SSH2025_2030
JF-Expert Member
- Jul 9, 2012
- 9,661
- 9,753
jamaa wamejirekebisha aisee na sasa wameongeza ndege so punctuality, reliability ni ya hali ya juu sana ukilinganisha na ATC na Precision.
Watanzania muwe na shukrani wakati mwingine. Sisemi kuchikichia na chenji za wananchi ni jambo jema lakini wakati mwingine mnawatega bure. Unanunua bites za buku mbili jero then unaangusha hapo msimbazi safari ya dk50. Na mko angani.hamna kibanda cha mangi huko juu eti tuseme ataenda kuomba chenji mara moja. I think it is a professional of telling you guys that they are really sorry n that they cant provide a change so tembea zako huko lakini siku nyingine uje na chenji kamili.
Lets be considerate kidogo basi heeeeeeee!!
dah at least umesema,, ata kwa economies of life kwanini uache kunywa maji ya chupa ndogo kwa 500/- ukiwa nje ya airport mpaka ukanywe maji ya chupa ndogo kwa 3000/- ati kwa vile umesafiri kwa ndege alafu watoa 10000/- wataka upewe chenchi hewani,, nadhani na ulimbukeni wachangia pia hapa na kutokuwa logical
Kweli tupu. Crew wengi wa fast jet kiingereza mgogoro.hata yale maelezo ya jinsi ya kufunga mkanda na kujiokoa anasoma kwenye karatasi lakini Bado anachapia.ishu ya chenji ni Kweli pia.
cha ajabu wanaolalamika kingereza kibovu ni waswahili wanaojua kiswahili fasahaUmeenda kusafiri au kusikiliza english????
sasa jamaniiiii kule hewani kama chenji hawana wataendaje "duka la jirani" kuomba chenji!?????ingieni na chenji kamili muone kama watawanyang'anya na nyingine mlizoficha mfukoni!
kingine usitarajie makubwa ktk safari ya dk 50 kama ile ya masaa 6+!
Kuna siku moja natoka MWZ kuja DAR, pale Airport ya Mwanza nje kuna kale ka-bar kapo opposite, kuna babu mmoja akawa anapiga ugali wa muhogo na sangara, kumbe nae alikuwa ni msafiri, tulipokuwa angani akainuka kwenda toilet ile ya kule mbele karibu na mlango wa cockpit, nadhani aliharisha sana yule babu masikini maana baada ya kutoka choo kile kilifungwa na abiria wengine wote tukawa tunaelekezwa kutumia kile choo cha nyuma.