Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 365,195
- 843,331
unapoalikwa kwenye sherehe kaa kiti cha nyuma ili ukumbi ukishafurika waalikwa utafutwe kule uliko ufuatwe ushikwe mkono na kupelekwa siti ya mbele! Hii ni heshima pia ni sifa njema na ni hitaji muhimu la mwanadamu katika kudhihirisha thamani yako kwao
Ila kama ukialikwa kwenye karamu ukakuta viti havijajaa usikimbilie kukaa viti vya mbele, waepuke wanaokuhimiza kwenda kukaa huko, hawakutakii mema kwakuwa ukumbi utakapofurika waalikwa na ukafuatwa na kuambiwa hiki si kiti chako, twende kule nyuma tumeluandalia kule! Hii ni aibu, hii ni dhihaka na sifa hasi, wenye tafakuri wengi huliepuka hili
Habari za wiki hii zinasikitisha, zinakatisha tamaa hakuna msisimko ni habari mbaya kila kona...huu ni mwendelezo wa miezi na miezi wa kutibua na kuharibu kila kitu
Ni kilio kila kona kuwa uchumi unaporomoka, si kutoka kwetu sisi tuliopewa jina la wachochezi bali kwa washika dau na nguli wa biashara na uchumi
Biashara zinakufa, vitega uchumi vingi vinadorora, mali za pesa mingi zinauzwa kwa bei ya kutupa...nchi imeanza kuchechema na kuchechemea
hatuna habari njema tena za kujenga Taifa bali kila kinachosikika ni msiba wa kiuchumi biashara na kipato mahali fulani, ni habari za watu kutumbuliwa na kuswekwa ndani, ukiangalia kwa jicho la kiroho ni kama msiba mmoja mkubwa sana....tunapita katika bonde la uvuli wa mauti
kama ulikimbilia kukaa mbele wakakusifia ulikosea sana kuwaamini, kitambo si kirefu utashikwa mkono uonyeshwe kiti chako halisi....ni falsafa ya kiti usikarike ukatuharibia karamu
Tunachanja kuelekea mbugani....kamwe na kamwe milele na milele mchimba kaburi huingia mwenyewe