Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
Wananchi wa kitongoji cha Maramba kata ya Luilo walisema kuwa wanampongeza mbunge Filikunjombe kwa msaada wake wa nyavu ya kutegea nyani( Lipilipili) ambayo imewawezesha kutega nyani zaidi ya 80 hadi sasa toka zilipotolewa miezi miwili iliyopita.
Maeneo mengine ambayo mbunge Filikunjombe alitoa msaada wa Lipilili kwa ajili ya kutega nyani hao ni pamoja na Liughai na Lifuma kata ya Luilo ambako pia wamefanikiwa kutega nyani zaidi ya 50.
Huku wananchi wa kata ya Rupingu katika kijiji cha Nindi na kata ya Lifuma kijiji cha Mtalawamba walisema kuwa msaada huo wa mbunge wa mitego ya nyani umeongeza kasi ya wananchi kuanza kulima zaidi mazao ya chakula kutokana na awali kuogopa kulima kutokana na nyani hao kutishia usalama wa zao.