Fahamu kuhusu Uchawi wa Mapenzi (Limbwata)

Fahamu kuhusu Uchawi wa Mapenzi (Limbwata)

Habari zenu Great thinkers.

Najua wapo watu ambao hawaamini kwamba katika mapenzi kuna kitu kinaitwa limbwata. Hata mimi nilikuwa siamini kabisa kuhusu hili suala lakini hivi karibuni nimeamini.

Nlikuwa naishi kwenye mkoa mmoja hivi miaka kama miwili au mitatu iliyopita.

Katika kijiji kile alikuwepo baba mmoja mwenye mke na watoto wanne.

Huyu baba alikuwa mtu wa heshima na pesa zake za kumtosha kubadilisha mboga....kifupi ni kwamba hakuwa na dhiki.
Mke wake sasa.....alikuwa ni kicheche balaa....alikuwa anagawa utadhani sio mke wa mtu. Ilifika hatua akawa anatoka na kijana mmoja jirani tu na nyumbani kwake na huyo kijana alikuwa na mkewe kabisa.

Basi ilikuwa yule kijana akimfuma yule mwanamke na mwanaume (hawara mwingine) anamshushia kipigo hadharani....siku nyingine kamdunda weee akamburuza hadi nyumbani kwake akafika getini kamsukumizia ndani....na mumewe yupo ndani!

Nilikuwa napata shida najiuliza hivi huyu baba ni mzima kweli? Maana katika kipindi chote sikuwahi kusikia ana mgogoro na huyo mkewe mzinzi.... Siwezi kusema hana akili timamu maana majukumu yake ya kiofisi alikuwa anayatekeleza vizuri kabisaa.

Eti wana MMU nisaidieni kama hili sio limbwata basi ni kitu gani? Siwezi kukubali kwamba eti ilikuwa ni ndoa ya kawaida hii.
Wewe mwenzangu huko mtaani kwako umewahi kukutana na matukio kama haya?
 
Kuna tofauti gani kati ya mtu kudata kwenye mapenzi kwa mwenzake na limbwata?
 
ni mapenzi tu hayo... hamna limbwata asee!!! mahaba niue, mtu anapewa kila kitu kwanini asiweuke...
 
Limbwata lipo kitheory zaidi! Tatizo ni akili mbovu ktk mapenzi, kumkuta mtu uko vizuri ktk utendaji wake wa kazi za kiofisi haimanishi ni mzuri ktk ndoa au mahusiano yake kimapenzi!

Kuna me ni mapoyoyo sana!
 
Sijui kama hilo neno "limbwata" linafaa ila kuna kitu kama hicho kinatumiwa na watu (sana ni wanawake)
 
Limbwata lipo kitheory zaidi! Tatizo ni akili mbovu ktk mapenzi, kumkuta mtu uko vizuri ktk utendaji wake wa kazi za kiofisi haimanishi ni mzuri ktk ndoa au mahusiano yake kimapenzi!

Kuna me ni mapoyoyo sana!

Ina maana huyo baba alikuwa poyoyo kiasi cha kushindwa kujitetea kweli?
 
Back
Top Bottom