Filamu za bongo-part1 na part2

phina

JF-Expert Member
Jul 18, 2011
414
126
Nina uhakika mengi yamesemwa kuhusu hili, lakini mbona sioni mabadiliko jamani??yani unakuta movie inaenda taratiiiiiiibu...kitu kinachukua saa moja na nusu-content is poor!alafu naambiwa watchout for part 2!!!wats there to wait for??
Watengenezaji/anayehusika wafanye kitu sasa-mabadiliko.tunatamani kuokoa sanaa lakini hambebeki!ebo!!!
Na mshukuru mabasi ya mikoani yanayoonyesha hizo muvi..
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Kuwe na mabadiliko kwani umeambiwa hua wanasikiliza maoni ya watu?

Lazima waendelee kuwaonyesha scene ya mtu anaendesha gari kwa dakika kumi ili mlipie kitu kimoja mara mbili.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
hivi kwa nini mnaziangalia? Nyie ni sawa na wakazi wa mabondeni wanaolalamikia serikali baada ya mafuriko
 
Nilipata kuongea na wasamazaji fulani wakasema waTz wanapenda vitu cheap na kudanganywa. Kwa mfano wao wangetengeneza filamu yenye DVD moja wangependa kuuza sh 5000/= lakini wanadhani waTZ wataona wametoa pesa "nyingi" halafu wamepewa "ka-DVD" kamoja tu. Hivyo ni bora wawauzie part 1 & 2 kwa jumla ya 6000/=.

This is very bad. Hata hivyo inatoa picha juu ya uelewa wa jumla wa waTz. Bado tuko nyuma sana katika mambo mengi na si filamu pekee (sitetei uzembe). Angalia mashabiki wa soka wa Tanzania wanavyodanganywa na magazeti. Magazeti huandika titles kama:

  1. Papic ataja bunduki za kuua Zamalek
  2. Kili Stars kuichinja Brazil
  3. Yanga kama Man U!
Uongo mtupu!!!!

Lakini mambo yanabadilika pia japo pole pole.
 
...........................
Na mshukuru mabasi ya mikoani yanayoonyesha hizo muvi..

Wiki iliyopita nilisafiri kwenda mkoa mmoja hivi, then kwenye basi (kama unavyosema) walionesha filamu ya Kanumba na Ramsey Noah ya Devil Kingdom..... aisee, mimi ni mtetezi wa akina Kanumba na Ray lakini kwa vigezo vyangu Kanumba kacheza chini sana ya kiwango. Kaongea kiingereza ambacho ni kama vile hakikuwa scripted. Kiingereza cha Ramsey kimenyooka (achilia mbali matamshi ya ki-Nigeria nisiyoyapenda) na ni kama vile katunga mwenyewe. Sasa, sina tatizo na uwezo wa wastani/mdogo wa Kanumba kuongea fluently kutoka kichwani.. kwanini asiandike kiingereza kizuri (hata kama ni kwa kusaidiwa au kurekebishwa) then akariri? Kanumba anaweza kukariri na akatamka vizuri (angalau). Huu ni uzembe. Matokeo yake akawa bubu mbele ya Ramsey (asinidanganye kuwa ilipangwa). Kama ilipangwa awe bubu that much basi mtunzi wa stori na director ni wazembe/wabovu balaa. Director ni yeye mwenyewe Kanumba. Kwa "uzito" wa Ramsey ("kutoka Nigeria bana!!!"), yeye Kanumba, akina Myamba na Title ya filamu, then the movie was supposed to be much much better than that.
 
kilengesa cha kunumba ni nooomaaaaaaa yani cha ajabu sana kama cha mtoto wa darasa la tatu anayejifunza kingeleza
 
Film industry ilianza vizuri saana Bongo.... But bahati mbaya saana thou walikuja kwa kasi bado yaonekana wanasimama badala ya kusonga mbele... Hakuna ambacho wanaboreshe kusema sasa ziwe na quality nzuri na standard pia.... Wapo so based on kujiboresha the way they look na the way they will appear katika movie and where they will appear....
 
tatizo waliiangia kwenye industry ya movie kwa kucopy staili za wanigeria sasa wanakosa ubunifu wakwao, kwa kifupi wanaigiza takataka tupu hata ukisema ununue kazi zao kuwasupport utaishia kupoteza hela zako halafu hamna chochote wanachokibuni, kwa mfano kanumba ni director, script writter, main character, location manager, editor yaani ni upuuzi mtupu
 
Mimi hata sizilaumu hizi ndume zinazothubutu angalau kutengeneza hivo vi-movie maigizo! Lawama zangu natupa kwa wanataaluma wa sanaa za maigizo waliochimbia taaluma zao na sasa wanafanya biashara ya kuuza kuku wa mayai na kufuga ng'ombe wa maziwa!
Ndugu zanguni huwezi ukatarajia kitu chema out of laymen! U want a professional display, there must be professionals.
Hawa std 7 watatengeneza movie gani? and ur sitting there throwing your blames, Ooh! Kanumba Bwana! kanumba bwana! Akina.

