Flash Back Memories: Matukio ya Boarding School

Wako wapi members wa Mkwawa high school
The complex Cassino. 1990's -2000's

Wanafunzi kutorokea makanyagio kununua maandazi kwa jina la uficho zilikuwa zinaitwa nyama au banzi.

Batch ya 1999-2001 kuna jamaa alikuwa mkorofi sana ali act kama agent wa hizo nyama anachukua huko makanyagio anazileta shule. .alijulikana kama mzee wa nyama.
 
Kulala abroad( nje ya shule na kurudi asubh.) Unalala kwa mmama au mwanafunz wa kike mtaan.2 kufungiwaa na mwanamke kwa nje na wafumaniaj! Kukosa vtafunwaa vya chai# kupuliza;
 
Kweli boarding raha nakumbuka kuna mwl wa commerce wa kike alikuwa anachapa mboko na hakuna mwanafunzi alimtaka sasa bahati akafikwa na umauti bwn! Sasa kipindi anakata roho hosp hatukuwa na habari.Sasa Staff member (walimu)wakaja kututangazia kile kifo kwa majonzi makubwa eebwanae shule yote frm 1 to iv wote tuliruka juu na kushangilia kwa Furaha ila mboko tulikuwa za ukweli ila hakika hatukufanya vizuri but hasira tu
 
Hii shule itakuwa Arusha nn mkuu
 
Haha huu uzi unachekesha hatarii, ngoja tu share kidogo
1. Nakumbuka tulivo toroka siku ya jumapili kwenda kwny sherehe kijijini mara gafla kumbe mwalimu alikuwa mwalikwa na alituona bila sisi kumuona akarudi shule chap kaitisha Rocoo (ikumbukwe huyu ticha ana pikipiki) na kuna umbali wa kutosha kutoka kwenye sherehe mpaka shule. Kama kawaida tukamaliza tukio na msosi mwingine tukaweka kwenye mifuko meusi tukaweka kweny mabegi kila na mtu na mzigo wake wa kutosha apo wa kula siku2 au 3,
kimbembe kikufika shule tuuu tulitumia chimbo letu kuingia Kama kawaida cha ajabu kila mtu anakushangaa tukajua kimenuka wee baada ya dk kadhaa kengelee ikagongwa sitakaa nisahau kilicho endelea baada ya hapo
2. Kuibiwa chupi zote na kubaki na moja tuu nashkuru mungu ilikuwa imebaki week kadhaa kufunga shule
3. Nguo zangu kuchanganywa na maharage
A level hakukua na mengi kama O level ila moja la kushangaza nlilolikuta humu ni kutongozwa na demu mwenzako na alafu couple nliona za kutosha uku (hii ilikuwa single sex)
Duu mungu ni mwema nlitoboa lakini boarding duuu lazima ukomae na ujitie ukichaa ku survive
 
Dah umenikumbusha pugu secondary wazee wa pondi mixer beto dah nimepamiss sana
 
Watoto wa kishua hasa wa dar wakija na viatu vya kulingishia(raba au timbaland)watu wanaiba mguu mmoja kila pair.
 
Daaaaa Mimi nilikuwa WANTED......

Yaan kama ingekuwa nchi kama marekani ningekuwa the most notorious Killer in the country

Kiss cha kuwa wanted nikikisimulia wrote mtalia machozi...., ngoja niishie hapa
 
Lyamungo ama umbwe nini?
 
Nakumbuka jamaa mmoja shabiki wa damu wa ASENALI, dah alikua jamaa angu sana, siku hiyo timu yake ilifungwa 8 na man u, alilia machozi kabisa akimlaumu wenger, dah nikimkumbushaga mpaka leo anacheka tu mwenyewe
 
Hahahhaha,umekumbusha tulivyokuwa tunafoji stemp,jamani tunafuta mhuri halafu tunatumia hiyo stemp kutuma barua,pia shida ya maji ndo ilisababisha watu tupige passport size,yaani nilishaapa kamwe wanangu hawawezi kusoma boarding schools
Hahahaha stemp inafutwa muhuri mpk inaonekana mpya na bahasha za kuchonga kwa kutumia karatasi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…