Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 58,912
- 132,334
- Thread starter
- #21
Mwiba, hawa wanaowaliza nyinyi kila siku hapa kwenu Zanzibar ni kina nani kama sio CCM?,CCM wanajificha maana hata mwangalizi hakuna ,lile kundi la akina Shamhuna ni kundi likijidai tu na wakijificha chini ya mwevuli wa CCM lakini hamna kitu walikuwa na malengo yao na si kuendesha nchi ,wamepigwa na chini ,hata huku Bara mnajua kuwa Zanzibar hakuna CCM.
Kama kweli Zanzibar hakuna CCM, waliopo madarakani ambao wataendelea na kuendelea na kuendelea ni kina nani?,
October hiyo inakuja, Maalim kashalabishwa asali, anasubiri kuchonga mzinga, na pia ameingia kwenye ule urembo wa mtego wa makamo wa kwanza, penye urembo ndio penye ulimbo, mkishanasa kwenye uliombo hiyo October, msianze kulioa lia ohh CCM hivi, CCM vile!.