Nikiaangalia bongo movies ni goofs mwanzo mwisho! Labda kwa kuwasaidia lianzishwe jukwaa hata hapa JF tuzichambue hizi movies kila zinzpotoka may be itasaidia kuboresha siku zijazo!\

Halafu Luccy Kiwhere nae Bwana hizo choice za movies dstv Swahili! Aibu tupu, Mi-subtitles imekaa hovyo hovyo!
Kuna moja ilichekesha mpaka leo nikiikumbuka huwaga nacheka mwenyewe! Mtu na pacha wake wamegombania mme! Halafu huyu anagudua script ilikuwa imekaa hivi

Linda, nataka nikuuwe! (Kashikilia kisu mkononi)
pacha anauliza; Unataka kuniuwa!
Unataka kuniuwa!
Linda; Eeee!L
Pacha kaitikia: Haya niuwe!
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Mimi hata sizilaumu hizi ndume zinazothubutu angalau kutengeneza hivo vi-movie maigizo! Lawama zangu natupa kwa wanataaluma wa sanaa za maigizo waliochimbia taaluma zao na sasa wanafanya biashara ya kuuza kuku wa mayai na kufuga ng'ombe wa maziwa!
Ndugu zanguni huwezi ukatarajia kitu chema out of laymen! U want a professional display, there must be professionals.
Hawa std 7 watatengeneza movie gani? and ur sitting there throwing your blames, Ooh! Kanumba Bwana! kanumba bwana! Akina.

Nikiaangalia bongo movies ni goofs mwanzo mwisho! Labda kwa kuwasaidia lianzishwe jukwaa hata hapa JF tuzichambue hizi movies kila zinzpotoka may be itasaidia kuboresha siku zijazo!\

Halafu Luccy Kiwhere nae Bwana hizo choice za movies dstv Swahili! Aibu tupu, Mi-subtitles imekaa hovyo hovyo!
Kuna moja ilichekesha mpaka leo nikiikumbuka huwaga nacheka mwenyewe! Mtu na pacha wake wamegombania mme! Halafu huyu anagudua script ilikuwa imekaa hivi

Linda, nataka nikuuwe! (Kashikilia kisu mkononi)
pacha anauliza; Unataka kuniuwa!
Unataka kuniuwa!
Linda; Eeee!L
Pacha kaitikia: Haya niuwe!

Pacha: umeniuuuwa but why umeniuwa?
 
Phina, naomba uelewe kuwa sinema za Part 1 na 2 ni sumu mbaya iliyopandikizwa tu
kwa makusudi fulani. Soko la filamu lilikuwa likikua vizuri na kuleta ufanisi, lakini kitendo
kilichofanywa na msambazaji wa filamu nchini, Steps Entertainment, kuwalazimisha
watayarishaji wa filamu kutengeneza sinema yenye sehemu mbili au zaidi hata kama
hadithi hairuhusu, ndiyo sababu ya kuididimiza tasnia hii kwa maana ya kupungua ubora
wa kazi husika.

Kitendo hiki pia humlazimisha msanii kuigiza awamu ya pili ya filamu (kwa pesa ileile) hata
kama hakuwa na lengo la kuigiza sehemu hiyo, jambo hili linatafsiriwa kama kuendelea
kuwanyonya wasanii kupitia kazi zao kwa malipo kiduchu wanayowalipa.

Nina mfano hai ulimtokea mtayarishaji wa filamu nchini, Hamisi Kibari, anayejulikana
sana kwa filamu zake za 'Usiku wa Taabu' na 'Mtoto wa RPC' ambaye kwa sasa
ametoka na filamu ya 'Naomi', aliitengeneza filamu hiyo ikiwa katika sehemu moja tu,
baada ya kuridhishwa na script iliyopitiwa na wataalam kadhaa na kuonekana kuwa ni nzuri.

