From Dar to Goma: How I met, and had lunch with rebels

From Dar to Goma: How I met, and had lunch with rebels

Hakuna lolote hapa, kimsingi mwandishi yupo biased sana. Inaelekea anatumiwa na waasi kwa maslahi binasfi ili aupotoshe ukweli, isitoshe ana uhuru gani wa ku-report against waasi..?
 
Niliisoma kwa kiswahili gazeti jingine, naona hii ipo deep zaidi.
Kwa namna yoyote ile Rwanda na Uganda vinahusika sana.
Museveni alikiri kuwa M23 wana makao mjini Kampala.

Kumbuka Makenga alikuwa na Laurent Nkunda. Baada ya Mkapa, Anan na Obasanjo kumpiga mkwara Nairobi alikwenda na kumkamata Nkunda katika wiki. Wala si kumkamata ni kumwita arudi Kigali ambako hadi leo hana kesi.

Askari wa M23 wanatibiwa Kigali n.k.
Kila jitihada za kutafuta usuluhishi Kagame na Museveni wamekuwa Kikwazo.
 
Hakuna lolote hapa, kimsingi mwandishi yupo biased sana. Inaelekea anatumiwa na waasi kwa maslahi binasfi ili aupotoshe ukweli, isitoshe ana uhuru gani wa ku-report against waasi..?

labda kama hajipendi
 
What are Tanzania interests in Congo that Tanzania will gladly die for Kabila? Dont tell me regional peace........please!
 
Richard Mgamba tena. Mara nyingi huwa anatumiwa kwa maslahi ya kundi fulani. Kwa mara ya kwanza nilimfahamu alipotumiwa na Hubert Sauper kutengeneza documentary ya Darwin's Nightmare.
 
Ninamfahamu Richard na kumuheshimu kama mwandishi mwenye juhudi, nimesoma baadhi ya maandishi yake na huwa napenda msimamo wake sio mtu wa kuburuzwa. Nampongeza kwa juhudu zake za kufika huko alikoenda. Lakini naona article hii ameitoa wakati ikiwa bado haijaiva, yaani ni hadithi ya safari yake ya Goma badala ya habari ya kuboresha kile kinachozungumzwa. Mimi kama mwl, tena wa creative writing, hii habari inakosa majibu mengi tu, kwa mfano, nini hasa alichokua anaki investigate? na nini source yake ya verification maana haiwezi kuwa report za mazungumzo yake na M23 as if ndio the gospel truth. Halafu nafikiri kilichosemwa kingeweza kufanyika kwa nusu ya kurasa zilizotumika, of course hii kazi ilitakiwa iwe edited, sema kwa kuwa shirika lake halina magwiji, nafikiri waandishi mahiri wa lugha hii kama Jenerali Ulimwengu, Atilio Tagalile na Hilal Sued wangepewa kui polish, japo wangemrudisha field, lakini angetoka na kiboko ya kazi, nawashauri pia waandishi hawa wasiogope kuwatumia wasomi wenzao kusomeana kazi, mimi watu hawa wamenisaidia sana kuboresha kazi zangu za kizungu, maana ni wataalamu wa hasa, Kazi tofauti Richard big up
 
Hii kitu imetupwa humo gazetini nzima nzima bila kuhaririwa vipi ?,ina makosa mengi ya kisarufi.
Au Wahariri ndio walewale wa Mtakuja Ward Secondary School.

 
Inakosa mtiririko mzuri wa kingeereza!ilitakiwa kuwa edited!Lakini huu ni Mpango wa Kagame kuipoza SADC kama hausiki na mgogoro wa DRC...Kwa wanaokumbuka kama mwezi mmoja uliopita Kabila aliwasafilisha waandishi karibu kutoka vyombo vya habari vyote vya Tz kwenda DRC,akawalipia kila kitu,na waliporudi kila Gazeti liliisifu Serikali ya Kabila na Kabila mwenyewe!!R WANDA hawakufurahi..nao wamemtumia huyu ku-neutralize ziara ile....all in all,jamaa kafanya kazi nzuri na ya kijasiri..lakn kama HUBERT SAUPER na "Darwin's Night Mare" vilimumpa mamilioni,kwanini na safari ya Goma isiwe na Motive behind?
 
Niliisoma kwa kiswahili gazeti jingine, naona hii ipo deep zaidi.
Kwa namna yoyote ile Rwanda na Uganda vinahusika sana.
Museveni alikiri kuwa M23 wana makao mjini Kampala.

