FACT: Tanzania ya Magufuli haina Industrial Strategy

FACT: Tanzania ya Magufuli haina Industrial Strategy

VIWANDA TRANS!!!!!

ulisha wahi panda gari kutoka unapo pajua kwenda usipo pajua???

Iko hivi.......

katika maisha kuna kipindi tunapanda usafiri either daladala, bus, ama bodaboda huku atujui tunako kwenda, ila tutokapo tunapajua vizuri tu!!!!

hufika mahala ukasikia kondakta anataja vituo, kwakuwa wewe hupajui unapokwenda basi unamuuliza jirani yako pembeni kwenye siti "hivi ni hapa ndo napo kwenda ama kushuka??? ndipo panaitwa ........." nayeye anakupa majibu "sijui kama ni hapa" labda tumuulize konda,"

konda naye yuko mbaaaali........

maana mlundikano wa watu kwenye gari unamfanya asifikike kiraisi!!! hata anapotaja vituo,..... sauti yake haifiki kwa haraka kwa abiria wake!!!

anapiga story huko mbele, mara apigane na makonda wenzake!!! mara afokeane na wanafunzi wasio na nauli za kutosha, mara abadilishe muziki kwa karimoti kake aliko kashika mkononi,

mara agombane na mama mwenye mikungu yake ya ndizi iliyopakizwa kwenye gari lake kwamba amelipia kidogo aongeze hela maaana mzigo mkubwa, wakati anapanda walisha kubaliana bei vizuri tu,

so yuko bizy na mambo mengine meeengi kuliko kujua abairia wake wanapaswa kushuka wapi!!!

mnaendaaaaaaa mpaka mwisho....... wengi mnapitishwa vituo, maaana dereva anakanyaga mafuta na yeye ndio anaamini anajua njia na hakuna mwingine!!!

inafika mahala dereva na konda wanaaza kulaumiana mbona ulikua unambii kusimama,??? hii nikutokana na wingi wa abiria waliopitishwa vituo,!!!! konda anakasirika abiria wanakasirika, dereva anashuka kwenye gari anaendakukaa pembeni anawatazama tu!!!


hii inakugharim wewe abiria kutafuta usafiri wa kukurudisha kwenye kituo ulichopitilizwa!!!!


twendeni tu!!! tukipitilizwa tutarudi kwa miguuu!!! nihayo kwa leo wapendwa wangu!!!!
 
Mkuu, unaamka usiku wa manane badala ya kutafuta watoto wewe unamuwaza mwanaume mwenzako?
Mkuu natumaini uko poa mawazo mbadala ndo yanajenga nchi.issue ya viwanda inahitaji kuona mbali tungeanza na kuwa assembly park ya vipuri kutoka nje then from pale tuanze process ya industrialization.natamani issue ya viwanda isiwe kisiasa ila waachiwe think tank kufikiria
 
Swali lako nila msingi. Lakini JF ya siku hizi siyo ile. Hivyo tegemea matusi tu.

Lakini niliwahi sikia mahala flani kwamba hawa jamaa wa buku saba wametafutiwa shamba maeneo ya Rufiji ili wakalime. Ngoja tusubiri labda ni kweli maana imagine they get paid Tsh 7k everyday, this is a misuse of public funds.

I blame it on Maxine Mello

no one else
 
Kuhusu viwanda ilikua danganya toto hili mamburula yampe kura...na alifanikiwa kupewa kura na mamburula ya lumumba...anadhani kuanzisha viwanda ni sawa na kuagiza beer bar
 
Mkakati wa viwanda uko katika nyaraka mbili: (1) Sera iliyopo sasa ya maendeleo ya viwanda (Strategic Industrial Development Policy - SIDP) iliyoanza kutumika 1996. Hii sera inasema viwanda vitajengwa na sekta binafsi na jukumu la serikali ni kuweka mazingira mazuri kwa maendeleo ya viwanda. Jambo la ajabu ni kwamba tangu sera hii ianze kutumika idadi ya viwanda imepungua kwa kiasi kikubwa. (2) Mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano, 2016/17-2020/21 (FYDP2), ambao umekuja na 'mkwara' wa kauli mbiu kwa Kimombo: "Nurturing Industrialization for Economic Transformation and Human Development". FYDP2 tayari imeanza 'kutekelezwa' lakini jambo la ajabu tena ni serikali kutokuwa na mkakati wa kuboresha na kuendeleza sekta ya kilimo ambayo ni mhimili muhimu wa maendeleo yoyote ya viwanda. Katika bajeti ya mwaka huu kwa mfano, fedha 'kiduchu' iliyotengwa kwa ajili ya maendeleo ya kilimo ni uthibitisho kuwa FYDP2 ni usanii mtupu.

