platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,366
- 11,154
Wewe ni mwanaume na umepitia mengi linapokuja suala la mahusiano ya kimapenzi. Kifupi una mengi umejifunza na kuona: Umeumizwa na kuumiza mpaka roho imeingia uyabisi.
Halafu unakuja katika pilipilika za kawaida unapata g/f mpya........Huyu hajawahi kuingia ulimwengu huu wa mapenzi, hajawi kuumiza wala kuumizwa. Kifupi ameona pengine marafiki wakiumizwa na yeye kuishia kuona kama ni jambo tu la kuachana.
Sasa yupo kwako, anakupenda sana na anaona Dunia bila wewe haiwezekani, hafikirii ipo siku ataumizwa. Haoni wala hasikii linapokuja swala kuhusu wewe. Anakuamini kupita hata mzazi wake, na anafanya mengi kwa ajili yako. Na zaidi anaamini huwezi kumdanganya kabisa, ingawa wewe binafsi uongo ina sehemu kiasi fulani katika maisha ya kimapenzi kutokana na uliyopitia.
Wakati mwingine unamuonea huruma.....unafikiri at least awe anaku-doubt hivi ili siku mambo yakiharibika asiumie zaidi. Lakini yeye ndio anazidi kuonyesha namna wewe ulivyo shujaa wake!!
Ndio maana nakuuliza ulishawahi kuyapitia haya? Uliyaendesha vipi haya mahusiano. Vipi yalipovunjika!..........!!
Halafu unakuja katika pilipilika za kawaida unapata g/f mpya........Huyu hajawahi kuingia ulimwengu huu wa mapenzi, hajawi kuumiza wala kuumizwa. Kifupi ameona pengine marafiki wakiumizwa na yeye kuishia kuona kama ni jambo tu la kuachana.
Sasa yupo kwako, anakupenda sana na anaona Dunia bila wewe haiwezekani, hafikirii ipo siku ataumizwa. Haoni wala hasikii linapokuja swala kuhusu wewe. Anakuamini kupita hata mzazi wake, na anafanya mengi kwa ajili yako. Na zaidi anaamini huwezi kumdanganya kabisa, ingawa wewe binafsi uongo ina sehemu kiasi fulani katika maisha ya kimapenzi kutokana na uliyopitia.
Wakati mwingine unamuonea huruma.....unafikiri at least awe anaku-doubt hivi ili siku mambo yakiharibika asiumie zaidi. Lakini yeye ndio anazidi kuonyesha namna wewe ulivyo shujaa wake!!
Ndio maana nakuuliza ulishawahi kuyapitia haya? Uliyaendesha vipi haya mahusiano. Vipi yalipovunjika!..........!!