Familia inaangamia kwa UKIMWI...

Familia inaangamia kwa UKIMWI...

Annina

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2009
Posts
437
Reaction score
59
Kuna familia tupo nayo karibu inaangamia kwa ukimwi. Alianza baba na mama, akafuatia kaka, dada na leo dada mwingine - wamebaki 2 tu sasa kwenye familia ya watu 7! Kuna watu wanasema ukimwi ukiingia kwenye familia unaweza kuondoka na watu kadhaa... kitaalam haikubaliki lakini kuna kesi nyingi za namna hii sijui kwanini


Annina
 
kisayansi inakataa augment kwamba ukimwi ukiingia kwenye familia wote mnapukutika...but my take is familia ya hivyo imeshamiri kwa uzinifu ndo maana
 
50/50 kwa sababu kuna magonjwa ya laana kwa waliokiuka maagizo ya Mungu, sasa kama mzazi kawarandisha watoto kwa fani ya kutumika hovyo unategemea nini? thy will be die by the same way too, thas why watu wengine wanadai ukimwi ukiingi katika familia unweza ukawamaliza woote,
 
kisayansi inakataa augment kwamba ukimwi ukiingia kwenye familia wote mnapukutika...but my take is familia ya hivyo imeshamiri kwa uzinifu ndo maana

Kuna uwezekano kama wa babu Seya na wanawe. kwamba ama baba alikuwa anagonga pale pale wanake wanagonga au dada walikuwa wanaliwa na mtu mmoja bila kujijua. Hizo zipi sana mitaani. Kwa upande wa baba na wanawe wa kiume, wanaweza kuwa walikuwa wanakula mercury (Hg; au maarufu kama House girl) bila kujijua. Kuna kesi za namna hiyo. Au wakina dada wakilambwa na mtu mmoja either kwa kujijua au kutojijua. Zipo sana mitaani hizi. Vinginevyo, kuna suala la kuchangia viwembe au machine za ndevu. In an extreme case; ni uzinzi uliopitiliza katika familia. Ni rare case, lakini zipo.
 
Kuna familia tupo nayo karibu inaangamia kwa ukimwi. Alianza baba na mama, akafuatia kaka, dada na leo dada mwingine - wamebaki 2 tu sasa kwenye familia ya watu 7! Kuna watu wanasema ukimwi ukiingia kwenye familia unaweza kuondoka na watu kadhaa... kitaalam haikubaliki lakini kuna kesi nyingi za namna hii sijui kwanini


Annina
is just the insident jmani and nothing more.. mwishowe na ushirikina utausishwa...
 
.........Hii familia inaangamia kwa ukimwi kwa sababu ya tabia zao mbaya, ujue Annina tabia unaweza kumrithisha mtoto wako.......kama mzazi ni malaya utakuta hadi watoto pia malaya.
Watoto mara nyingi wanaiga tabia za wazazi, hivyo si ajabu kwa hiyo familia kuteketea kwa ukimwi.
 
Usistaajabu ya Musa...

Kisa hiki kilitokea chuoni hapa Dar. Wanafunzi wa kiume waliamua kujitafutia visichana au wamama wa kuwakaangia mahanjumati, na waajiriwa walijitahidi hata kama ni kutumia masalo basi chuzi liwe zito n.k. wanafunzi walijipanga kwa makundi ya watu 4-6 hivi, walichanga pesa za chakula na kumlipa mpishi wao.

Hakuna aliyejua nini zaidi kinaendelea zaidi ya kupikiwa misosi.
Dactari wa dispensary ya chuo alishituka kesi za ugonjwa wa zinaa zilikuwa zikiongezeka kila kukicha. Dr. akaanza kufanya research ya chinichini, kugundua nini kinaendelea. Kwa siri alimuuliza kila mgonjwa aliyehudhuria tiba, kwamba anafikiri ni nani aliyempa ugonjwa. Wanafunzi wao bila kujua nani anaumwa nini kwa wakati gani, ikagundulika kila aliyeulizwa amtaje mwanamke anayefikiri amempa ugonjwa wa zinaa, karibu wanafunzi 10 walimtaja dada aliyekuwa anawapikia hapo chuoni.

Kumbe dada alikuwa anapika na kuhudumia bila uchoyo.

