Faida ya kuishi duniani ni ipi kama tulizaliwa ili tufe?

Mangi shangali

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
533
815
Habari zenu,

Natumaini wote wazima.

Huwa najiuliza swali hili kila siku. Na jibu sijawahi kupata, sasa kuna umuhimu gani wa kuishi duniani hali ya kuwa utakufa?

Biblia inasema kuwa Adamu na Hawa walikula tunda pale edeni eti ndo sababu tunakufa. Ina maana kuwa kifo hakikuwa kabla ya kula lile tunda na hata sijui ni tunda gani hilo, biblia imetuficha kutupa ukweli.

Sasa kifo na tunda linahusiana na nini? Kama MUNGU hakutaka Adam na Hawa wale lile tunda ya nini aliliweka kwenye bustani ya edeni? Majaribio mengine bana.

Hilo tunda lina ubaya gani? Kitu umekiumba kwanini ukataze kisiliwe? Biblia imetudanganya hapo.

Jamani hata kwa akili ya kawaida kweli upande mazao yako shambani halafu ukataze familia yako kula kweli inakuja? Biblia imeficha ukweli.

Hivi kweli uzae watoto wako halafu uje kuwauwa kisa hawajakutii au hawajafanya utakacho??

Kama tuliumbwa ili tufe ina faida gani kuishi duniani. MUNGU angetuuliza kila mmoja kama utakubali kuishi ili uje kufa baadae kuliko kutufanyia umafia kama huu.

Mtu unahangaika kutafuta maisha kwa kila hali hata muda mwingine hupati milo yako vizuri ili kujibana upate maisha mazuri, sasa unafanya yote ya nini wakati utakufa?

Mambo haya yanachanganya kichwa sana.
 
Ni hivi kijana Mungu alimuumba binadamu na lengo la Mungu ni kwamba binadamu asife, kifo kilikuja baada ya binadamu kutenda dhambi ya kula lile tunda ambalo lilikuwa la kutambua mema Na mabaya Na kabla ya kula tunda binadamu alikua haujui ubaya wowote so kula tunda kulifanya binadamu aondoke kwenye lengo la Mungu Kwa kuujua ubaya, na ubaya ndio uliozaa mauti so mauti ilikuja baada ya binadamu kuujua ubaya automatically kifo kikatokea
 
Ni hivi kijana Mungu alimuumba binadamu na lengo la Mungu ni kwamba binadamu asife ,kifo kilikuja baada ya binadamu kutenda dhambi ya kula lile tunda ambalo lilikuwa la kutambua mema Na mabaya Na kabla ya kula tunda binadamu alikua haujui ubaya wowote so kula tunda kulifanya binadamu aondoke kwenye lengo la Mungu Kwa kuujua ubaya,na ubaya ndio uliozaa mauti so mauti ilikuja baada ya binadamu kuujua ubaya automatically kifo kikatokea
Sasa hilo tunda lilikuwa bustani la kazi gani??
 
Unajua elimu ya kiroho watu hawaijui vizuri, kwanza unatakiwa utambue tunakufa mwili lakini nafsi ni immortal yani haifi so sisi binadamu wote tulishaumbwa toka zamani Kwa iyo kuna transition kuanzia rohoni kuja kwenye mwili then rohoni tena kwenye u milele Kwa iyo sasa Mungu alipoona binadamu kaujua upande wa pili wa ubaya Na kumbuka Mungu kiasili hakai na ubaya wowote so ili kutuokoa kwenye hii dhambi ndipo akamleta yesu ili aweze kutusaidia kuuona uzima ule wa milele yani kufanya restoration
 
Tafuta biblia zilizo halali utajua maana ya Tunda, achana na hizo nakala za kihuni walizotafsiri VATICAN kwa kuficha ficha mambo kwa maslahi yao.

Mtu wa kwanza hakuitwa Adam wala mkewe hakuitwa eve maana hawakuwa na asili ya Uzungu, pili hawakuishi huko walikotuaminisha hawa wachungaji na wanasayansi uchwara.

Tatu Tunda maana yake ilikuwa ni maarifa/Neno la ujuzi wa kutambua mambo fulani hapa dunian, na Mti ulito toa hayo matunda ni Malaika ambao waliishi dunian na walikuwa na mission zao hapa hapa dunian.

