Pasco, heshima mbele mkuu. Siku ya mapinduzi ya Zanzibar, nilikuwa nina umri wa miaka minne, na sitasahau siku ile ambapo tulila msituni na mamangu pamoja na dadangu katika harakati za kujificha kutokana na watu kuwa wanakimbia huku na kule. Sijawahi sahau hata siku moja. Wakati wa mapinduzi yale, watanganyika hawakuwepo, wala mapinduzi yale hayakufanyika ili baadaye tuje tuunde serikali ya muuungano? Tulifanya yale mapinduzi kwa maslahi ya watu wa zanzibar, na tulikuwa tunaitaka Zanzibar huru na si vinginevyo. Nikiwa kama mhanga wa adha za yale mapinduzi, siwezi kukubali damu ya wazanzibar iliyomwagika kwa ajili ya ukombozi wa wazanzibar ipotee bure.
Wazanzibari hadi hivi sasa bado hatupo huru, kwa kuwa hatuna uwezo wa kufanya mambo yetu wenyewe. Wazanzibar tunaamuliwa mambo yetu na watanganyika ambao wanatudanganyishia nafasi za uwaziri na umakamu wa rais. Sisi hatuna shida na nafasi hizo, tunataka zanzibar huru. Tunataka uhuru tulioupigania wakati wa mapinduzi ya mwaka 1964, utunufaishe wa zanzibar na iwe ni shukurani kwa mashujaa wetu waliopigania uhuru wetu.
Pasco, kwa nafasi yako, yawezekana hicho unachokisema ndo kinadhihirisha msimamo wa serikali ya Tanganyika. Sasa nasema wazanzibar hatujanyamaza katika hili. Tunaendelea na mikakati, wala msijeshangaa siku tutakapo iondoa serikali ya CCM madarakani na kuweka kiongozi mwingine atakayeitangaza Zanzibar kama nchi huru.
Msema hovyo, kwanza samahani kwa kuku under estimate kuwa huujui uhuru wa Zanzibar, pili nilipoona jina lako la Msema hovyo, nikadhania wewe ni msema hovyo kweli, kumbe ni jina tuu.
Pole kwa kuwa ni muhanga wa Mapinduzi yale sasa naomba tubishane kwa hoja based on facts na sio hisia tuu.
1. Kwanza tukubaliane, Zanzibar ilipata uhuru Desemba, 1963, that is a fact, you can't deny. Hivyo Zanzibar inachokitaka sasa sio uhuru, bali restoration ya its soverenity iliyoipoteza kwenye muungano na sio uhuru.
2. Pili, 'Umoja ni Nguvu', hivyo muungano wowote wenye nia ya kuleta umoja, ji jambo jema, ni jambo la kheri, licha ya kuwepo matatizo haya na yale. Hii inamaana, ukiondoa kero za muungano, muungano ni jambo la kheri.
3. Na tatu tukubaliane sababu zilizopelekea muungano wa Tanganyika na Zanzibar wakati ule zilikuwa valid na tena kwa nia njema ya usalama wa Zanzibar hata kama ghara yake ni ustawi hasi. Hebu ifikirie Zanzibar bila Muungano, ingekuwa Zanzibar gani?. Si mgeishia kuchinjana kila kukicha?. Just imagine, japo ulikuwa mdogo wa miaka 4 tuu wakati wa Mapinduzi, mimi nimesoma accont ya mlichowafanya Waarabu kwenye mapinduzi yale, hakuna aliyeandika wala unyama wa mapinduzi hayo haupaswi kuhadithiwa, itakuwa ni kujenga chuki na kutonyesha vidonda kwa waliofiliwa. Bila muungano, manowari ya Uingereza ilishatia nanga Mombasa, tayari kuvamia Zanzibar na kumrudisha Sultan Jamseed. Jee Sultan angerudi, unaweza kuimagine hatima ya wanamapinduzi?. Lazima mumshukuru sana Nyerere na Karume ndio maana wengine wenu mpaka leo mnaweza kukohoa kudai uhuru.
Nakubaliana nanyi kuwa sababu zilizopelekea muungano doesn't exist anymore na pia makubaliano yale ya msingi yameshakiukwa na kupindishwa na kuongezwa bila ridhaa ya upande wa pili kulikopelekea muungano huu kuzongwa na kero lukuki, dawa ya kero hizi ni kuzitatua na kuzirekebisha na sio kuuvunja muungano.
Kwa vile muungano iliingiwa kwa nia njema 'in good faith', naomba hata tunapojadili maslahi ya Zanzibar kwenye muungano huu, tudadili in good faith tukitanguliza utaifa mbele na kuacha hisia nyuma.
Nakuhakikishia wewe Msema hovyo na wengine wa aina yako, hata ikitokea muungano ukavunjika leo, kesho, Zanzibar hamtabaki salama kama mnavyojidhania, wale mliowachinjia baba zao na mama zao kwenye mapinduzi yale, na kuwabakia binti zao huku wengine mkijitwalia kuwafanya wake zunu, damu yao itawashukia na utafika muda, jambia zitatembea tena!.
Tukiuvunja muungano huu uliopo sasa, Wazanzibari ndio watakuwa the biggest loosers maana ni Zanzibar ndio ina gain the most ndani muunganu huu at the expense of sisi wabara!