Mbunge wa CCM
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 475
- 22
wapendwa, mi sikukuu hii ya krismass na mwaka mpya nasherehekea pamoja na rafiki yang mmoja mchina. pamoja na mambo mengine huwa ananifundisha kidogokidogo kuongea kichina, sasa juzi tukiwa katikati ya hekaheka za sikukuu, akanifundisha kuwa mapumziko yaani rest kwa kichuna huitwa "xiuxi" ukimsikia anavyotamka, ni sawa na kutamka "shushi" kwa kiswahili. mfano kusema kesho sitaenda kazini, napumzika kwa kichina unasema: "mingtian wo bu qu shang ban wo xiuxi" sasa hili likanirudisha nyuma kidogo enzi nasoma shule ya sekondari.
wakati nikiwa sekondari ya awali katika shule siyo ya bweni, nilikuwa naishi na kaka yangu aliyekuwa askari na tuliishi katika nyumba za askari maarufu kama laini au laini polisi. kama mjuavyo moja ya majukumu ya kila siku ya askari ni ulinzi. sasa kulikuwa na msemo pale laini miongoni mwa askari na wanajamii wengine wa laini kuwa siku ambazo askari hakwenda lindoni, yaani anapumzika, tulisema kuwa "anakula shushi" mfano utasikia"mimi niko shushi hadi jumatatu" akiwa na maana kuwa haende kazini (anapumzika) hadi jumatatu.
sasa waungwana na wakereketwa wote wa lugha yetu adhimu, je nini asili ya hili neno shushi. na je lina uhusiano gani (kama upo) na neno la kichina "xiuxi" linalotamkwa "shushi"?.
ufafanuzi tafadhari
wakati nikiwa sekondari ya awali katika shule siyo ya bweni, nilikuwa naishi na kaka yangu aliyekuwa askari na tuliishi katika nyumba za askari maarufu kama laini au laini polisi. kama mjuavyo moja ya majukumu ya kila siku ya askari ni ulinzi. sasa kulikuwa na msemo pale laini miongoni mwa askari na wanajamii wengine wa laini kuwa siku ambazo askari hakwenda lindoni, yaani anapumzika, tulisema kuwa "anakula shushi" mfano utasikia"mimi niko shushi hadi jumatatu" akiwa na maana kuwa haende kazini (anapumzika) hadi jumatatu.
sasa waungwana na wakereketwa wote wa lugha yetu adhimu, je nini asili ya hili neno shushi. na je lina uhusiano gani (kama upo) na neno la kichina "xiuxi" linalotamkwa "shushi"?.
ufafanuzi tafadhari