Fahamu athari ya jina lako katika mapenzi

Fahamu athari ya jina lako katika mapenzi

Hakuna kitu kama hicho, hii ni elimu ya nyota ambayo inasema binadamu wapo wa aina 4 kwa u' nafsi yake . Aina ya maji, aina ya upepo, aina ya mchanga(udongo) na aina ya moto. Wanapoangalia majina wanaangalia na hii asili ya u' nafsi wako.

Wanadai mwenye asili ya Moto hafai kumuoa au kuolewa na asili ya udongo, kwani moto na udongo unazalisha fukuto. Bali moto unaendana na maji kwa sababu maji yanapoza. Na mwenye asili ya upepo na moto hawaendani kwani upepo unakoleza moto, kwa hiyo fukuto lao litakuwa kubwa zaidi, na hawaishii hapo tu utapangiwa mpaka muda wa kuoa. Kama kuoa ni alfajiri, au mchana au usiku na saa vilevile utapangiwa.

Mbeleni usije ukashtuka ukapewa pete yenye jiwe la rangi nyekundu/njano/kijani ukaambiwa rangi moja wapo ni rangi yako ya bahati. Kwa kifupi hii ni elimu ya nyota na haina faida wala ukweli isipokuwa utajitesa tu wewe mwenyewe.
 
amina anampenda sana saidi na mapenzi yao ni ya dhati,lakini hapa kwa khadija na juma hakuna mapenzi japo juma anampenda khadija asiyempenda juma
Hapo Kwa Juma na khadija umetumia kigezo au kanuni gani, sijaelewa
 
We nawe unatudanganya hapa, mbona tuna mifano mizuri kwenye jamii yetu ambapo tumeona wapenzi hawajadumu ingawa utofauti wa majina yao ni mkubwa, mfano Abdul (diamond) na wema sepetu, diamond na zali na wapo kibao tu


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Fact yangu ni kwamba ulioongea hapo huo ni upuuzi na nia ya kuwaibia watu wenye matatizo ya mahusiano
Jina halipendi unaopenda ni moyo ungeniambia kuwa jina la mtu linaweza kusadifu tabia yake kidogo inamantiki japo hii dhana inaande kupotea kabisa

Ingekuwa hivyo kusingekuwa na maumivu ya mapenzi kwa sababu wote mnakuwa hamna hisia sababu ya majina hayajapishana herufi saba,

Mapenzi ni hisia inayoanzia kwenye macho hadi moyoni

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtoa Mada kama si KWA MGANGA MAPENZI sijui,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom