EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

Status
Not open for further replies.

AshaDii

Platinum Member
Joined
Apr 16, 2011
Posts
16,189
Reaction score
18,113
Habari wana JF,

Nimebahatika kuwasiliana na Mbunge wa Kigoma kwa ticket ya CHADEMA, Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe; na kuwasilisha ombi langu la kumhoji 101 kwa kupitia mtandao huu wa JF kwa ruhusa ya Maxence Melo mmoja wa JF Founder. Bahati nzuri sana kiu yangu juu ya kuweza pata hiyo nafasi ya kuweza interview imekuwa na muitikio chanya kutoka kwa Zitto mwenyewe. Namshukuru sana kwa hilo.

Nawasilisha utaratibu wa member yeyote wa JF kuweza kushiriki pia katika huu mjadala ambao naamini na kuwahakikishia kuwa utakuwa ni moto, wa kujenga, wa kupata majibu, wa kuridhisha (nikiweka matumaini makubwa hapa) ama kukera (hasa kwa wasio ridhika kirahisi) na pia kuweza kutoa majibu ya yale mengi ambayo tunajiuliza juu ya Mkuu Zitto ambaye bahati nzuri sana ni verified member wa hapa JF.

  1. Hii thread ndiyo imetoa taarifa hiyo na hapa hapa itatumika kukusanya maswali yoote kwa wale ambao wana kiu ya kuuliza maswali. Naomba nitadhaharishe kuwa maswali yawe ya msingi, ya kujenga na vilevile kuweza kupata majibu ambayo ni muhimu kwa jamii yetu.
  2. Comments zote za kejeli, matusi, kukashifu ama kuonekana sio msingi wala kutohusiana na hii hoja niliyowakilisha hapa itatolewa kwa msaada wa mods ( Paw, Roulette, Cookie, Fang, PainKiller na Silencer ambao nimewaarifu hapa sasa hivi kwa njia ya kuwa tag - Wakuu naomba msaada wenu wa dhati).
  3. Maswali yatakusanywa toka kurushwa kwa hii thread hadi pale itakapoonekana kuwa yapo ya kutosha ili nitakapowasiliana na Mkuu Zitto tuwe tayari tumejipanga kwa maswali ambayo yatakuwa faida kwetu, si leo tu bali hata hapo baadae.
  4. Naomba nisisitize kuwa mahojiano yatakuwa kati ya MIMI na Mkuu Zitto. Hivo nitajitahidi kuwakilisha vema na kuhakikisha kuwa nakusanya maswali ya wanachama yote na kuyaweka katika mlolongo ulio sawa. Kwa mukatadha huu - hii inakuwa kama 'golden chanc'e kuweza kuitumia kwa wale wote wenye kiu ya kuuliza maswali kwa kutaka kujua juu ya yale ambayo Zitto anajua/fikiria/panga.
  5. Baada ya kukusanywa kwa maswali taarifa itatolewa ya LINI hiyo 'Exclusive Interview' itafanyika. Hiyo thread itarushwa katika Jukwaa la Great Thinkers na kila mmoja ambaye ni member na non-member atakuwa na uwezo wa kufuatilia nini kinaendelea.

Ombi langu kwa members wote ambao wapo intersted:
-

Nilikuwa na kiu sana ya kuweza kupata nafasi ya kumhoji Mkuu Zitto kwa niaba ya members wa JF tokana na ukweli kuwa ni mmoja wa wanasiasa vijana ambaye huleta controversies nyingi juu yake na hoja zake. Wanachama wengi hupenda kuongea kwa niaba yake kana kwamba wamjua (it may be true or not); na kuwasilisha hoja zao kana kwamba ni za mwisho (final say).

Naomba ushirikiano wa kuniwasilishia maswali na hoja za msingi, na naomba tutumie hii fursa kuweza jua what Zitto is all about, what he thinks on certain issues, what he stands for, what he believes in AND why he thinks/ believes/stands for what ever it is that he postulates especially on what defines him... i.e POLITICS.