Kumbuka Makenga alikuwa na Laurent Nkunda. Baada ya Mkapa, Anan na Obasanjo kumpiga mkwara Nairobi alikwenda na kumkamata Nkunda katika wiki. Wala si kumkamata ni kumwita arudi Kigali ambako hadi leo hana kesi.

Askari wa M23 wanatibiwa Kigali n.k.
Kila jitihada za kutafuta usuluhishi Kagame na Museveni wamekuwa Kikwazo.

Hilo la Nkunda linatoa picha kubwa juu ya ushiriki wa Rwanda. Kama alikamatwa kwanini hana kesi? I wish to know more of this lake zone conflict. Tanzania ushiriki wetu upoje?
 
hii habari ni nzuri,lakin na wasiwasi watu watashindwa kuisoma ni ndefu na tz ni wavivu kusoma
 
Ila mwandishi hajaweka details za uchunguzi wake. Mostly ameweka flow inayokupa hisia lakini isiyojibu swali la nini hasa kafuata. Pamoja na kuwa ni investive journalism, bado organisation ya safari ingejibu maswali muhimu. Kama ulialikwa kuhudhuria sherehe za chama, na ghafla unapata guts za kuahirisha tukio lililokupeleka unaenda war zone so simply. Inaibua swali muhimu, nani yupo nyuma yake? Anampeleka mpakani na kumsubiri arudi. Nani huyo anayeorganise meeting na head of rebels wakati hata heads of states huwa wanakutana nje ya war zone? Its a good piece of writing anyway
 
Wakati masilahi ya Rwanda na Uganda ndani ya Kongo yanajulikana, Tanzania ipo ipo tu.

Tulizipigania nchi kibao kusini mwa Africa lakini hatukufaidika na fursa zilizokuwepo kwenye hizo nchi. Hata ushindi wa vita vya Kagera ilitakiwa itupe faida badala ya umasikini... Tusisubiri kulipwa na Manaani kwa wema tunaizifanyia hizi nchi.

Vinginevyo kazi ya mwandishi ni yakupongezwa na bila shaka imekidhi mahitaji ya aliyeimtuma be it Kagame, M7 au Dr. Mengi.
 
Nimesoma yote pia. Kitu ambacho naona wengi hamjakistukia ni kuwa huyu katumwa na Rwanda. Na huu ni mkwara kwa SADC kuwa goma sio somalia. Tujiandae kupoteza wanajeshi huko.

Na mwandishi anatukumbusha kuwa kuna bifu linaendelea dhidi ya Tanzania kutoka Uganda na Rwanda.

wewe unaakili mwandishi ni pro M23 tusti na zaidi anapa sifa za uongo Sultan Makenga.
eti mara anasema Makenga ni General mara anasema Ni Brigadier wakati ukweli makenga ni Colonel.
tena anasema makenga wazazi wakake wako ukimbizini wakati ukweli makenga ni Mnyarwanda na Baba yake anaishi Kigali.
 
Mgamba ni mwandishi mwenye guts hapa Tanzania. Ni habati mbaya kuwa ilikuwa ngumu kuongea na wakazi pia kujua feeling zao juu ya kinaachoendelea.

Na kama anatamani story yake ijibu maswali mengi anapaswa arudi huko kimya kimya bila mwaliko rasmi wa waasi ili apate picha ama inayopingana au inayasupport haya ya mwanzo kutoka uraiani ofcourse hii itakuwa safari ya hatari zaidi kuliko hii ya mwanzo.
 
Hili swala la DRC si la leo , USA ,UN na UBELIGIJI(Belgium) ndiyo wahusika wakuu wa dhahama yote.
Wao ndio walioongoza harakati zote kumkamata hdi kumuua Waziri mkuu wa kwanza
Patrice Emery Lumumba.
 
Nguruvi3,

..suala la DRC ni very complex.

..lakini bila hata kujisumbua sana, hivi si majuzi tu wamefanya UCHAGUZI MKUU wa pili tangu Mobutu aondolewe madarakani??

..sasa hawa rebels walikuwa wapi wakati wenzao wanafanya UCHAGUZI?

..pia DRC wana utawala wa majimbo, je hawa rebels wameshindwa kutatua matatizo yao ktk level ya jimbo mpaka waanzishe vita na serikali kuu??
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom