From Madame B to Mung Chris...

From Madame B to Mung Chris...

Hongera kwako

Wewe ni mfano mzuri wa wengi waliopitia mengi ma kuandika humu na mwishowe kumpata mwenza mlieshibana.

Nawatakia kila la kheri.. ila najua wengi watakumisi maana uliwachangamsha sana humu namaanisha wanaume haswaa

Karibu katika hatua unazopitia na mkija kufunga ndoa.. mimi nipo kwenye ndoa miaka mingiii hadi nasahau miaka kwa utamu wake.
 
Hongera sana mamy mungu awatangulie katika penzi lenu.. lol kumbe ni mung Chris ndo yuuuleeee mchaga wa koment yako moja hivi...

hongereni once again..



cc Smart911
Bhana eeee
Mchaga wangu hana tatizo na mtu mwenyewe.

Asante sana kipenzi.
Nashukuru nawe penzi lenu na Smart911 liendelee kuwa hot mpaka mzeeke pamoja.
Thanks
 
Mchaga lazima apagawe na ile kitu..ila madame B mungu anakuona.
Hahaahah
Siku hizi mpaka huko Simiyu ipo.
Sa hv hakuna cha Mombasa wala Tanga....hahahahaha
 
Sijui kitasa kimepata ufunguo, sijui ni ufunguo ndo umepata kitasa.....
Hongera Madame B na shemela
Mie kitasa, yeye ufunguo.
Kitasa kimepata ufunguo.

Asante shost mwaya.
Maana kwa hali ile kumpata wa kunivumilia makasheshe yangu hapa jukwaani isingewezekena.
Ila jamaa ndo kajitosa mzimamzima na maisha yanasonga kabisa.

Asante kipenzi.
Wewe nitakuweka kamati ya michango ya harusi pale January.
 
Hongera kwako

Wewe ni mfano mzuri wa wengi waliopitia mengi ma kuandika humu na mwishowe kumpata mwenza mlieshibana.

Nawatakia kila la kheri.. ila najua wengi watakumisi maana uliwachangamsha sana humu namaanisha wanaume haswaa

Karibu katika hatua unazopitia na mkija kufunga ndoa.. mimi nipo kwenye ndoa miaka mingiii hadi nasahau miaka kwa utamu wake.
Waoo
Asante sana cocochanel.
Kiukweli jamaa ni jasiri, maana aliruka viunzi na changamoto zote zilizosemwa juu yangu na kuamua kusonga mbele.
Hakujali waja wanasema nini.
Wapo waliomvunja moyo,
Wapo waliomkatisha tamaa.
Ila niseme tu ukweli kuwa hawajui kuna maisha nje ya Jamii forums.

Haya maisha ya kujificha nyuma ya keyboard yana ukomo wake.
Si kila mara tutajificha.
Inabidi muda mwingine tuwe-wahalisia ili mambo na vitu vingine visitupite.

Wanaume nitaendelea kuwachangamsha mpaka pale nitakapofika ukomo kwamba siwezi hata type au kushika simu, maana nitakuwa na ulezi wa baba na mtoto.
Asante sana.
Nashukuru
Nitaingia huko soon, japo niliyapitia nyuma, ila kila mwanaume na uleaji wake....🙂🙂🙂
 
alafu design Mung mpole pole!sasa madame sasa!yaan ni pipa na mfuniko kbs!sasa huwa mby mkutane wote wajanja wajanja!hawa wakiamua kuwa serious watadumu!
Hahahhah
Jamaniiii
Mung Chris wangu mpole sana.
Japo anaambiwa hataniweza, ila nina imani ataniweza tu maana mwanamke ana uleaji wake
Sie tutadumu....tutawaletea vijukuu tu mlee maana hapa nahisi kama nina mapacha.
Nitalea mpaka nichanganyikiwe
 
Matokeo chanya ya Jamii forum.
Kabisa mkuu.
Hii mitandano ya kijamii ikitumiwa vyema, huleta matokea chanya kama haya.
Japo wapo wanaopenda yaende (-) ila Mungu ndo ameshapanga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom