Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,798
- 12,240
EWURA- Energy and Water Utilities Regulatory Authority na kwa kiswahili ni Mamlaka ya uthibiti ya Nishati na Maji kila malipo ya huduma hizo kutoka kwa watumiaji wote inakusanya 1% kama tozo. Hizi ni fedha nyingi sana na hasa ukizingatia uwingi wa watumiaji wa umeme, gesi na maji.
Aidha EWURA ni miongoni mwa taasisi chache za umma ambazo zinalipa mishahara mikubwa kwa watumishi wake. Ni vizuri kulipa mishahara mizuri kwa watumishi lakini pia ni vema mishahara mikubwa iendane na huduma na uwekezaji katika maendeleo ya nchi ili kupunguza makali ya maisha magumu ya wananchi.
Binafsi sifahamu mradi wo wote wa maendeleo unaotekelezwa na EWURA. Ningependa nifahamishwe je fedha zote za tozo zinazokusanywa ni kwa ajili ya mishahara, mafunzo na posho za safari tu? Nakumbuka enzi za Magufuli EWURA ni miongoni mwa taasisi za umma zilizolazimishwa kutoa gawio kwa serikali, je mpaka leo gawio linatolewa?
Isije ikawa EWURA ni tobo la kuvujisha fedha za umma!
Aidha EWURA ni miongoni mwa taasisi chache za umma ambazo zinalipa mishahara mikubwa kwa watumishi wake. Ni vizuri kulipa mishahara mizuri kwa watumishi lakini pia ni vema mishahara mikubwa iendane na huduma na uwekezaji katika maendeleo ya nchi ili kupunguza makali ya maisha magumu ya wananchi.
Binafsi sifahamu mradi wo wote wa maendeleo unaotekelezwa na EWURA. Ningependa nifahamishwe je fedha zote za tozo zinazokusanywa ni kwa ajili ya mishahara, mafunzo na posho za safari tu? Nakumbuka enzi za Magufuli EWURA ni miongoni mwa taasisi za umma zilizolazimishwa kutoa gawio kwa serikali, je mpaka leo gawio linatolewa?
Isije ikawa EWURA ni tobo la kuvujisha fedha za umma!