Leo
08/06/2012 ndio mashindano ya kombe la Ulaya mwaka 2012 yanaanza nchini Poland na Ukraine:
Historia fupi:
Mashindano haya yalianza mnamo 1960 kutokana na wazo la Rais wa chama cha soka cha Ufaransa wakati huo
Bw. Henri Delaunay alilolitoa mnamo 1927. Mwanzoni mashindano yakijulikana kama
UEFA European Nations Cup ambapo yalishirikisha mataifa manne tu. Jina la sasa ambalo ni
UEFA European Football Championship ilianza kutumika mwaka 1968.
Itakumbukwa kuwa bingwa wa kwanza alikua ni
USSR na mashindano hayo yakifanyika nchini Ufaransa.
Tokea mashindano yaanzishwe ni nchi 9 tu ndio zimefanikiwa kulibeba kombe na mpaka sasa bingwa mtetezi ni
Uhispania.
Ujerumani wamebeba kombe hili mara 3(Mara mbili wakijulikana kama
Ujerumani Magharibi),
Ufaransa na
Uhispania wamefanikiwa kulibeba mara 3.
Ufuatao ni mtiririko wa mabingwa tokea kombe lilivyoanzishwa hata sasa.
[TABLE="class: outer_border, width: 500, align: left"]
[TR]
[TD]
NCHI
[/TD]
[TD]
MWAKA
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1960[/TD]
[TD]USSR[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1964[/TD]
[TD]Uhispania[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1968[/TD]
[TD]Italia[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1972[/TD]
[TD]Ujerumani Magharibi[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1976[/TD]
[TD]Czechoslovakia[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1980[/TD]
[TD]Ujerumani Magharibi[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1984[/TD]
[TD]Ufaransa[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1988[/TD]
[TD]Uholanzi[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1992[/TD]
[TD]Denmark[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1996[/TD]
[TD]Ujerumani[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2000[/TD]
[TD]Ufaransa[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2004[/TD]
[TD]Ugiriki[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2008[/TD]
[TD]Uhispania[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Nani ataibuka bingwa wa Euro 2012?
Ikumbukwe mpaka sasa hakuna nchi ambayo imeshawahi kutetea ubingwa.
Tuungane sote wapenzi wa soka kufuatilia mtanange huu.
Mechi za Leo: Live Score
Uholanzi 0 (FT) 1 Denmark
Ujerumani 1 (FT) 0 Ureno