Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 121,947
- 95,237
Huo ni mpango maalum uliopangwa kishamba ili kuwapumbaza watanzania na kuwaaminisha kuwa bunge hili ni sawa na lililopita lenye wapinzani.Mbunge wa viti maalumu, Felister Njau amepewa siku saba kuthibitisha kauli yake aliyoitoa bungeni kuhusu kukamatwa kwa mabegi matano ya kura wakati wa uchaguzi mkuu 2020.
Felister ametakiwa kupeleka uthibitisho huo na naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson leo Jumatano Februari 3, 2021 kutokana na kauli yake hiyo aliyoitoa bungeni wakati akichangia hotuba ya Rais John Magufuli ya ufunguzi wa Bunge la 12.
My Take
CCM wamepita kwa wizi wa kura, Covid19 wamepita kwa wizi wa vifungu vya katiba. Ngoma droo
Hiyo ni kete ya Ndugayi kuwahadaa watanzania kuwa bunge lipo active kumbe ni sawa na kikao cha wana ccm tu