Fedha za kugharamia bima ya afya kwa wote zikusanywe kupitia tozo mpya kupitia malipo ya bili za maji

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,207
4,702
Ndugu Watanzania kwa mazingira ya sasa Bima ya Afya ni hitaji la msingi kwa kila Mtanzania.

Hata hivyo changamoto iliyopo ni hali ngumu ya Kiuchumi kwa Watanzania walio wengi.

Naishauri Serikali iwasilishe muswada Bungeni wa Bima ya Afya kwa wote kupitia Tozo zitakazokusanywa kupitia malipo ya bili za maji nchi nzima.

Tozo zimethibitika kuwa na manufaa makubwa kwenye Ujenzi wa madarasa, vituo vya afya na barabara.

Napendekeza kiwango maalumu kikatwe mara moja kwa kila malipo yatakayofanyika kulipia huduma za maji na kisha kiasi kitakachokusanywa kiwasilishwe kwa mamlaka husika.

Kupitia mfumo huu Mteja atalipia huduma hii bila kuona au kuhisi mzigo wowote na wakati huo akiwezesha kupatikana huduma muhimu ya Bima ya Afya.

Ndugu zangu Watanzania hakuna linaloshindikana.

Bima ya afya kwa Watanzania wote inawezekana.

Kazi Iendelee.
 
Kwani hamna vyanzo vigine vya mapato zaidi ya kutesa wana nchi mlisema wenyewe hi nchi tajiri, sasa utajiri uko wapi? Mbona makato na tozo zimezidi
 
Mimi nilidhani ungeshauri serikali ya awamu ya sita iuze baadhi ya ndege kutoka atcl kwa kuwa ilithibitisha kuwa shirika linajiendesha kwa hasara kwa miaka 5 ili pesa ielekezwe huko.
 
So na sisi tunaokatwa mishahara yetu unatuambiaje..au unataka tukatwe mara mbili?
 
C4ED67D4-F41C-4BC8-B1A5-BFAA1195C3DF.jpeg
 
Yaani wafanyakazi wa sekta binafsi na serikali wanakatwa sehemu ya mishahara yao ili wakalipe bima za kwao na familia zao halafu tena muwakamate kwenye tozo kupitia maji wakawalipie na watu wengine?
 
Back
Top Bottom