Hawa jamaa wamejisahau sana ni cancer mbaya sana katika hii nchi.
Alafu hivi siku hizi JF imekuaje?Yaani hii thread pamoja na mambo ya msingi yaliyoandikwa ina zaidi ya dakika 40 haina wachangiaji.Cha ajabu zikija thread za majungu ndio watu wanazipenda.JF is no longer forum for great thinkers!
Mtanisamehe,tumekuwa watu wa ajabu sana siku hizi.
kibo 10 ,hii ndio JF ya leo.
Anyway,labda hii mada sio mpya hapa Jukwaani.
Kumbuka mambo ni tofauti kabisa siku hizi. Nchi (Tanzania Bara na Zanzibar) imejaa vijana waliozaliwa miaka ya 1980. Unajua karibu asilimia 60 ya wapiga kura 2015 walikuwa na umri siyo zaidi ya miaka 35. Vijana wengi hawana elimu ya kutosha, uchambuzi wao uko chini. wanajua kuimba demokrasia lakini ukimuuliza kuwa demokrasia ni nini hawwezi kutoa jibu la maana. Wako vijana, na hawa ni wengi, wanaodhani kuwa demokrasia ni kutukana, kumsema kiongozi, kutotii mamlaka na kadhalika. hawajui kuwa demokrasia inaendana na nidhamu, hilo hawafahamu. Halafu wengi sio wachambuzi, hawasomi vitabu na maandiko mbalimbali. Wao ni mabingwa wa kuangalia TV na wanadhani huo ndio uchambuzi. Hawana muda wa kusoma theories, paradigms, political systems, democratization procdesses; self emancipation; geo politics. Wao wanadhani demokrasia ni ile inayohubiriwa na marekani na wasitambue kuwa huko marekani demokrasia yenyewe iko matatizoni kutokana na matajiri kushikilia maamuzi. Hawajui ukomunisti ni nini, na wala hawajui kuwa matatizo ya afrika yanasababishwa na neo-colonialism na kwamba mataifa wakoloni walitoa uhuru wa bendera na sio uhuru wa kiuchumi.
Vijana wengi wanafahamu kuwa demokrasia ni vyama vingi vya siasa na siyo zaidi ya hapo na kwamba demokrasia ya kweli ni pale upinzani unaposhinda kwenye uchaguzi na siyo vingine.
Vijana wengi hawawezi kujenga hoja iwe ni humu JF au kwingineko na kwamba matusi yakiwemo ya nguoni ni sehemu ya maisha yao. Hawawezi kuchangia mijadala ya maana ndani ya JF au kwingineko lakini wanaweza kuchangia tu ikiwa mijadala hiyo ni ya kuwasema watu na hasa viongozi na kadhalika. Hawawezi kuchangia mada za maana kwa kuwa hawana uwezo wa kuchangia hoja na kadhalika....