Natanguliza Shukrani kwenu.

Pamoja Saana,

AshaDii.


UPDATE:-

Nimetoa kipengele binafsi naona badala ya kuuliza maswali inasababisha kuenda nje ya topic. Bring it on wakuu ulizeni maswali yenu. Karibuni..

ZINGATIA:-

Mda wa kuweza kuwakilisha (ma)swali mwisho saa tano kamili ya usiku wa leo ya tarehe 19/11/2012. Asanteni kwa ushirikiano wenu.

 
Last edited by a moderator:
Mkuu nashukuru kwa jitihada ulizozifanya kwani hili ni jambo jema sana,lakini naona umejihami sana kiasi cha kutaka huyo Zitto aulizwe maswali unayotaka wewe au kwa lugha nyingine aulizwe maswali yanayokupendeza wewe na jamaa zao wenye mawazo kama yako.Hii inapoteza maana ya huu mjadala!
 
Mimi ningependa kujua kama Zitto anaujua mshahara wa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mshahara wa makamu wa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na ule wa raisi wa Zanzibar.

Na kama anajua mishahara yao, yeye kajuaje? Maana sisi wengine au nijiongelee mwenyewe, mimi sijui na nimekuwa nikitaka kujua tokea mwaka 2007 na mpaka leo hii bado sijajua na sijakutana na mtu anayejua kwa uhakika.

Na kama nikipenda kujua ni wapi pa kwenda? Na kama mishahara ya hao waheshimiwa haiwekwi wazi, sababu ya/za kutokuwekwa wazi ni nini/zipi hasa maana kwa ufahamu wangu sisi walipa kodi ndiyo tunalipa mishahara yao, na sisi ndiyo waajiri wao hivyo kimsingi tunastahili kujua tunawalipa kiasi gani kwa kazi wanazozifanya.

Nina mengi sana ya kusema na kuuliza kuhusiana na hili suala ila kwa kuanzia nadhani haya yanatosha kwa sasa. Nategemea Zitto atajibu maswali bila kukwepa wala kuurapa.
 
Bila ya shaka maangalizo yako yatazingatiwa na sisi tunasubiri kwa hamu sana hayo mahojiano.
 
zitto, ulisema hutogombea tena ubunge, je nani umemuandaa katika jimbo hilo au ndo unawaachia ccm?
 
Nyani Ngabu

Mkuu siwanasemaga mshahara ni siri ya mfanyakazi mwenyewe!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu siwanasemaga mshahara ni siri ya mfanyakazi mwenyewe!

Ngoja nikuulize: wewe unafanya kazi? Kama unafanya kazi mwajiri wako anaujua mshahara wako?

Na mwajiri wa raisi wa Tanzania ni nani?

Mbona nchi zingine mishahara ya viongozi wao wa juu inawekwa wazi na siyo siri?

Ina maana hao wa nchi zingine ni wajinga kuweka mishahara ya viongozi wao wazi kwa kila mtu kuijua?
 
Thanks. Mimi binafsi sijamjua Zito kwa jinsi ya udugu au urafiki ila kutokana na fikra na falsafa zake za jinsi ya kuleta maendeleo ya nchi yetu na kusimamia raslimali zetu. Amekuwa na uwezo mkubwa wa kujenga hoja na kusimamia kitu anachokiamini pamoja na upinzania mkubwa anaopata nje na ndani ya chama chake.

Swali langu kwa Mh. linajikita zaidi kwenye upatikanaji wa viongozi wa vyama vyetu hapa TZ.

Swali la Kwanza:
Yeye anafikiri ni mfumo gani wa kupata viongozi wa vyama vyetu kwa ngazi za juu kama M/kiti, Makamo M/kiti na Katibu Mkuu unafaa, wa kuteua na kupigiwa kura za wajumbe au kugombea na kupingiwa kura za wajumbe.

Swali la 2: Yeye kama mwanasiasa kijana katika jamii anauzungumuziaje uchaguzi viongozi wa CCM uliopita? Unaakisi matakwa ya TZ? Maana tulikuwa na kiu tumsikie.
 
