Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,894
- 155,916
Zikiota kichwani Nywele
Chini ya paji la uso Nyusi
Juu ya jicho Kope
Kati ya pua na mdomo Sharubu
Kidevuni ndevu
tuendelee......
hizi nazo ni fedha?
Hapana kiongozi me nitatofautiana na wewe hapo umetafafasiri matumizi ya neno pesa linabadilika kutokana na mazingira ila haujatueleza pesa linamajina gani tofauti na neno lenyewe pesa mfano mzuri ni wa Nyani Ngabu hapo juu ametoa majina ya mtaani ni sahihi kbs na mimi nitakupa yangu km vile mavumba, njuruku na mengine mengi sana.
mh, mkono wa kidhungu manoti ya kialbaino,,,,PESA INA MAJINA MENGI KULINGANA NA MAHALI NA MATUMIZI
1.Kwenye ibada inaitwa Zaka/sadaka
2.Msibani inaitwa rambirambi
3.Shule inaitwa Ada au Karo
4.Kwenye vyombo vya usafiri inaitwa nauli
5.Ukiinunulia haki inaitwa rushwa
6.Kumdhamini mtu mahakamani inaitwa dhamana
7.Kwenye uchaguzi inaitwa takrima
8.Ukiwapa kina Preta snowhite inaitwa hongo
Mengine tukumbushane....
ukilipa wazazi wa mrembo ili uchukue wanaita MAHARI.
Hapo kwenye NJURUKU piga ua wewe ni chinga