Mtu wa kwanza alipewa ONYO asiwasiliane na hao malaika wala kuwaomba wampe/wamwambie Habari za maarifa waliyonayo ambayo walukatazwa kuyajua maana yalikuwa nje ya uelewa wao(Tunda).

Baada ya kuumbwa kwa mwanamke ambaye biblia za uongo zinamuita eva/hawa huyu hakuumbwa kwa udongo kama Adam bali aliumbwa kutokana na Imagination+mawazo ya Adamu kuhusu uwepo wa kiumbe kitakachofanana nayeye kitakachomtoa upweke hivyo eva aliumbwa kwa staili hii.

Kwakuwa Eva hakuwa na Uelewa sawa ama nguvu sawa na adamu bali alishawishika na kiumbe ambacho biblia zenu zinasema ni nyoka(Dragon) ambaye ndiye alimshawishi eva na eva ndiye wa kwanza kuyasikiliza maarifa ya wale malaika walioambiwa wasiyasikie na baadae akamueleza Adam, hapa ndipo chanzo cha maovu kilipoanza.

Adam hakufa kama tunavyodanganywa bali alipewa laana kwa wazawa wake na hata eva hakufa tafuta ktk biblia yako hutoona maala wanaeleza hili jambo zaid ya kudanganya kuwa adam alikufa na umri wa miaka fulan which is nonsense.

Unatakiwa ujuwe kuwa Adam mission yake aliyoletwa dunian ilikuwa ni kuongeza idadi ya malaika waliosaliti ambao idadi yao ilitakiwa kuwa replaced na wana wa adam atakao wazaa na mkewe maana Adamu nae kabla ya kuumbiwa mwili alikuwa ni sehemu ya malaika, baada ya anguko la shetan na wenzie ndipo ikaja sababu ya adamu kushushwa dunian na akafanyiwa mwili ili aweze kuendeleza uumbaji wa malaika wapya(wanadamu).

Idadi inayotakiwa kwa wana wa adamu kureplace idadi ya malaika waliosaliti mbingu inajulikana na huenda ikatimia muda ukifika.

Shida za dunia hazitokwisha na hizo raha mnazotamani hazitopatikana maana huyo kiumbe anaeitwa shetan hataki idadi ya wana wa adamu itimie maana ikitimia na ule mwisho utafika na hukumu kwa shetan na wafuasi wake itafika.

Shetan si mjinga kuwapotosha watu na kuwafanya wamsaliti Muumba ili tu idadi isifikie na malengo ya shetani kuutawala ulimwengu yaendelee uku idadi ya wana wa adamu ikiendelea kudhorota na anguko la wengi liwepo.

Tutafute elimu nje ya box, Hilo kanisa la kizungu la Katolic wakishirikiana na madhehebu yote na dini zote hawa ndio wahuni nambari moja waliopotosha Biblia ya kweli kwa kufuta baadhi ya vitabu na vingine kuvipotosha kwa kuedit na kuweka uongo mwingi maana hawa wote wako chini ya shetan kuhakikisha wana wa Adamu hatuijui kweli na hatuifikii ile idadi inayotakiwa kureplace jeshi la shetani.

Tuendeleeni kushabikia mamipira, maushenzi ya kubishiana dini ya nani ndio sahihi, kuuwana sisi kwa sisi, kujadiri uwepo wa Mungu na ujinga mwingne tunajichelewesha sisi wenyewe
 
Tafuta biblia zilizo halali utajua maana ya Tunda, achana na hizo nakala za kihuni walizotafsiri VATICAN kwa kuficha ficha mambo kwa maslahi yao.

Mtu wa kwanza hakuitwa Adam wala mkewe hakuitwa eve maana hawakuwa na asili ya Uzungu, pili hawakuishi huko walikotuaminisha hawa wachungaji na wanasayansi uchwara.

Tatu Tunda maana yake ilikuwa ni maarifa/Neno la ujuzi wa kutambua mambo fulani hapa dunian, na Mti ulito toa hayo matunda ni Malaika ambao waliishi dunian na walikuwa na mission zao hapa hapa dunian.

Mtu wa kwanza alipewa ONYO asiwasiliane na hao malaika wala kuwaomba wampe/wamwambie Habari za maarifa waliyonayo ambayo walukatazwa kuyajua maana yalikuwa nje ya uelewa wao(Tunda).