Mkuu nashukuru kwa jitihada ulizozifanya kwani hili ni jambo jema sana,lakini naona umejihami sana kiasi cha kutaka huyo Zitto aulizwe maswali unayotaka wewe au kwa lugha nyingine aulizwe maswali yanayokupendeza wewe na jamaa zao wenye mawazo kama yako.Hii inapoteza maana ya huu mjadala!


Nikiri kuwa mimi pia nina maswali ya kumuuliza na hata nikipata nafasi ya kukaa naye face to face tukizungumza tu yaliyo msingi na ndani ya maswali ambayo ninayo inaweza chukua sio chini ya masaa mawili ama zaidi. Naamini ningefanya jitihada zaidi hiyo nafasi ningepata...

Kwa muktadha huo Sijajihami Mkuu... Nimeona ni kheri nitoe tahadhari mapema sababu ni mpitaji mzuri tu hapa JLS, najua ni namna gani watu wanakuwa na sumu kali wakiona jina la Zitto ama lolote lihusulo yeye. Najua kuwa bila tahadhari basi tunaweza kuwa na pages za kejeli na tusipate yaliyo msingi. Nakuhakikishia kuwa maswali yote nitawakilisha na ndiyo maana nikaona nisiwe mchoyo wa hiyo nafasi nihusishe na members pia. Hivo Tukutuku kama una swali uliza na litafikishwa...

Karibu sana.
 
Mie nataka aweke wazi msimamo wake hasa katika swala la kuwania uraisi 2015,je ni kweli ana nia hiyo na kama anayonia kwanini hafuati taratibu za chama ktk kvangaza nia badala yake ananukuliwa na vyombo vya habari mara kwa mara juu ya swala hilo? Je haoni kwa kufanya hivyo analeta mgawanyiko ndani ya cdm? Kuna tetesi kuwa anatumwa na ccm kufanya hivyo ili kupunguza nguvu ya cdm je ni kweli? Kama si kweli kwanini haweki mambo wazi na kuacha kufanya mambo yanayomfanya aonekane kama pandikizi ndani ya cdm?
 
Umefanya jambo zuri ila mipaka uliyoanza kuiweka inanitia shaka kidogo.Nisaidie kumuuliza swali hili,
1-Yale majina ya baadhi ya viongozi anaowatuhumu wanamiliki fedha haramu(nyingi)nje ya nchi kwa nini anabaki nayo ndani?Yeye kama Mtanzania mzakendo na nchi yake kwa nini kama anao ushahidi wa kutosha ameshindwa vipi kuwapeleka mahakamani na kuwafungulia mashitaka?
 
Ashadii - "maisha binafsi" ndiyo "msingi" wa "maisha ya kiongozi mwadilifu"...! Binadamu awaye yote anapojaribu "kuficha masiha yake binafsi" fahamu fika kuwa huyo binadamu anayo mapungufu makubwa sana "ki-uongozi"...!
 
Mwanangu Ashadii umeniudhi leo kwa mara ya kwanza. Inaonekana kama huyo Zitto wako ana matatizo mengi kiasi cha kuogopa baadhi ya mambo yasiguswe.

If indeed he is but a public figure hiyo protectionism ya nini? Hii maana yake ni kwamba unataka aulizwe anachotaka kuulizwa. Kwa mfano, kama ataulizwa ataoa lini au kwanini haoi na umri unakwenda kama kiongozi wa umma kuna ubaya gani? Maana wengi wanashangaa ni vipi ataweza kuongoza taifa iwapo hana hata uwezo wa kuwa na foundational unit yaani familia.

Pili kulikuwa na tetesi kuwa naye ameficha mafweza Uswisi. Hii inaweza kulenga kumchafua ili awagwaye waliofanya hivyo, je huoni kuwa hii ni nafasi adimu ya kuondoa shaka? Pia kama yeye ni mwanasiasa mahiri kwanini akingiwe kifua kama kichanga.
 
