Mangi shangali
JF-Expert Member
- Feb 9, 2023
- 533
- 815
Habari zenu,
Natumaini wote wazima.
Huwa najiuliza swali hili kila siku. Na jibu sijawahi kupata, sasa kuna umuhimu gani wa kuishi duniani hali ya kuwa utakufa?
Biblia inasema kuwa Adamu na Hawa walikula tunda pale edeni eti ndo sababu tunakufa. Ina maana kuwa kifo hakikuwa kabla ya kula lile tunda na hata sijui ni tunda gani hilo, biblia imetuficha kutupa ukweli.
Sasa kifo na tunda linahusiana na nini? Kama MUNGU hakutaka Adam na Hawa wale lile tunda ya nini aliliweka kwenye bustani ya edeni? Majaribio mengine bana.
Hilo tunda lina ubaya gani? Kitu umekiumba kwanini ukataze kisiliwe? Biblia imetudanganya hapo.
Jamani hata kwa akili ya kawaida kweli upande mazao yako shambani halafu ukataze familia yako kula kweli inakuja? Biblia imeficha ukweli.
Hivi kweli uzae watoto wako halafu uje kuwauwa kisa hawajakutii au hawajafanya utakacho??
Kama tuliumbwa ili tufe ina faida gani kuishi duniani. MUNGU angetuuliza kila mmoja kama utakubali kuishi ili uje kufa baadae kuliko kutufanyia umafia kama huu.
Mtu unahangaika kutafuta maisha kwa kila hali hata muda mwingine hupati milo yako vizuri ili kujibana upate maisha mazuri, sasa unafanya yote ya nini wakati utakufa?
Mambo haya yanachanganya kichwa sana.
Natumaini wote wazima.
Huwa najiuliza swali hili kila siku. Na jibu sijawahi kupata, sasa kuna umuhimu gani wa kuishi duniani hali ya kuwa utakufa?
Biblia inasema kuwa Adamu na Hawa walikula tunda pale edeni eti ndo sababu tunakufa. Ina maana kuwa kifo hakikuwa kabla ya kula lile tunda na hata sijui ni tunda gani hilo, biblia imetuficha kutupa ukweli.
Sasa kifo na tunda linahusiana na nini? Kama MUNGU hakutaka Adam na Hawa wale lile tunda ya nini aliliweka kwenye bustani ya edeni? Majaribio mengine bana.
Hilo tunda lina ubaya gani? Kitu umekiumba kwanini ukataze kisiliwe? Biblia imetudanganya hapo.
Jamani hata kwa akili ya kawaida kweli upande mazao yako shambani halafu ukataze familia yako kula kweli inakuja? Biblia imeficha ukweli.
Hivi kweli uzae watoto wako halafu uje kuwauwa kisa hawajakutii au hawajafanya utakacho??
Kama tuliumbwa ili tufe ina faida gani kuishi duniani. MUNGU angetuuliza kila mmoja kama utakubali kuishi ili uje kufa baadae kuliko kutufanyia umafia kama huu.
Mtu unahangaika kutafuta maisha kwa kila hali hata muda mwingine hupati milo yako vizuri ili kujibana upate maisha mazuri, sasa unafanya yote ya nini wakati utakufa?
Mambo haya yanachanganya kichwa sana.