Baada ya kukamilisha kazi hiyo aliipeleka Steps, ambaye aliipitia na timu yake, waliisifia sana
lakini wakamshauri kuwa kama anataka waisambaze lazima aangalie uwezekano wa kuirefusha
kwa kutovikata vipande (scenes) mapema, bali aviache viendelee kwa zaidi ya dakika tano,
aongezee establishing shots nyingi na kuweka flashback ndefu ili angalau filamu iwe ndefu
kwa ajili ya kuikata sehemu mbili, jambo ambalo Kibari hakukubaliana nalo kwa kuhofia
kuharibu mtiririko wa stori.

Baadaye Kibari aliamua kufanya utafiti kuhusu faida na hasara ya filamu hizi za part 1 na 2
kwa kumfuata msambazaji mwingine, ambaye alimweleza kuwa watazamaji wengi na hata
wauzaji wa filamu wa rejareja wamekuwa wakizikacha filamu zisizokuwa na sehemu mbili na
husubiri hadi sehemu ya pili itakapotoka ndipo wanunue, jambo ambalo limekuwa likisababisha
hasara kwa watayarishaji wa filamu zisizokuwa na sehemu mbili.

Kulazimisha sinema iwe na namba moja na mbili kunasababisha kuoneshwa kipande (scene)
kimoja cha mtu kwa zaidi ya dakika tano akifanya tukio moja, mfano mtu anatoka kuoga
anaingia chumbani, kisha anaaza kupaka mafuta, anavaa nguo, anachana nywele na kupaka
vipodozi! Yote yakiwa yanafanywa kwa zaidi ya dakika tano! Jambo hili limekuwa linavuruga
lengo la sinema ambalo ni kuwaburudisha na kuwaelimisha watazamaji kama ilivyo dhana nzima
ya filamu na ugizaji, na badala yake limekuwa likiwakera.

Utoaji wa filamu ya part 1 na 2 ni sumu mbaya sana iliyopandikizwa kwa watazamaji wa filamu
ambao wamekuwa wakiamini kununua sinema yoyote isiyokuwa na part 1 na 2 ni kuibiwa, na
imekuwa kama jeraha kubwa lililogeuka kuwa gonjwa sugu mfano wa saratani. Hivi sasa
tunashuhudia filamu zisizo na ubora zikijitokeza kila uchao kwa sababu ya kulazimisha utengenezaji
wa sehemu mbili kinyume na taaluma ya filamu.

Watayarishaji wengi wa filamu wanaopeleka kazi zao Steps, hata kama zina ubora hujikuta
wakikataliwa kwa sababu tu hazina sehemu mbili, kitu ambacho ni unyanyasaji, hujuma kwa
soko la filamu na hakizingatii taaluma (professionalism).

Kwa sasa imekuwa ni jambo la kawaida kwa filamu moja kuigawa na kuwa na sehemu zaidi
ya moja na kubatizwa jina la part 1 na kuendelea hata kama zitafika mia ni jukumu la
mtayarishaji wa filamu husika, na ukiuliza utaambiwa kuwa wasambazaji wanapambana na
maharamia wa kazi za wasanii, wakigawa wanasababisha wezi hawa kupungua, jambo ambalo
sidhani kama lina ukweli wowote.

Kilichofanywa hapa ni kiini macho tu na wizi, kupunguza bei ya DVD hadi 1,500/- na kuigawa
filamu mara mbili au zaidi, ambapo mtazamaji anayehitaji kuiangalia filamu yote humlazimu
kununua DVD nyingi (sehemu ya filamu zote) ambazo zimegawanywa, na hujikuta akizinunua
kwa bei kubwa zaidi tofauti na inavyosemwa kuwa bei imeshushwa. Kama lengo ni kupambana
na uharamia wa filamu basi kwa mtindo huu watakuwa wamechemsha, kwa kuwa filamu bandia
bado ni gharama nafuu.

Kimsingi ugawaji wa filamu katika sehemu zaidi ya moja unamnufaisha zaidi msambazaji na wala
si mtumiaji ambaye amejengewa dhana ya kwamba sinema isiyokuwa na sehemu mbili haifai na
anaibiwa pesa zake. Filamu ya Part 1 na 2 ni sawa na filamu moja yenye dakika 70 hadi 90, na
ukiangalia kitaalamu zaidi utagundua kuwa ndani ya filamu hiyo kuna filamu fupi sana isiyozidi
dakika 20, kwa kuwa vipande vingi ni establishing shots, flashbacks ndefu, na matukio marefu
yasiyo na maana kabisa.

