Falsafa ya R 4 za Rais Samia inakupa Mtanzania uhuru wako wa kweli

FaizaFoxy

Platinum Member
Apr 13, 2011
92,894
109,227
Toka nilipoanza kuzisoma na kuzifanyia tafiti zangu binafsi R 4 za mama Samia nimeona na nnaendelea kuona kuwa R 4 za mama Samia zimelenga kumpa uhuru wa kweli kila mmoja wetu kivyake na siyo uhuru wa kukusanywa kikundi na kujazwa ujinga na "viongozi".

Tatizo kubwa na la kipekee la Watanzania ni ujinga, hili nimelirudia mara kwa mara na naendelea kulirudia. Naamini kwenda shule pekee na kujaza vyeti ukuta mzima siyo kuelimika, kuelimika ni zaidi ya hapo. Hutoelimika mpaka uwe na uwezo wa kusikiliza na kufata hekima njemaza qwengine daima.

Kuondoa ujinga ni pale wewe kama wewe utapoanza kufikiri, kuwaza na kutenda kwa faida ya jamii na kuwacha mazowea ya ujinga wa u "mimi", "u yangu" na "u vyangu". Anza u sisi, u vyetu. Fikiria wenzako kabla hujajifiria nafasi yako. uwa huru ni kuwa na fikra za faida kwa wengine, siyo kwako. Bila kuwa na faida kwa wengine huna faida yoyote.

Ujinga mwengine ni ujinga wa kuwa tegemezi kwa wengine tuliojazwa nao kuanzia mkoloni mpaka leo hii. Ukienda kuomba msaada kwa rafiki, kaka, dada, mjomba, shangazi (kwa mtazamo wako ana uwezo) wa kukusaidia akishindwa kukusaidia basi kishakuwa mbaya, huo ni ujinga wa utegemezi. Anza kuufuta kwa kufanya "reconciliation".

R 4 za mama Samia zina vina virefu na vipana sana na vina vyake vinatugusa sote, kila mmoja wetu kivyake kwa faida ya walio wengi.

R ya kwanza "Reconciliation" ya mama Samia ina kina (very deep) kuliko tunavoisoma kijuu juu kuwa ni kusameheana tu. Unapomsamehe mwenzako hufikirii maumivu yaliyokupata wewe bali unafikiria kuyaponya maumivu na kuondoa makovu yako kwa kumsamehe yeye kwa faida yako, yake na ya jamii kwa ujumla. Kusamehe {forgiveness) ni dhana moja tu katika "reconcialtion".

Nikiiongelea hii dhana moja tu ya "Reconciliation" ntaujaza huu uzi bila kuzigusia dhana nyingine.

Kwa ufupi "reconciliation" imelenga kukuweka huru kwanza katika fikra zako na vitendo vyako, inakupa amani ya moyo na nafsi yako na ya wale ambao ume "reconciliate" nao. Reconciliation ya kwanza kabisa ni kukubali ndani ya moyo wako kuwa upo huru na jamii yako inayokuzunguka na hauna minyororo (minyonyoro, ki mama Samia) inayokufunga nafsi na mawazo yako. Reconiciliation ni ufunguo wa kuifunguwa minyororo inayokuzonga zonga kifikra na kukuweka huru kabisa.

Leo naishia hapo, nikitoka hapo ntaingia kwenye R ya pili.

Anza kuwa huru kwa kufanya reconciliation" na nafsi yako kwanza, halafu tazama unaendelea kufanya "reconciliation" na nani kila siku ya maisha yako?

Unapochangia uzi huu kuwa huru bila kujizonga zonga na minyororo uliyojifunga au uliyofungwa kwa kufanywa u mjinga wa kuburuzwa. Fanya "reconciliation" ya kweli. Ongea na nafsi yako.

Itaebdelea.
 
Reconciliation na wamasai Ngorongoro itafanyika lini baada ya Mahakama kusema kuwa Tangazo la kuwahamisha maasai Ngorongoro lilikuwa BATILI?
Hapo ndiyo utaelewa kuwa mama Samia anafata kanuni na sheria.

Nani alithubutu kuiolpinga serikqli ya Nyerere iliyohamisha halaikibya watu kwa nguvu? Wakati wa vijiji vya ujamaa.

mwenyewe umeandika "Tangazo li1ikuwa batili". Hiyo inamaanisha kuwahamisha Siyo batili bali zifatwe sheria.

Mbona wengi sana wameondoka kwa hiyari yao na wameanza maisha mapya mwaka wa pili huu.
 
Hqpo ndiyo utaelewankuwa mama Sqmiq qnqfqtw kwnuni nansheria.

nqni alith7butu I uishitak8 serikqli ya Nyerere iliyohamishq watu kww halqiki, wakqti wa vijiji vyw ujqmqq?

mwenyewe umeandika "Tangazo li1ikuwa batili". Hiyo inamaanisha kuwahamisha Siyo batili bali zifatwe sheria.

Mbona wengi sana wameondoka kwa hiyari yao na wameanza maisha mapya mwaka wa pili huu.
Rudi edit ueleweke, mbona kama umevurugwa na Hy comment?
 
Hakuna mwenye uwezo wa kuziishi hizo R nne huko CCM... acheni kudandia misamiati msiyoielewa wala kuiweza!
 
Anazielewa sana na anazitenda kwa vitendo kila siku, sema wengi hamuelewi tu.

R 4 si za kuzungumzwa kwa maneno tu, ni vitendo.

..i guess kila mtu na kiwango chake cha uelewa.

..wewe unaona Maza ametekeleza hicho anachoita reconciliation.

..mimi naona Maza hatekelezi reconciliation, na haelewi maana ya dhana hiyo.

..kila mtu abaki na mtizamo wake.
 
..i guess kila mtu na kiwango chake cha uelewa.

..wewe unaona Maza ametekeleza hicho anachoita reconciliation.

..mimi naona Maza hatekelezi reconciliation, na haelewi maana ya dhana hiyo.

..kila mtu abaki na mtizamo wake.
Haha mtu anaimba Resilience huku anachamba na kuparua watu wanaotumia uhuru wao wa mawazo mara Kuwaita vijamhuri na hasira juu!! Hamna mwenye akili huko CCM wakuweza kutafsiri hizo R nne kifasaha zaidi ya kutafuta sifa tu!
 
Aidha SSH anataka hizo 4R kwa dhati na moyo safi kabisa lakini kuna watu ndani ya CCM hawazitaki, au SSH anatuhadaa wananchi kwa hizo 4R kuvuta muda mpaka 2025.

Kwa maoni yangu, tutamwona SSH halisi baada ya 2025. Na ikiwa ni CCM ndio hawataki hizo 4R basi tumwombee mheshimiwa Rais wetu, kwasababu watafanya juu chini kumkwamisha.
 
Tumesikia, mwambie Watanzania wanataka katiba mpya,ashushe Bei ya vifaa vya Ujenzi na vyakula,ahakikishe umeme na Mafuta ya vyombo vya moto yanapatikana, arejeshe BimaToto Afya kadi, apeleke vitabu vya kutosha na Waalimu mashuleni, ahakikishe Madawa yanapatikana mahospitalini na kukamilisha Mswada wa Bima kwa wote.

Akifanya hayo tutamsikiliza siyo ngonjera za 4R.

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom