ESCROW sio siri tena, mambo yote hadharani

ESCROW sio siri tena, mambo yote hadharani

Hakuna Scandal imeongelewa na kutingisha serikali kama Escorow ,cha ajabu hakuna kilichofanyika ,wacha niendelee kuona haya ni maneno tu mpaka nitakapo aminishwa vinginevyo
 
" If you can't beat them,Join them" Maisha ndiyo haya haya,hakuna mengine kwa kizazi hiki isipokuwa kizazi kifuatacho ambacho pia hakina mwelekeo.
 
Hii game napenda sana ichezwe, kama ileeeee iliyowatoa kwa kadi nyekundu wachezaji uwanjani khaaa....!!

Hapa mashabiki wanaruhusiwa kulipigia kelele, na wale team upinzani ndiyo zaidi.....


Ule wimbo waliokuwa wanaimba kuwa team *** mbele kwa mbeleeee, then wanasema wataisoma # sijui ,walikuwa wanawaimbia team pinzani, na baadhi ya mashabiki wa team pinzani waligeuka...

Sasa ni mda wa washabiki wa team pinzani na wachezaji pinzani kuliimbia hili kwa mara ya pili, tena kwa nguvu zote, ili kulipiza kisasi, sheria ya mwamuzi kwa miezi mitano kuwazuia wasiimbe, wala wasipige kelele zozote mpaka msimu mwingine wa league....

eheee....kuna zile team zilizoungana team ile yenye rangi nyekundu na nyeupe, ile ya rangi ya zambarau yenye stricker anayetaka mwamuzi aamue hili swala, kwani si tu linateza team bali washabiki wotee wa team mbili...huu ndo mda wa kulipigia keleeeeeeeeeee................

piga keleeeeeeeeeeee..................miezi sita inatosha kuwa kifungoni yaani kutopiga kelele, wala kumkosoa mwamuzi sasa mda wenu umefika wa kupiga keleeeeeeeee........


***WENYE IQ KUBWA NA WALE AMBAO HATA SHULENI HAWAKUWA WAVIVU KUSOMA VITABU NDIYO WATASOMA NA KUELEWA KISHA WATACOMMENT NA KU-LIKE.


Pigieeeeeeni keleleeeeeeeeeeeeee
 
As long as Baba wa Ikulu alihusika katika wizi huo Ukweli hautakuja kuwekwa wazi hata siku moja na mbaya zaidi katiba yetu inawalinda hata akitoka madarakani.ngoja tuisome namba
 
mpigania ufisadi alizima lugumi kama anazima mshumaa ataweza escrow!
utasikia kuna majitu wanamsifu jamaa eti anapingana na ufisadi huwa nawashangaa
 
najiandaa kushika uraisi baada ya miaka 20 ijayo kazi nitakayoifanya ni kuandika katiba ambayo rais aweze kushitakiwa n a kufungwa akitoka madarakani
 
Mh Magufuli atawatumbua Sana watumishi wazembe kwa unyonge wao,atawafukuza na kuwa funga Sana watumishi hewa kwa unyonge wao na atawasurubisha Sana wanasiasa wa upinzani kwa Sababu ya unyonge wao lakini hapa kwenye ESCROW ndiyo break yake.

Hata uwe mtakatifu vipi bila kuikataa CCM na kazi zake zote ni lazima ugeuke kuwa mjusi,hata uwe mchapa kazi vipi bila kuikata CCM na kazi zake zote lazima uwe legelege,hata Kama uwe mbishi na mjuaji Sana bila kuikata CCM na kazi zake zote lazima ubadilike na kuwa mtu wa ndiyo mzee na hata kama uwe Moto Sana kiutendaji bila kuikataa CCM na kazi zake zote lazima urudi ukiwa baridi Kama kifaranga cha kuku kilichokosa Joto la mama yake.
Watumishi Ndio Punching Bag ya Rais!
 
nakubaliana nawe,huyu mzee ni facilitater,au analobby kwenye makorido ya ofisi za serikali,haya mambo ya kufanya lobbying yapo hata washington na dunia nzima kwa ujumla,na pesa huwa inatumika kulobby mawaziri,masenetor ili fulani apate kandarasi etc,sema huku kwetu inaweza kuitwa rushwa na ufisadi
Wenzetu chochote wanachofanya wanahahakisha kina benefit kwa wananchi kwanza. Wana sign contract ambayo itawafaidisha wananchi lakini huku kwetu ni tofauti, maslahi yao mbele wananchi baadae!
 