Akina kaka lazima tujiangalie, jilinde mwenyewe. Ukihisi umepata kaugonjwa jaribu kumchukua mshiriki wako mkatibiwe wote, kama ugonjwa una tiba.

Pole kwa familia hii iliyokufa kwa ukimwi, lakini sijui nani alaumiwe, hatujui kama walijamiiana wanafamilia au kila mmoja alihangaika kwa wakati wake.

Ukimwi ni gonjwa la wote tusipoangalia litatumaliza. Jifunze kusema "hapana" au uwe na mpenzi mmoja ambaye hajaambukizwa na usimwambukize.
 
Hawa watu ni wastaarab angalau kwa kadri ya ufahamu wangu - hasa watoto, inasikitisha sana wanavyokwisha wakijiona, kwa vyovyote baada ya misiba 2 ya mwanzo watoto watakuwa walijitahidi kuwa makini zaidi (busara ya kawaida) lakini bado wameambukizwa na vilio vinaendelea


Annina
 
.........Hii familia inaangamia kwa ukimwi kwa sababu ya tabia zao mbaya, ujue Annina tabia unaweza kumrithisha mtoto wako.......kama mzazi ni malaya utakuta hadi watoto pia malaya.
Watoto mara nyingi wanaiga tabia za wazazi, hivyo si ajabu kwa hiyo familia kuteketea kwa ukimwi.


Si lazima familia iwe malaya. Inaweza kuwa pia ni bahati mbaya. Pamoja na kwamba kila siku kuna wimbo wa kutumia condomu, nikikuuliza swali wewe Pretty; ni mara zote kweli umeweza kutumia au watu wako unakutana nao wanatumia mpira? Unaweza kuwa naye naye mmoja, lakini na yeye ana mmoja kweli na huko nje anatumia kondomu kweli?!! Ni bahati tu kwamba unajikuta huna UKIMWI either aliyekuingilia hana, au posibility ya maambuzi haikuwepo kwa muda ule wa kitendo kutokana na sababu za kibiologia. Chances hizi ni nyingi sana sana mitaani.

Kwa maana hiyo, inawezekana familia ina mkosi/bahati mbaya tu. Kwamba kila aliyekuwa akijaribu kulamba nje anakutana na virus,,, and so and so...! Zipo hizi pia. Kwa maaana hiyo, kwa jinsi UKIMWI ilivyo sasa kwenye jamii yetu, usithubutu kumsema mwenzako vibaya aliyeambukizwa au anayekufa kwa ukimwi. Next unaweza kuwa wewe bila kutarajia.
 
Kuna familia tupo nayo karibu inaangamia kwa ukimwi. Alianza baba na mama, akafuatia kaka, dada na leo dada mwingine - wamebaki 2 tu sasa kwenye familia ya watu 7! Kuna watu wanasema ukimwi ukiingia kwenye familia unaweza kuondoka na watu kadhaa... kitaalam haikubaliki lakini kuna kesi nyingi za namna hii sijui kwanini
Annina

Hii ni rahisi sana, sio kuwa wanalia virusi kwenye ugali, hapana.

Zinaa ndio chanzo kikubwa! Unakuta mfano baba ni kipanga, hivyo analeta ngoma home, mama anaichukua. Huku, pia viwanja vya karibia mabinti hawakatizi mbele ya mzee, matokeo yake sampling frame za vijana nazo zinakuwa zishakuwa katika usawa wa mzee! Matokeo yake, chain inaunganika, linakuwa duara! Hapo habari ndio inaishia
 
Kuna familia tupo nayo karibu inaangamia kwa ukimwi. Alianza baba na mama, akafuatia kaka, dada na leo dada mwingine - wamebaki 2 tu sasa kwenye familia ya watu 7! Kuna watu wanasema ukimwi ukiingia kwenye familia unaweza kuondoka na watu kadhaa... kitaalam haikubaliki lakini kuna kesi nyingi za namna hii sijui kwanini


Annina

mpenzi annina upo???????????/ kimya kabisaaaaaaaaaaaa mpendwa!!!!!!!!!!! au shughuli zimekuzidi??? haya pole, mpenzi.

mi naona hayo ni matukio tu, naweza kusema ni random incidents. sasa ni kwa sababu yanaibua hisia nzito hasa yanapohusu familia moja ndio maana kuna hisia nyingine zinaibuliwa.

