Unachosema ni sawa kabisa, Italy hata wenyewe sidhani kama walitegemea wangefika semi finals na kesho wanaweza kufanya maajabu mengine kwa kuwafunga Wajerumani maana sasa wameshapata confidence na kesho watajituma sana uwanjani.
BAK mi napingana na wewe na ntapingana na ww mpaka mwisho wa Dahari...
Mwaka wowote wa mashindano yoyote makubwa ya Soka ni lazima Italy ipewe nafasi kubwa kuingia nusu fainali, fainali au kuchukua kombe na ndo maana miaka ambayo italy wanaboronga na kutolewa mapema basi hata bet za kamali zinapungua wachezaji na kupungua ladha pia.
Italy mwaka 94 imecheza fainali ya Dunia, mwaka 98 imetolewa robo kwa penati na France hii ni ktk world cup, euro 2000 anafungwa fainali na france golden goal, world cup 2002 wanaboronga na kutolewa na Korea ktk raundi ya pili, euro 2004 wanatolewa na scandinavian countrys, 2006 wanabeba kombe la dunia kwa mara ya 4, 2008 wanatolewa nusu fainali na spain kwa penati, 2010 south africa wanatolewa raundi ya kwanza...
Ninachopingana na wewe ni kauli yako ya kusema Italy akimfunga mjerumani itakuwa bahati...
Nenda katafute kati ya timu hizo mbili ni nani kaburuzwa Mara nyingi zaidi na nani akishinda kesho basi wachezaji wake watavua bukta na kukimbia uwanja mzima?
Pia kauli yako ya kusema eti Buluda mpaka kufika hapa atakuwa kajenga confidence pia napingana na wewe...
Nimekupa orodha ya mashindano na hatua Italy walizofika so kwa kuingia nusu fainali hii sidhani kama ni ajabu kwa wachezaji kama Buffon, chielini, pirlo, de rossi, di natale na casano.
All in all kwa taarifa yako hawa Spain wameibuka mwaka 2008, nyuma ya hapo walikuwa kama Saudia arabia tu.
So unapotaka kuzungumza soka la Ulaya na Dunia basi kwa unyenyekevu unatakiwa uwataje Italy...
Forza Italia