Utengenezaji wa filamu ya part 1 na 2 ni njia ya kuwaibia watazamaji kijanja bila kutoa jasho.
Mbona filamu za Kihindi ni ndefu sana lakini hazina part 1 na 2? Ila kutokana na msisimko wa
visa na msuko mzuri wa stori zao utajikuta umemaliza filamu bila kuulizia part 2.

Kitaalam kuna neno linaloitwa ‘serialization', yaani muendelezo wa visa kuhusiana na
mhusika fulani au hadithi husika. Mfano mzuri ni filamu za God Father, Da Vinci Code,
Harry Porter na kadhalika. Pia kuna sinema kama The Princess Diary, ambayo ina sehemu
mbili lakini zilizopangiliwa vizuri kiasi kwamba huhitaji kupata sehemu zote ili kuijua stori,
kila sehemu inatosha kukuburudisha bila msada wa sehemu ya pili japo ya pili ni kama
muendelezo wa sehemu ya kwanza.

Kibari ameamua kutoa filamu ya Naomi ambayo licha ya kuwa na sehemu mbili lakini
kila sehemu ina stori inayojitegemea, yenye maudhui na visa tofauti ili kumpa burudani
mtazamaji, jambo ambalo limezingatia taaluma husika.

Wananchi na wanunuzi wa sinema za Bongo wanapaswa kufahamu kuwa kununua filamu
za part 1 na 2 ambazo kimsingi zilipaswa kuwa sehemu moja tu ya filamu ni kuibiwa.
 
Film industry ilianza vizuri saana Bongo.... But bahati mbaya saana thou walikuja kwa kasi bado yaonekana wanasimama badala ya kusonga mbele... Hakuna ambacho wanaboreshe kusema sasa ziwe na quality nzuri na standard pia.... Wapo so based on kujiboresha the way they look na the way they will appear katika movie and where they will appear....


Unakumbuka Masaa 24 "Mpasuko wa Moyo" ya John Kalage
na wakina Cheni, lol kweli tulianza vizuri....
ila nilipata nafasi ya kuona TBC filamu moja ya wakina Prof Amandina Lihamba na wazee wengine ni ya zamani sana, ni filamu tamu sana.

Pia kuna filamu iliwahi kuonyeshwa na kwenye TV ya hawa jamaa wa Bagamoyo, walishiriki wakina Irene sanga, Vitalis Maembe (kipindi hicho ndio anatoka) na wasanii wengine wa pale bagamoyo.

Kitu cha ajabu hapa kwetu TZ, vitu vinavyofanywa na kwa utaalamu na ubora wa viwango vinavyoeleweka huwa havipewi promo na media zetu hivyo hata wananchi wanakuwa hawavijui sana.

Kuna wabongo wengi sana wanauwezo mkubwa sana kwenye mambo haya ila soko limewakataa....

Kumbuka wakati ule ZIFF, filamu zilizokuwa zinashiriki zilikuwa ni za dizaini hizo hapo ambazo wabongo wameigiza na wabongo wengi hawazijui ila zilikuwa zinafanya vizuri nje ya mipaka hasa ulaya.....
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Phina, naomba uelewe kuwa sinema za Part 1 na 2 ni sumu mbaya iliyopandikizwa tu
kwa makusudi fulani. Soko la filamu ......................................................

Bishop nakubaliana na yote uliyosema. Sasa kuna jitahada zozote ninyi kama wadau wa filamu (umepata kuwa katibu wa Tanzania Film Federatiion (TAFF)) kupambana na hali hii? Wengine tunaowaza kuingia katika medani ya Filamu tunatishwa sana na mazingaombwe haya.
 
Bishop nakubaliana na yote uliyosema. Sasa kuna jitahada zozote ninyi kama wadau wa filamu (umepata kuwa katibu wa Tanzania Film Federatiion (TAFF)) kupambana na hali hii? Wengine tunaowaza kuingia katika medani ya Filamu tunatishwa sana na mazingaombwe haya.