nijuavyo mie, dhambi haiambukizwi hata tabia vilevile. japo ukimwi kama ugonjwa unaambukizwa hata kwa watoto wadogo/wachanga kupitia wazazi wao.

zaidi ya yote ni rehema za Mungi tu ndio maanana sisi tunaendelea kuwa hai na afya kama tulivyo. yaipatayo hiyo familia pia ni mapenzi ya Mungu. kama ingekuwa wanavuna walichopanda kwa tabia zao mbaya, hebu fikiria wangapi wana tabia mbaya zaidi na bado wana afya nzuri na furaha?

angalia dunia ilivyochafuka, ina maana hao ndio waovu zaidi? la hasha ni mapenzi ya Mungu tu, na ndio mamana mimi na wewe na wengine wote bado tunaishi hata leo hii. si kwamba tumempa Mungu rushwa au kwamaba tu wema sana au tuna akili sana au wazuri sana, la hasha ni mapenzi ya Mungu.

rejea wmbo wa "Mungu anakupenda" wa Kijitonyama Upendo Group (upo kwenye hii website ya JF)

usiache kuiombea hiyo famlia mpenzi
 
Si lazima familia iwe malaya. Inaweza kuwa pia ni bahati mbaya. Pamoja na kwamba kila siku kuna wimbo wa kutumia condomu, nikikuuliza swali wewe Pretty; ni mara zote kweli umeweza kutumia au watu wako unakutana nao wanatumia mpira? Unaweza kuwa naye naye mmoja, lakini na yeye ana mmoja kweli na huko nje anatumia kondomu kweli?!! Ni bahati tu kwamba unajikuta huna UKIMWI either aliyekuingilia hana, au posibility ya maambuzi haikuwepo kwa muda ule wa kitendo kutokana na sababu za kibiologia. Chances hizi ni nyingi sana sana mitaani.

Kwa maana hiyo, inawezekana familia ina mkosi/bahati mbaya tu. Kwamba kila aliyekuwa akijaribu kulamba nje anakutana na virus,,, and so and so...! Zipo hizi pia. Kwa maaana hiyo, kwa jinsi UKIMWI ilivyo sasa kwenye jamii yetu, usithubutu kumsema mwenzako vibaya aliyeambukizwa au anayekufa kwa ukimwi. Next unaweza kuwa wewe bila kutarajia.


nimekubali mwanjelwa, haya mambo siyo rahisi kama wengi wanavyoyachukulia. ni kweli njia kubwa ya kupata ukimwi ni zinaa, lakini sidhani kama ni sahihi kuihukumu hiyo familia kwa kuiita familia malaya na isiyo tii maagizo ya Mungu. Huenda ni kazi ya Mungu inakamilika hapo, ndo maana mtoa thread amesema hawa watu ni wastaarabu tu, hapo ni kuwaombea tu. yawezekana kuteketea kimwili kwa hii familia ni kuokoka kiroho ka upande mwingine. zaidi ni kwamba yanayotokea kwenye hiyo familia yanaweza yakawa ni chanzo cha mabadiliko miongoni mwetu, na pia hata maoni yetu yaweza kutufanya tutende dhambi juu ya hao watu- haswa pale tunapopata ujasili wa kuwahukumu kwa kuwaita wazinzi. labda niwaulize watu hapa. kama nduguyo anaumwa na anahitaju huduma yako, utatafuta gloves za kuzuia kugusana moja kwa moja , hata kabla hujajua anaumwa nini??? , ikiwa wengi waliambukizwa katika kumhudumia aliyeanza kuumwa mwanzo, wangewezaje kujizuia kuugua na kufa baada ya huyo wa kwanza kuwaambukiza???. au ni wanapi hapa tukijisikia vibaya tu tunaanza a kupima ukimwi????. siyo mpaka yote yanaposhindikana ndo tunapima ukimwi??? sasa nuda wote huo kabla ya kujua , ni kweli wauguzaji wanakuwa wamechukua tahadhari za kutosha kuzuia mugusano hatarishi na mgonjwa ?????.

haya mambo yanazungumzika yakiwa kwa wenzio, yakiwa kwako, huwezi kuona , nikama kutafuta kujibeba mwenyewe ukiwa umekaa
 
