kuwa Zanzibar hakuna CCM.
 
Back
Top Bottom