Fastjet: Basi linalopaa angani

Fastjet: Basi linalopaa angani

fastjet kwa mwanza wamewamaliza kabisa PW maana wasukuma wanakwea pipa utafikiri mashindano, sasa fastjet anzisheni MWANZA to NAIROBI na DAR-NAIROBI
 
Kaka acha kutetea ujinga,mm nauza vocha ila hata ukitaka voda rusha ya 200 ukanipa elfu10 chenji ntawapa hata kama muwe kumi napata wapi chenji? Naenda mapema bank naomba chenji hakuna kutegemea huruma za mangi sasa hilo shirika kubwa hivo wanashindwa?

sasa hiyo itakuwa biashara ya change au usafiri?
 
Natumaini wengi wetu tumepata bahati ya kupaa na Fastjet katika maeneo tofauti hawa jamaa kwa kweli wahudumu & huduma ndani ya ndege ni za kusikitisha yaani utafikiri umepanda basi la abiria.

Iweje huduma ambazo wanalipisha ukimpa hela kubwa (ya chenji) harudishi na huyo mhudumu hutamuona tena moaka unashuka kwenye ndege sijui hata wanaendaga kujifungia wapi.

Nimesafiri sana na hawa jamaa hasa KIA-DAR, DAR- MBEYA na DAR - MWANZA kila ukiwapa hela ya chenji hsabu maumivu, ukijidai kuuliza swali kwa kiingereza ndo umemkimbikiza mazima anazuga HOLD ON ndo anajidai bizeeee anakupita kama hakujui mpaka ndege inatua. ukienda ofisin kwao Daah Hatareee.

Ndugu zanguni Fastjet badilikeni

Sasa wewe unahudumiwa utoi tipu? Ebo?
 
mkuu uliloga hapo ulipoamua kuongea kiingereza. wengi wa wahudumu wa mule ni form 4 failure na ajira za mule zimekaa kujuana Juana ktk kubana matumizi si unajua tena BUDGET AIRLINE
 
nilistuka kuona Bus linalopaa angani kumbe ni ubahili wa huyu bange kama huwezi fastjet panda British airways
 
Nawakubali sana Fastjet aisee, mimi nina tiketi zangu kadhaa za DAR-KIA na DAR-MWANZA mpaka mwezi wa 5, na wakati mwingine huwa naenda ELDORET (Kenya) so nakwea DAR to KIA then naunga basi mpaka NAIROBI then basi to ELDORET Full KUSAVE.
 
Je kwenye lile bac letu la air tanzania hali ilikwaje miaka ile?
 
Naona fastjet si nafuu tena kama wanavyodai

Mkuu uko sahihi kabisa.

Kwa Dar Moshi kuna wakati Precision wanakuwa rahisi zaidi.

Hata nauli zikiwa sawa, precision wako nafuu kwa kuwa unaweza kubeba mzigo wa 23kg.
 
Natumaini wengi wetu tumepata bahati ya kupaa na Fastjet katika maeneo tofauti hawa jamaa kwa kweli wahudumu & huduma ndani ya ndege ni za kusikitisha yaani utafikiri umepanda basi la abiria.

Iweje huduma ambazo wanalipisha ukimpa hela kubwa (ya chenji) harudishi na huyo mhudumu hutamuona tena moaka unashuka kwenye ndege sijui hata wanaendaga kujifungia wapi.

Nimesafiri sana na hawa jamaa hasa KIA-DAR, DAR- MBEYA na DAR - MWANZA kila ukiwapa hela ya chenji hsabu maumivu, ukijidai kuuliza swali kwa kiingereza ndo umemkimbikiza mazima anazuga HOLD ON ndo anajidai bizeeee anakupita kama hakujui mpaka ndege inatua. ukienda ofisin kwao Daah Hatareee.

Ndugu zanguni Fastjet badilikeni

Sa na wewe unadhani chenji wanatoa wapi?kuna duka la mangi mle, toa pesa tumia hadi iishe
 
Fastjet hawana makosa....jina linajitosheleza airline ya safari fupi na budget airline, next time nenda na change yako, kibongobongo wanajitahidi, Ulaya wana budget airline kama EasyJet na Rynair wanatengeneza siti za kusimama kama basi za mbagala
Eti siti za kusimama!!!!!!!
 
mkuu uliloga hapo ulipoamua kuongea kiingereza. wengi wa wahudumu wa mule ni form 4 failure na ajira za mule zimekaa kujuana Juana ktk kubana matumizi si unajua tena BUDGET AIRLINE

ujuzi wa lugha ni lazima uingie darasani?
 
Watanzania tujifunze lugha kwa bidii tunakosa vingi kwa kung'ang'ania KISWAHILI chetu ona sasa hata wanyarwanda wanatuzidi kwa lugha sasa wanaongea kifaransa, kiingereza, kiswahili na kinyarwanda ukienda interview mkiwa na sifa zinazofanana anakupiga bao kwenye lugha
 
Back
Top Bottom