Mipango yetu huwa inabaki kwenye shelf za wizara
 
Sasa wewe Unataka strategy gani zaidi ya ile aliyotoa Mkulu ya kuwahimiza wa TZ wafyatue watoto wengi kwenye 'viwanda' vya kwenye kaya zao?!

HAHAHAAAAA, hihihiiiiii 😀😀😀😀😀😀😀 kumbe alikuwa anamaanisha viwanda vya kwichi, kwichi, Kwichi? nchi yangu inafurahisha sana 😛😛😛
 
Priority ya sasa ni kuhamia Dodoma, na hii inatarajiwa kukamilika 2020
 
Wewe elewa tu kuwa Tanzania ya viwanda inakuja, na pia Tanzania ya Magufuli ni Tanzania ya viwanda.

Mambo ya strategy tuwaachie wazungu. Mifuko ya jamaa imezuia fao la kujitoa ili wajenge viwanda. Ni viwanda, viwanda, viwanda. Tunaweza kuweka viwanda kila kata kama shule za sekondari. Hapa Kazi Tu
Kuweka viwanda kila kata ni Strategy.
Kumbe hata maana ya Strategy hujui?
 
Wewe elewa tu kuwa Tanzania ya viwanda inakuja, na pia Tanzania ya Magufuli ni Tanzania ya viwanda.

Mambo ya strategy tuwaachie wazungu. Mifuko ya jamaa imezuia fao la kujitoa ili wajenge viwanda. Ni viwanda, viwanda, viwanda. Tunaweza kuweka viwanda kila kata kama shule za sekondari. Hapa Kazi Tu
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13]
 
1 Nguvu za umeme unaendana na viwanda?
2 Wawekezaji au Serikali ndio itakayojenga viwanda?
Maoni yangu sioni kama kweli kuna dalili ya kujengwa viwanda lakini ilikuwa ni njia ya kupata kura wakati wa kampeni tu. Siasa inauza maneno mazuri kuliko hata mwanaume anavyo mtongoza mwanamke.
Hata cha viwanda wala nini labda viwanda uchwara.
 


Kama ipo ileteni hapa tuone iliandikwa na nani na how ambitious is it na je inaendana na hii karne tuliyopo au bado iko kwenye zama za stone age?

Nishatafuta sana hii kitu kwenye website za wizara na serikali sijaipata

This document is harder to find than ile ya muungano wa Tanganyika na Unguja

Kwa mujibu wa dictionary; Strategy - an elaborate and systematic plan of action.

Mkuu umefikiria jambo ambalo nimekuwa nalifikiria kwa muda mrefu, watu weusi tumekuwa kama tumewekewa kitambaa cheusi machoni, jambo kama la viwanda halitakiwi kuwa la mtu mmoja ambaye atakaa madarakani kwa muda wa miaka mtano au kumi, linatakiwa kuwa jambo la kitaifa ili hata chama chochote kikiingia madarakani kiendelezee pale serikali iliyopita inapokuwa imeishia. Kwa bahati mbaya jambo hili halifanyiki.

Nimekuwa nikisoma vitabu vya entrepreneurship vya India, ukifuatilia unakuta mkakati wa serikali ya India unaanzia kwenye entrepreneurship development Program. Hawa entrepreneurs ndio baadae wanakuja kuendeleza na kuanzisha viwanda vipya. Baada ya hapo wanaanzisha indusrial zones, hizi zinawekewa facilities zote yaani maji, umeme na miundombinu ya usafirishaji n.k. Siyo hivyo tu, wana vipaumbele vyao na incentives za kuwawezesha wananchi wao katika suara zima la uanzishaji viwanda.

Sisi huku mipango kama hiyo haipo na kwa bahati mbaya ktk utawala huu watu wamezuiwa kufikiri na kutoa maoni yao, kila mtu anafikiri kama mkulu anavyotaka wafikiri, kwa hiyo mambo makubwa kama STRATEGY sahau.
 
Mkuu natumaini uko poa mawazo mbadala ndo yanajenga nchi.issue ya viwanda inahitaji kuona mbali tungeanza na kuwa assembly park ya vipuri kutoka nje then from pale tuanze process ya industrialization.natamani issue ya viwanda isiwe kisiasa ila waachiwe think tank kufikiria

Katika utawala huu hakuna mtu anaruhusiwa kufikiri tofauti, huoni mawaziri wa sheria wanajifanya hawazijui sheria na katiba? huoni wachumi wanajifanya hawazijui namba? so in this administration people are not allowed to think out of the box, they are thinking and saying what the boss want to hear, and that is ridiculous and self destructive.
 
Back
Top Bottom