Baada ya kuumbwa kwa mwanamke ambaye biblia za uongo zinamuita eva/hawa huyu hakuumbwa kwa udongo kama Adam bali aliumbwa kutokana na Imagination+mawazo ya Adamu kuhusu uwepo wa kiumbe kitakachofanana nayeye kitakachomtoa upweke hivyo eva aliumbwa kwa staili hii.

Kwakuwa Eva hakuwa na Uelewa sawa ama nguvu sawa na adamu bali alishawishika na kiumbe ambacho biblia zenu zinasema ni nyoka(Dragon) ambaye ndiye alimshawishi eva na eva ndiye wa kwanza kuyasikiliza maarifa ya wale malaika walioambiwa wasiyasikie na baadae akamueleza Adam, hapa ndipo chanzo cha maovu kilipoanza.

Adam hakufa kama tunavyodanganywa bali alipewa laana kwa wazawa wake na hata eva hakufa tafuta ktk biblia yako hutoona maala wanaeleza hili jambo zaid ya kudanganya kuwa adam alikufa na umri wa miaka fulan which is nonsense.

Unatakiwa ujuwe kuwa Adam mission yake aliyoletwa dunian ilikuwa ni kuongeza idadi ya malaika waliosaliti ambao idadi yao ilitakiwa kuwa replaced na wana wa adam atakao wazaa na mkewe maana Adamu nae kabla ya kuumbiwa mwili alikuwa ni sehemu ya malaika, baada ya anguko la shetan na wenzie ndipo ikaja sababu ya adamu kushushwa dunian na akafanyiwa mwili ili aweze kuendeleza uumbaji wa malaika wapya(wanadamu).

Idadi inayotakiwa kwa wana wa adamu kureplace idadi ya malaika waliosaliti mbingu inajulikana na huenda ikatimia muda ukifika.

Shida za dunia hazitokwisha na hizo raha mnazotamani hazitopatikana maana huyo kiumbe anaeitwa shetan hataki idadi ya wana wa adamu itimie maana ikitimia na ule mwisho utafika na hukumu kwa shetan na wafuasi wake itafika.

Shetan si mjinga kuwapotosha watu na kuwafanya wamsaliti Muumba ili tu idadi isifikie na malengo ya shetani kuutawala ulimwengu yaendelee uku idadi ya wana wa adamu ikiendelea kudhorota na anguko la wengi liwepo.

Tutafute elimu nje ya box, Hilo kanisa la kizungu la Katolic wakishirikiana na madhehebu yote na dini zote hawa ndio wahuni nambari moja waliopotosha Biblia ya kweli kwa kufuta baadhi ya vitabu na vingine kuvipotosha kwa kuedit na kuweka uongo mwingi maana hawa wote wako chini ya shetan kuhakikisha wana wa Adamu hatuijui kweli na hatuifikii ile idadi inayotakiwa kureplace jeshi la shetani.

Tuendeleeni kushabikia mamipira, maushenzi ya kubishiana dini ya nani ndio sahihi, kuuwana sisi kwa sisi, kujadiri uwepo wa Mungu na ujinga mwingne tunajichelewesha sisi wenyewe
Noma sana
 
Ni hivi kijana Mungu alimuumba binadamu na lengo la Mungu ni kwamba binadamu asife ,kifo kilikuja baada ya binadamu kutenda dhambi ya kula lile tunda ambalo lilikuwa la kutambua mema Na mabaya Na kabla ya kula tunda binadamu alikua haujui ubaya wowote so kula tunda kulifanya binadamu aondoke kwenye lengo la Mungu Kwa kuujua ubaya,na ubaya ndio uliozaa mauti so mauti ilikuja baada ya binadamu kuujua ubaya automatically kifo kikatokea
Hoja dhaifu kama hizi ndio zinafanya maelezo ya wasioamini uwepo wa Mungu yaonekane yana mantiiki.

yaani Mungu muweza ya yote alishindwa kubaini kwamba ipo siku binadamu aliyemuumba atakuja kutenda dhambi?.
 
Tafuta biblia zilizo halali utajua maana ya Tunda, achana na hizo nakala za kihuni walizotafsiri VATICAN kwa kuficha ficha mambo kwa maslahi yao.



Tuendeleeni kushabikia mamipira, maushenzi ya kubishiana dini ya nani ndio sahihi, kuuwana sisi kwa sisi, kujadiri uwepo wa Mungu na ujinga mwingne tunajichelewesha sisi wenyewe
Paukwaaa....
 
Back
Top Bottom