Ndio maana wanaume wa kiafrika tunawahi kufa na hatuendelei. Mke badala ya kua msaidizi anakua mnyonyaji, kupe, yeye ni kuhakikisha unakamlika hadi ufe.Ukiwa kama baba wa nyumba unatakiwa ujue mahitaji ya familia pesa yetu ni ya kuongezea pale inapohitajika lakini isitegemewe
Ni kweli unavyosema, mwanaume ukikubali kuwa dunia imebadilika na unaishi na co-partner basi na wewe ukumbuke kupuga deku chooni na kufua mashuka J' most. Huwezi kuwa na keki yako na kuila kwa wakati mmojaMleta mada umeteleza. Hakuna mwanaume anayejitambua anayeweza kukwepa majukumu yake kama ana uwezo huo. Dunia imebadilika sana, kwa sasa Wanawake wengi tu wana Kazi nzuri na wanalipwa vizuri sawa na wanaume au hata zaidi. Sasa kama wewe na mumeo mna vipato vizuri na amekuomba mchango wako ili kusukuma familia na nyingine ziende kwenye maendeleo shida iko wapi? Hii tabia ya kichoyo ya kutaka mwanaume akufanyie kila kitu wakati majukumu ya nyumbani anayafanya house girl sio nzuri hata kidogo. Kumbe maisha ni ya wawili, kama yeye ndo maisha anayoyataka kwanini usiende nae na umsupport?
Sent using Jamii Forums mobile app
me love u you know
Daby mwanaume anaebeba majukumu ya familia ana mamlaka kamili ya familia yake. Kama ma waume unajisikiaje ufike nyumbani fridge imejaa na unakaa kabisa kwenye sofa unaomba uletewe bia unywe. Kesho mke akichelewa kurudi una ubavu wa kumuuliza ulikuwa wapi?Nakubaliana na mwanaume kusimamia show. Ila naomba niulize swali Sky.
Hivi uanaume ni nini? Ni kuhudumia familia/mwanamke?
Je, mwanamke akihudumia familia 100% naye ni mwanaume? Je, mwanaume asipomhudumia mwanamke uanaume unakwisha?
Ni kweli kabisa na mwanaume anaebeba majukumu tunakuwaga wepesi sana kugundua kuwa mambo yake si mazuri. Kuna vitu kama cornflakes za watoto, socks, kalamu ambavyo mwanamke anaona huruma hata kumwambia baba yaoNdio maana zamani kijana akitaka kuoa anaulizwa uwezo wa kuhudumia familia. Kuwa na shamba, makazi na uwezo wa kujishughulisha..
Mambo yakienda vibaya kwenye nyumba, anaelaumiwa ni mwanaume. Sikatai kuna kipindi mambo yanagoma kwa kitamvo lakini isiwe utaratibu wa kumfanya mke abebe jukumu lisilo la kwake, na ukitekeleza wajibu wako, bila hiyana unakuta anasaidia baadhi ya mambo hata bila shurti, nnachopinga ni ile mke kuingizwa kwa ulazima abebe kuhudumia familia.
Barikiwa sana rafiki
Kwa hali hiyo atakunyanyasa tukama kuna nia ya kujenga familia imara haina hata haja ya kuhimizana. zitatoka hata zaidi ya 50%. Napenda mwanamke muwajibikaji katika familia. Mwanamke akiwajibika hata mimi nitawajibika asilimia zote.
Nakubaliana na hili...Daby mwanaume anaebeba majukumu ya familia ana mamlaka kamili ya familia yake. Kama ma waume unajisikiaje ufike nyumbani fridge imejaa na unakaa kabisa kwenye sofa unaomba uletewe bia unywe. Kesho mke akichelewa kurudi una ubavu wa kumuuliza ulikuwa wapi?
Mawazo yako ni mazuri sana ila wengi wenu mnaharibiwa na ndugu zenu kuwaeleza wanaume hawatabiriki anaweza kuoa mwingine. Inatakiwa nawe ujenge kwa siri etc. Aidha mwanamke akihisi unachepuka atakomoa tu hata akiwa na mamillion hatoi hata ndululu.Ni kweli kabisa na mwanaume anaebeba majukumu tunakuwaga wepesi sana kugundua kuwa mambo yake si mazuri. Kuna vitu kama cornflakes za watoto, socks, kalamu ambavyo mwanamke anaona huruma hata kumwambia baba yao
Enzi za babu, bibi, baba na mama zetu ningekubaliana nawe kwa hili, ila kwa maisha ya sasa, HAPANA 110%, sababu wafua boxers n.k. isiwe kisingizio cha mke asitoe mchango wake ndani ya nyumba, mbona ni kujipanga tu, kwanza kiasi gani?! Wataka hela zenu zote ziishie Boutique na Saloon? Kwa sasa mwadai usawa, mwataka kila kitu kitu kiwe pasu kwa pasu, sasa huoni usawa uanzie nyumbani kwetu kwanza? Mamie ili mambo yaende kila mtu kwenye boma letu lazima a chip in, kuanzia sisi, watoto wetu kama wakubwa n.k.Ni pale mwanaume anapokhimiza utoe 50% ya budget yenu ya ndani, hapo si umeshajiweka kuwa unaishi na co-partner? Baada ya hapo unaamka asubuhi unategemea utandikiwe kitanda na boxers zako kule bafuni zifuliwe. Kama mke mambo yake yake yakienda vibaya si unamuweka kwenye hatari ya kupata kidume cha kumpa ile 50% ambayo unaitegemea? Kama unataka kuweka heshima ya ndoa ndani jitume kama mwanaume kwanza pesa yetu ni ya chumvi na mchuzi mix.
Kwahiyo unakubali kuwa dunia hii ya leo tunaishi na co-partners?Enzi za babu, bibi, baba na mama zetu ningekubaliana nawe kwa hili, ila kwa maisha ya sasa, HAPANA 110%, sababu wafua boxers n.k. isiwe kisingizio cha mke asitoe mchango wake ndani ya nyumba, mbona ni kujipanga tu, kwanza kiasi gani?! Wataka hela zenu zote ziishie Boutique na Saloon? Kwa sasa mwadai usawa, mwataka kila kitu kitu kiwe pasu kwa pasu, sasa huoni usawa uanzie nyumbani kwetu kwanza? Mamie ili mambo yaende kila mtu kwenye boma letu lazima a chip in, kuanzia sisi, watoto wetu kama wakubwa n.k.
Note : Wanaume wengi wanapenda vitu natural, punguzeni vikolombwezo feki kama nywele, eyelashes, makeup, nails n.k. mbona hela itatosha tu ndani ya nyumba..
Kabisa..Ofcourse heshima ya mume na mke kitamaduni iko pale pale, hata kwenye vitabu vya dini kama muumini wanashauri na kusisitiza..Kwahiyo unakubali kuwa dunia hii ya leo tunaishi na co-partners?
I concurMwanamme akikubali 50/50 kwenye kuhudumia (matumizi)...hana budi kukubali 50/50 kwenye majukumu mengine.
Mfano, kupika, kufua, kuangalia watoto, usafi wa nyumba nk.
Isiwe tu kwenye budget. ...