Dah, unajua kuna matatizo mengi sana katika tasnia hii, kwanza watayalishaji wa filamu nchini
wamekosa mafunzo ya msingi (nitty-gritty) ya namna ya kutengeneza kazi zao katika kiwango
kinachokubalika, wengi ni wabinafsi na wanaowekeza kidogo na kutarajia wavune mara dufu
kwa mara moja. Ubinafsi huo umesababisha filamu zetu kuwa ni kitu kisichozingatia au kuhitaji
taaluma yoyote. Watu wanalipua kazi na wanafanya mambo bila kuzingatia utaalam. Wanafanya
mambo ili mradi wanajua watauza na kupata pesa, basi. Ubinafsi huu umekuwa ni sababu kuu ya
kuufanya uwanja wa filamu wa Tanzania kuwa sehemu inayoongoza kwa kutokuwa na mgawanyo
wa majukumu. Si ajabu kuona mkurugenzi wa kampuni ya kutengeneza filamu, ndiye aliyeandika
skripti, ndiye muongozaji mkuu, ndiye muigizaji mkuu na kadhalika.

Lakini hata hivyo kipindi chote nimekuwa nikipigania tasnia hii iwe rasmi, nimeshawahi kumuandikia
Waziri Nchimbi mara kadhaa na nimewahi kuwasilisha ripoti yangu ya utafiti kwa Rais Kikwete ili waone
umuhimu wa tasnia hii na kuirasimisha. Unajua sekta ya filamu hapa nchini licha ya ubovu wa filamu zake
ambazo huwa naziangalia kwa ku-Fast Forward, lakini imesheheni utajiri mkubwa sana, tatizo ni kwamba
hadi sasa bado si rasmi kiasi cha kuwafanya wadau wake waendelee kuwa masikini wa kutupwa pamoja
na kuingiza mamilioni ya pesa ambayo hata hivyo yanawafaidisha wafanyabiashara wachache huku
serikali ikiwa haiambulii chochote.

Huu mpango wa Serikali wa Kurasimisha Biashara na Rasilimali za wanyonge nchini (Mkurabita)
hauonekani kuwasaidia wajasiriamali katika tasnia hii ili waweze kufanya kazi kwenye mazingira
yaliyo rasmi kwa kuwa hali ilivyo sasa inawafanya wakose fursa nyingi za kukuza kazi zao ikiwa ni
pamoja na kutoa kazi bora. Pia inawakatisha tamaa wanaotaka kuwekeza katika tasnia hii kama
wewe kwa kuwa hawana uhakika na soko. Mimi mwenyewe ingawa nipo kwenye tasnia hii kwa
miaka mingi na nimebahatika kuisomea lakini sijawahi kutoa filamu kwa kuwa kuna mambo mengi
yanayokwaza. Na hata ukitengeneza filamu nzuri hali hii inazifanya filamu zionekane hazina thamani kutokana
na tasnia kutokuwa rasmi. Kwa sasa kidogo serikali imeanza kuitambua tasnia hii, labda tusubiri kuona
watu makini wakijitosa katika ulingo, kwani katika kukabiliana na wimbi la watendaji wasio na uwezo wala
taaluma, Serikali kupitia Bodi ya Ukaguzi wa Filamu na Michezo ya Kuigiza ilizindua kanuni mpya za Sheria
ya Filamu na Michezo ya Kuigiza mjini Musoma mkoani Mara, zilizozinduliwa na Makamu wa Rais,
Dk. Mohamed Gharib Bilal. Kanuni hizo zimeainisha adhabu mbalimbali ikiwemo kulipa faini ya papo kwa
hapo isiyopungua Shilingi milioni mbili kwa watengenezaji, waoneshaji na wasambazaji wa filamu watakaozikiuka.

Kuzinduliwa kwa kanuni kuliambatana na kauli ya Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Dk Emmanuel Nchimbi, kuwataka wote kufuata sheria na kusajiri kazi zao kabla hatua za kisheria
hazijachukuliwa dhidi yao. Waziri Nchimbi alisema Serikali imechoshwa na uwepo wa filamu zisizo na maadili.

Kanuni hizi zinaelekeza kuwa anayetaka kutengeneza filamu lazima aombe kwanza kibali. Miongoni mwa
mambo yanayohitaji kibali ni pamoja na kutumia vifaa na mavazi rasmi yanayotumiwa na majeshi ya
ulinzi na usalama, madaktari, viongozi wa dini, manesi na sare za wanafunzi. Kibali hakitatolewa kwa
picha ambazo uchezaji, miondoko ya mwili wa mshiriki au msanii unalenga ama lengo pekee ni kushawishi,
kuwashawishi watazamaji kupata, kujenga taswira na hisia za ngono au kujamiiana.

Naamini kama serikali watazingatia haya, tutashuhudia watu makini wakiwekeza kwenye tasnia na
kuzika zama za utitiri wa hizi Bongo movie zisizo na kichwa wala miguu zinazokopi tamaduni za nje...
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Back
Top Bottom