Niende moja kwa moja kwa kile nilichokiwaza, nikajiuliza maswali na kujijibu Mwenyewe.
1. Hivi ni kweli BEN SAANANE alikuwa mkamilifu na mtiifu kwa 100% kwa Viongozi wake na chama chake kwa ujumla
2. Hofu ya CHADEMA juu kupotea kwa Ben Saanane ni kwa sababu BEN alikuwa mkosoaji mkubwa wa Rais Magufuli (kwa mujibu wa Tamko la Chama kupitia Mwanasheria wake mkuu, Tundu Lissu) au ni kwa sababu alikuwa Mfedheheshaji, Mtukanaji na mdhalilishaji mkubwa wa rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
3. Ndiyo chama kimetoa tamko na kikubwa tulichosikia ni kwamba CHADEMA hawajui BEN alipo. Je Ile intelijensia ya CHADEMA ambayo tulihubiriwa ziku zote kuwa ni kubwa kuliko ya jeshi la Polisi yenyewe imefikia wapi na kumtafuta BEN? Idata ya ulinzi ya Wifred Lwakatare iko wapi?
4. Baada ya BEN kupotea, vijana wa BAVICHA hususan walioko mitandaoni wakiongozwa na Godlitsen Malisa, Hilda Newton na Eliza Beth wamekuwa wwkitumia nguvu kubwa sana kutaka kuonesha wameguswa sana suala la BEN huku wakito taarifa zenye utata juu ya BEN, Malisa akasema BEN hakuwa Mkurugenzi wa Sera na Utafiti wa CHADEMA huku Hilda akituambia BEN yuko Afrika kusini na kwamba tutulie tusiwe na wasiwasi. Malisa na HILDA wana agenda gani na kupotea kwa BEN? Wanajua nini kuhusu kupotea kwa BEN? Je ni nafasi ya BEN saanane ndiyo inatafutwa?(Mungu atawaaibisha, atamleta BEN aendelee na wadhifa wake).
FUNZO NILILOPATA:
Tunapoamua kuwa madui wa upande mmoja, basi tuhakikishe tunamoishi hatuna adui hata mmoja, ile methali kwamba Zimwi likujualo halikuli likakwisha imepitwa na wakati lakini misemo wa fimbo ya mbali haiui nyoka na ule wa UMDHANIAYE NDIYE SIYE kamwe haiwezi kupitwa na wakati. BEN ametofautina mara nyingi sana na viongozi wake waliopo na hata waliotoka ndani ya CHAMA. Hakika na maadui wengi sana hasa wa ndani kuliko wa nje kama tunavyofikiria. Kuna wakati ilisemekana BEN alikuwa anaondoka CHADEMA na hata mrundikano wa vyeo ambavyo amekuwa akipewa siku za hivi karibuni ni kumpooza tu. Rais wa awamu ya nne, Jakaya mrisho Kikwete aliwahi kusema maneno ambayo hatuwezi kuyasahau akiwa katika sherehe za mei mosi na wakati mkutano mkuu wa CCM
1. Akili ya kuambiwa changanya na ya kwako
2. Ukitaka kula lazima uliwe kidogo
BEN SAANANE popote alipo anapaswa kutafakari kwa kina ukaribu ambao anawekewa na watu wake wa karibu ambao awali walikuwa maadui.