Flash Back Memories: Matukio ya Boarding School

kuna mwalimu mmoja wa kike now ni marehem (RIP), ilikuwa ikifika zamu yake anazingua kichizi, saa 11 ameshazama bwenini kwa boys na anatembeza stick hatari, sasa boys wakawa wanamfanyia visa dizain ya kulala uchi af akiwasha taa jamaa anaamka mashine iko mnara, ticha anasema nimeshaona zaidi ya hizo, watu wakaona isiwe tabu, siku moja tukang'oa switch ya taa maana alikuwa akija tu anapapasa pale kwenye switch ili awashe taa, halafu bwezi zima tukatengeneza midoli vitandani ukicheki utadhani watu wamelala then tukaenda kweny mchakamchaka, ye amekuja kama kawaida yake akapapasa, dah alichezea shoti ya umeme, asubuhi asubuhi, haha
 
1.Nakumbuka tulivyogoma kula tukapigwa SP form six wote mwezi mmoja ukirudi unarudi na mzazi na barua ya serikali ya mtaa.
2.Vijana wa shule za Boyz kuwa na nguo za matukio kama kuna debate weruweru au machame utawaelewa.
3.Tulivyowapiga shule fulani inaitwa Lyamungo
 
Daaa umesahau chiluba na mazwi kupiga gongo,kidedi kuvutia ganja miksa chanji kwenda kuchi pilau j pili night
Ha ha ha usisahau kabla ya kwenda kidedi lazima tupoze pale kwa Aswile. Then lazima turipoti kwakina Jack Ko....wa pale tuoshe maana kulikuwa watoto warembo hataree. Then kidedi kupiga ganja afu Chiluba kupiga gongo. Dah idumu kantalamba.
 
Kupewa sh 100 ukanunue vitu vya sh 500 na chenji irudi,kila siku kuamshwa na mwalimu wa zamu ili kwenda assemble
 
Kuibia watu kwenye maloka kwa kutekenyesha funguo..au kwenye matrank ya chuma yale...mengine yalikuwa mepes bas tunayapiga butterfly..heheheee....kufua ilkuwa tatzo bas n kuanuliana mashat tu
Umenikumbusha mkuu, tranka likigoma mnalitikisa ili wali uchanganyike na madaftari na nguo
 
Ahahaha jamaa nahis jamaa baadae fungus walimzoea....Ulikuwa comb IPI mkuu PCB,EGM ama PCM?
 
Nilikua pugu ujamaa 5 PCM miaka 90,umekumbusha mbali sana mambo ya pond, kudrop na mwisho wa lami, bus letu lilikua uda la kwenda kisarawe, tulikua tunapandia msimbazi
Bila kusahau vyoo vya Pugu vilivyokuwa vikiitwa battle kutokana NA kwamba ukienda kujisaidia kubwa lazima uvue sharti kama unaenda pigana.
 
Hao waliokuwa wanafanya hivyo sasa hivi wako wapi? Wengi utakuta wameharibikiwa
 
Nyie ni makomando aisee..au unatupa scenes za komando kipensi?
Dah... tulikuwa tunafanya majaribio ya Molotov cocktail hatukujua hata madhara yake itakavyokuwa ndiyo maana tukajaribu kwenye magari ya jeshi 🙂
 
Nakumbuka nikiwa Weruweru girls tulikuwa tunalima sana, wakati wa kulima lazima nizidiwe, na nikilazimishwa najifanya nimezimia.
 
Ila mimi sitasahau jkt tu, tuliiba ndoo ya futari ya waislamu tukatokomea nayo mtoni wakati tunaenda kumwagilia bustani basi mashehe wakaanza kutafuta huku wamelipoti kwa MP jamaa walinikuta nina ndoo ya wali umebaki kidogo wenzangu walikuwa wanamwagilia nikabaki peke yangu. Siku hiyo nilicheze kichapo push up unainuka na fimbo, kofi unaenda chini na kofi au fimbo huu mchezo ulidumu kuanzia saa tatu usiku mpaka saa sita, alikuja kuniokoa afande wa zamu wa kombania yetu maana tulikoiba ilikuwa combania nyingine, afande aliwaambia akanishughurikie yeye basi akanirukisha kichura kidogo akanisimamisha akanipa big up sana ule wali uliosalia walikula combania nzima yaani ndo ikwa pona yangu ila mgongo ni damu tupu. Tuliiba wengi msala ukanishukia pekee yangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…