Nina mashaka mtoa mada umetumwa kumtetea mtu ila kaa tu kwa serikali hii kila kitu kitaeleweka tu.
 
Hata Mimi ningekua raisi wa Tanzania hili jambo nisingeligusa wala suala la katiba mpya
 
mwinyi hakuleta IPTL mkuu,unajua kipindi kile mwaka 1995 yalikuwepo maongezi kati ya nchi zinazoendelea na zile nchi za tiger economy kushirikiana kiuchumi ili kuepukana na unyonyaji wa nchi za magharibi,enzi hizo kiongozi wa malasysia ndo alikuwa kama rule model ya kuitoa malay katika umasikini na kuwa nchi ya viwanda,mojawapo ya zao la maongezi hayo mwaka 1996 mwinyi akiwa tayari kashaachachia madaraka ndo kina ruge akaingia ubia na kampuni la malaysia la mechmar,hili kampuni linatengea boiler na pia power plant,wakaungana na Ruge na kuunda kampuni iliyoitwa IPTL,
KAMPUNI YA NJE ILI IWEKEZE ILIKUWA LAZIMA ISHIRIKIANE NA MZAWA,
ndo huyo Ruge akatoa kiwanja,kama mchango wake,mechmar wakachukua mkopo bank za malasia na kununua mitambo 10 ya kuzalisha umeme,mkopo ulikuwa dola milioni 100,
wakaleta mitambo na kuisimika katika plot ya Ruge,
hadi inafika mwaka 1998 ,IPTL haijaanza uzalishaji na mwinyi hakuwepo.

Sijasema waziri Tibaijuka ndo alimpa kiwanja Ruge,kwani kipindi mitambo inajengwa tibaijuka alikuwa bado yuko UN


Sasa mkuu huoni kuwa unajivuruga mwenyewe, hivi mtu aliyepagawa na Bil 75 alipoziona alipata wapi hiyo connection ili awe partiner wa kampuni kubwa ya nje kama Mechmar au ndio mambo kama ya mmiliki wa LUGUMI, nilisoma mahali sijui alikuwa fundi viatu ila sina uhakika
 
Watu wanaotakiwa kukamatwa haraka ni singasinga,jaji utamwa, mwanasheria singasinga, katibu wa wizara ya nishati na madini wakti ule na wakuu wa board ya Tanesco wakati ule, tukiwakamata hawa watasema tu walipata amri kutoka kwa nani, hawa ni watu amabo walitumika vizuri sana kufanikisha huu wizi. Mtu kama prof ndulu kwa kweli tutakuwa tunamuonea, maana yeye alijua huu mchezo mapema ndo maana aliomba kinga kutoka kwa wahusika kabla ya kuruhusu pesa itoke, hivyo alijua kabisa fika kuwa hii pesa tunampatia mtu ambae hauhusiki ( PAP) lakini nahisi amri kutoka juu ndo zilitawala. Mimi nashangaa kwa nini tunashindwa kuchukua hatua haraka kwa swala kama hili, tunapoteza bil 300+ tunaona ni swala dogo?.
 
Sasa mkuu huoni kuwa unajivuruga mwenyewe, hivi mtu aliyepagawa na Bil 75 alipoziona alipata wapi hiyo connection ili awe partiner wa kampuni kubwa ya nje kama Mechmar au ndio mambo kama ya mmiliki wa LUGUMI, nilisoma mahali sijui alikuwa fundi viatu ila sina uhakika
nauli kutoka hapa mpaka malaysia kipindi kile haikuwa kubwa sana,na yule jamaa kasoma soma kidogo kwahiyo kufanya connection haikumpa tabu sana
 
Yeye ndiye mtengenezaji pekee wa bia ya Heineken nchini,bila shaka unajua jinsi biashara ya vileo inavyolipa
yule mzee ni dalali mzuri sana kumbe hata ishu ya bandari ya bagamoyo yumo?,
ila si wanajenga wachina na oman,ila yeye anajua kuupepeta mdomo,nadhani ndo coordinator ya shughuli nzima.
Hebu taja vitega uchumi vikubwa anavyomilki huyu babu,iwe hapa Tanzania ama south africa,ukiachia VIP[/QUOTl
 
Back
Top Bottom