Asante sana Akili Kichwani, mi nipo majukumu tu ndo maana napatikana kwa nadra... leo umeamkia upande gani maana umeshuka pointi tupu! ubarikiwe sana


Annina
 
Asante sana Akili Kichwani, mi nipo majukumu tu ndo maana napatikana kwa nadra... leo umeamkia upande gani maana umeshuka pointi tupu! ubarikiwe sana


Annina

nimefarijika sana kukuona tena hapa jamvini, nitafurahi ukikumbuka kutembelea na kule.....

annina kumbuka lakini nilikutahadharisha........ umesahau? tafadhari nielewe!
 
nimefarijika sana kukuona tena hapa jamvini, nitafurahi ukikumbuka kutembelea na kule.....

annina kumbuka lakini nilikutahadharisha........ umesahau? tafadhari nielewe!


dhuhu tabu...


Annina
 
.........Hii familia inaangamia kwa ukimwi kwa sababu ya tabia zao mbaya, ujue Annina tabia unaweza kumrithisha mtoto wako.......kama mzazi ni malaya utakuta hadi watoto pia malaya.
Watoto mara nyingi wanaiga tabia za wazazi, hivyo si ajabu kwa hiyo familia kuteketea kwa ukimwi.


jamani kuna familia nyingie unakuta kuna mgonjwa wa ukimwi katika kumuuguza member wengine wa familia wanajikuta wameshaambukizwa indirect, hii mifano ipo katika jamii yetu
 
nimekubali mwanjelwa, haya mambo siyo rahisi kama wengi wanavyoyachukulia. ni kweli njia kubwa ya kupata ukimwi ni zinaa, lakini sidhani kama ni sahihi kuihukumu hiyo familia kwa kuiita familia malaya na isiyo tii maagizo ya Mungu. Huenda ni kazi ya Mungu inakamilika hapo, ndo maana mtoa thread amesema hawa watu ni wastaarabu tu, hapo ni kuwaombea tu. yawezekana kuteketea kimwili kwa hii familia ni kuokoka kiroho ka upande mwingine. zaidi ni kwamba yanayotokea kwenye hiyo familia yanaweza yakawa ni chanzo cha mabadiliko miongoni mwetu, na pia hata maoni yetu yaweza kutufanya tutende dhambi juu ya hao watu- haswa pale tunapopata ujasili wa kuwahukumu kwa kuwaita wazinzi. labda niwaulize watu hapa. kama nduguyo anaumwa na anahitaju huduma yako, utatafuta gloves za kuzuia kugusana moja kwa moja , hata kabla hujajua anaumwa nini??? , ikiwa wengi waliambukizwa katika kumhudumia aliyeanza kuumwa mwanzo, wangewezaje kujizuia kuugua na kufa baada ya huyo wa kwanza kuwaambukiza???. au ni wanapi hapa tukijisikia vibaya tu tunaanza a kupima ukimwi????. siyo mpaka yote yanaposhindikana ndo tunapima ukimwi??? sasa nuda wote huo kabla ya kujua , ni kweli wauguzaji wanakuwa wamechukua tahadhari za kutosha kuzuia mugusano hatarishi na mgonjwa ?????.

haya mambo yanazungumzika yakiwa kwa wenzio, yakiwa kwako, huwezi kuona , nikama kutafuta kujibeba mwenyewe ukiwa umekaa

Kindimbajuu umesema sawa - tuzidi kuomba maana hali mbaya.


Annina
 
pia inategemea na elimu waliyo nayo kuhusu ukimwi, si lazima wote wawe wazinzi,kama ni familia moja lazima watakuwa wanauguzana je wanapata elimu ya kutosha kuhusu ugonjwa huo,kuna bibi kizee mmoja alikuwa anafanya biashara ya kuuza chips, alikuwa na mtoto wake mgonjwa wa ukimwi akawa anamkamua majipu, nae alikuja kufa na ukimwi watu walimshangaa sana bibi kizee huyo ila baadae ilikuja kugundulika wakati anamenya vile viazi alikuwa anapata minor cuts na ndio hizo zilizompelekea umauti,kwa hiyo nadhani itahitajika msaada wa elimu ya ukimwi mkubwa sana kwa familia hiyo
 
Back
Top Bottom