Ngoja nikuulize: wewe unafanya kazi? Kama unafanya kazi mwajiri wako anaujua mshahara wako?

Na mwajiri wa raisi wa Tanzania ni nani?

Mbona nchi zingine mishahara ya viongozi wao wa juu inawekwa wazi na siyo siri?

Ina maana hao wa nchi zingine ni wajinga kuweka mishahara ya viongozi wao wazi kwa kila mtu kuijua?

Mkuu mimi nafanya kazi na mwajiri wangu anajua mshahara wangu kwa kuwa yeye ndiye aliyeniajiri na ndiye anayeniandalia huo mshahara.Sisi kama wananchi ni kweli kabisa ni waajiri wa rais,lakini kuna utofauti kidogo kwa sababu there is no direct involvement in the supervision of our employee (Rais).Hata hivyo naamini ukienda ofisi ya rais utumishi unaweza kupata hizi taarifa bila shaka.
 
KWANINI ZITTO ULITUAHIDI UTATUTAJIA MAJINA YA WALIOFICHA FEDHA USWISS HUKUWATAJA
HUONI ULIDANGANYA BUNGE NA UMMA
Epuka kusema mbona fulani alitaja mkakaa kimya
au hayakuwa muhimu wakati wewe uliamua
2. Hukutuambia unaenda kuyataja kwenye tume teule uliyokuwa unapendekeza
3. Hugombei tena ubunge 2015 umemwandaa nani au unarudisha jimbo kwa ssm
 
Mkuu mimi nafanya kazi na mwajiri wangu anajua mshahara wangu kwa kuwa yeye ndiye aliyeniajiri na ndiye anayeniandalia huo mshahara.Sisi kama wananchi ni kweli kabisa ni waajiri wa rais,lakini kuna utofauti kidogo kwa sababu there is no direct involvement in the supervision of our employee (Rais).Hata hivyo naamini ukienda ofisi ya rais utumishi unaweza kupata hizi taarifa bila shaka.

Hakuna "direct involvement in the supervision of our employee" kivipi? No wonder tupo kwenye hali tuliyonayo!!!!

Na haya mambo ya "naamini ukienda ofisi ya rais utumishi unaweza kupata hizi taarifa bila shaka" ndiyo siyataki mimi. Kwanza unasema "unaamini", halafu unasema "unaweza", halafu katika sentensi hiyo hiyo unasema "bila shaka"!!

Good grief...wewe unajua au hujui?
 
Well said!!
Ashadii - "maisha binafsi" ndiyo "msingi" wa "maisha ya kiongozi mwadilifu"...! Binadamu awaye yote anapojaribu "kuficha masiha yake binafsi" fahamu fika kuwa huyo binadamu anayo mapungufu makubwa sana "ki-uongozi"...!
 
Ashadii - "maisha binafsi" ndiyo "msingi" wa "maisha ya kiongozi mwadilifu"...! Binadamu awaye yote anapojaribu "kuficha masiha yake binafsi" fahamu fika kuwa huyo binadamu anayo mapungufu makubwa sana "ki-uongozi"...!


Labda niulize kuwa unapo sema binafsi una maana gani? Kuna maswali binafsi... 'unapenda kula nini', 'siku gani huwezi sahau katika maisha yako?' 'unapenda maisha ya namna gani?' na the like...

Nimetoa hiyo tahadhari sababu watu hawachelewi kuleta maswali kama 'umewahi lala na wanawake wangapi?', 'girlfriend wako ni nani?' 'unafanya mapenzi mara ngapi kwa mwezi?' 'umewahi lala na AshaDii?'

Hivi umenipata maana yangu?

Naamini kabisa kuwa maisha ya Zitto binafsi ni open book, wengi wanamfahamu kwa mbali ama kwa kutokea anako tokea. Sasa kwa mtindo na maswali hayo sioni kuwa tukipata majibu yake kama lina faida yoyote kwa jamii.. Labda kama nakosea; but hivo ndio naamini.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom