Escrow kumuumbua Rais Kikwete

Escrow kumuumbua Rais Kikwete

Wakuu kama washauri wa Mtukufu Mhs Dr. Prof Kikwete wamesoma basi hawajaelimika!
Kama washauri wa Mtukufu Mhs Dr. Prof Kikwete ktk swala zima hili wamesoma basi itabidi tuulizie ni shule zipi na wapi wamepata hii elimu!

Kama washauri wa Mtukufu Mhs Dr. Prof Kikwete wamesoma na kufanya kazi na kuwa na uzoefu ktk shughuli zao, basi inabidi tujue huo uzoefu wameupata kwa kufanya shughuli zipi nk!


Sasa basi nirudi kwenye issue hii:

Kuna kitu kinaitwa ''KUJIFUNGA MAGOLI KATIKA MCHEZO WA MIPIRA'' Kwa hiyo kama hao washauri wa Mtukufu Mhs Dr. Prof Kikwete watamshauri kumpeleka huyu mama Anna TIBAIJUKA mahakamani basi kutuakuwa na sababu mbili, nazo ni kama ifuatavyo:


1. Labda wana njama au siri ya kumuacha Mtukufu Mhs Dr. Prof Kikwete kwenye MATAA ili mwisho wake IWE ni kichekesho ktk historia ya marais waliopita.
2. LABDA maskini elimu yao inaongozwa na uroho wa sifa pamoja na matumbo yao ambayo hayashibI badara ya KUONGOZWA NA taaluma ZAO.


MWISHO: Hivi nyie wakina Spika and company mnaofikiri kuchafuliwa kwa mama Tibaijuka kutwasaidia labda kupitisha majina yenu ili kugombea uraisi itawasaidia? Inabidi kufahamu kuwa nchi ilipofikia mtu kama Spika huwezi kuiongoza Tanzania ya leo. Hiyo sahau, na ndiyo maana hata Mtukufu Mhs Dr. Prof Kikwete unaona yanayompata masikini!

Ikumbukwe kumchukia mama Anna haitakusaidia kamwe. She is an international figure already, hivyo unafiki peleka huko kwenu mikoani lkn muacheni mama wa watu kwani kama amekosa ni makosa ambayo hayawezi kulinganishwa na yanafaonywa na hao ndugu zenu. Kumbuka hii issue mwisho wake labda inaweza kuwa mwisho wa yote ambayo Mzee wetu Nyerere aliyaeleza pale Dodoma wakati aliitwa ili awasaidie kuwaeleza ni candidate wa namna gani NEC iwachagulie wana CCM.

.
 
Inavyoelekea kuna mkakati ambao unaendelea ili Tibaijuka aonekane hana hatia. Mbona hawa akina Kubenea hawawataji akina Ngeleja, Chenge na wengine waliokula fedha hizo? Kubenea ni mpuuzi tena amepindukia

Upo kwa ajili ya kumshambulia kubenea au kukanusha ripoti hii? au wewe una maoni gani juu ya hili sakata ujue mda mwingine majibu yenu yanawafanya mdharauliwe
 
Wakati wananchi wengi wakiumizwa vichwa juu ya wizi huu wa kutisha ndani ya karne hii ya kila nyenzo za kufanya kazi kwa ufanisi wana CCM wanaumia vichwa kwa kukosa mgao wa pesa za umma. Nawambieni mwaka huu hamponi na mpigwe tu eeee maana tumekyoka sisi sasa mjifanye nyie ndo mna shida zaidi ,mnaijua pesa zaidi ama mna haki zaidi ya wengine mwaka huu mtakula kijani chenu nyaaambafu
 
Yaani kama kuna mtu anaonewa ni huyu mama Ana tibaijuka wezi wapo wanajulikana
sasa iweje huyu mama wamfanye mbuzi wa kafara? kumpeleka huyu mama mahakamani
hapo serikari itaonyesha ni namna gani ilivyo dhaifu kiutendaji

singa singa yupo Luge yupo na wengine waliochukua zile za stanbic wapo mbona
hawaongelewi wala kutajwa? na huyu Raisi Kesha tufanya mafala mara aseme pesa siyo
za umma sasa ni nani mlalamikaji kwa prof Tibaijuka? tuache kuonana mabwege

watajwe waliobeba fedha pale stanibic kwenye malumbesa siyo hicho kiasi kidogo
alichochotewa huyo mama pls vinginevyo tutaonana wabaya.

chimbondu sio katufanya mafala sisi ni mafala kweli mambo mangapi yametokea ya ajabu na mabaya tuko kimyaa tunabaki kulalamika nakupiga mikwara nyuma ya keybody na keypad tu.Tunawaachia badhi ya wanasiasa na waandishi nguli hatutaki kuwaunga mkono kana kwamba wao ndio watz wanaoumia pekee.

ya madakatari yaliishaje,mwangosi kesi yake ikoje,ulimboka walimsema wee mara kachukua pesa kahongwa sijuw nn mwisho wa siku akamtaja kupitia wakili wake aliehusika kumtesa wananchi tukaa kimya ingawa kunawatu walijiapiza humuhumu kumpigania kama angemtaja mtesi wake maisho wa siku kimyaaaaa.

Nawashaangaaa sana baadhi ya wanasiasa wanatupigania watz tusiotaka kupiganiwa .Inaniuma na kunikera sana.Watz tunaamin baadhi ya wanasiasa na wanaharakati pekee yao watatatua matatizo tulio nayo.


Ndio maana kila mtu anautaka urais kwa kuwa ni rahis kuwatawala watz bara kuliko kuitawala tz visiwani.
 
Last edited by a moderator:
Na ndo maana serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye mradi wa gesi asilia ili tujitegemee kiuchumi

Serikali hiyohiyo imewekeza sekta ya madi kwa lugha hiyohiyo ya "ili tujitegemee"!Je!Tumejitegemea?Ni Akili km zako ndizo zilizolifikisha Taifa katika Ufisadi na kila aina ya Ubaya utokanao na Serikali!Labda una mategemeo gani mapya kutoka kwenye Gas tofauti na hali ilivyo kwenye Madini?
 
Rushwa kwa kazi ipi? Katika sakata zima la Escrow wizara ya aridhi haikua na uhusiano wowote na sakata hilo wizara zilizohusika zinajulikana. Ukienda mahakamani na ushahidi huu wa kusema amepokea rushwa utagaragazwa na utaishia kulipa dhamana. Huingii akilini mtu ambae hana influence katika maamuzi na wala hakuna popote alipotoa ushauri na ripoti zote za Takukuru na CAG hakuna popote zinapomtaja zaidi ya kuonekana kwenye orodha ya mgao useme kua amepokea rushwa.

JK alisema huwezi kuamka tu asubuhi ukakuta fedha zimejaa kwenye akaunti yako. Zimetoka wapi? Zimeshuka kutoka mbinguni? Na JK aliyasema haya baada ya kuzungumza na Bodi ya Shule anayoingoza (anayoimiliki?) Tibaijuka, akiwemo Mzee Rupia. Mazingira ya rushwa ni dhahiri, na kukiukwa kwa maadili ya viongozi ni dhahiri. Sasa, anayeweza kuamua kama huyu mama ana hatia au la ni mahakama. Si wewe, wala mimi. Alipewa rushwa kwa kazi ipi, huyu mama ataileza mahakama wakati ukifika. Ripoti ya CAG haijamtaja popote haina maana kuwa Mama Tibaijuka hakupokea rushwa. Na wala si kazi ya CAG kuchunguza mashauri ya rushwa. Ripoti ya TAKUKURU unayosema haimtaji huyu mama kupokea rushwa umeiona? Unaweza kuiweka hapa?

Na kumbuka, anayetuhumiwa hapa ni Mama Anna Tibaijuka. Si wewe. Si Wizara ya Ardhi. Aliyepokea fedha kutoka kwa James Rugemalira ni Anna Tibaijuka. Si wewe. Si Wizara ya Ardhi. Kama ni kosa, limefanywa na mtu aitwaye Anna Tibaijuka. Kosa halikufanywa na Wizara ya Ardhi au Waziri wa Ardhi. Na kama ni kushtakiwa, atashtakiwa Anna Tibaijuka. Hatoshtakiwa Waziri wa Ardhi au Wizara ya Ardhi.

Ni nini kinakufanya uhusishe maovu ya huyu mama na Wizara ya Ardhi? Wizara ya Ardhi ni taasisi. Anna Tibaijuka ni individual.

Na kosa hapa ni rushwa, bila kujali hizo pesa zilitoka kwenye akaunti ya escrow au la. Je kama pesa hazikutoka kwenye akaunti ya escrow, ina maana tuhuma za rushwa zinalomkabili zitafutika? Je, mimi nikutuhumiwa kukupa rushwa wewe, tuhuma hizo zitafutika ikigundulika kuwa pesa nilizokuhonga nilizipata kwa njia halali?
 
mliompigia kura jk jipimeni akili zenu...
Umenena vyema.

One thing: Hivi sheria ya rushwa inasemaje? Hii nchi inaendeshwa na wendawazimu.
Mtoa rushwa haguswi, mnaedai kapewa rushwa mnamshitaki, hii ni akili ya wapi hii?
 
JK alisema huwezi kuamka tu asubuhi ukakuta fedha zimejaa kwenye akaunti yako. Zimetoka wapi? Zimeshuka kutoka mbinguni? Na JK aliyasema haya baada ya kuzungumza na Bodi ya Shule anayoingoza (anayoimiliki?) Tibaijuka, akiwemo Mzee Rupia. Mazingira ya rushwa ni dhahiri, na kukiukwa kwa maadili ya viongozi ni dhahiri. Sasa, anayeweza kuamua kama huyu mama ana hatia au la ni mahakama. Si wewe, wala mimi. Alipewa rushwa kwa kazi ipi, huyu mama ataileza mahakama wakati ukifika. Ripoti ya CAG haijamtaja popote haina maana kuwa Mama Tibaijuka hakupokea rushwa. Na wala si kazi ya CAG kuchunguza mashauri ya rushwa. Ripoti ya TAKUKURU unayosema haimtaji huyu mama kupokea rushwa umeiona? Unaweza kuiweka hapa?

Na kumbuka, anayetuhumiwa hapa ni Mama Anna Tibaijuka. Si wewe. Si Wizara ya Ardhi. Aliyepokea fedha kutoka kwa James Rugemalira ni Anna Tibaijuka. Si wewe. Si Wizara ya Ardhi. Kama ni kosa, limefanywa na mtu aitwaye Anna Tibaijuka. Kosa halikufanywa na Wizara ya Ardhi au Waziri wa Ardhi. Na kama ni kushtakiwa, atashtakiwa Anna Tibaijuka. Hatoshtakiwa Waziri wa Ardhi au Wizara ya Ardhi.

Ni nini kinakufanya uhusishe maovu ya huyu mama na Wizara ya Ardhi? Wizara ya Ardhi ni taasisi. Anna Tibaijuka ni individual.



Na kosa hapa ni rushwa, bila kujali hizo pesa zilitoka kwenye akaunti ya escrow au la. Je kama pesa hazikutoka kwenye akaunti ya escrow, ina maana tuhuma za rushwa zinalomkabili zitafutika? Je, mimi nikutuhumiwa kukupa rushwa wewe, tuhuma hizo zitafutika ikigundulika kuwa pesa nilizokuhonga nilizipata kwa njia halali?

Mimi nilichosema ni kua kama haya madudu yangefanyika kwenye taasisi iliyo chini ya wizara ya aridhi nisingemtoa moja kwa moja katika hili. Kinacholeta wasi wasi ni waziri mwenye dhamana na nishati kubaki msafi kwenye escrow na waziri wa aridhi akawa mchafu kwenye escrow hiyo hiyo labda kama Tanesco watakua chini ya wizara ya aridhi. Watanzania hatuwezi kuwa wajinga kiasi hicho cha kuangalia usafi wa mtu kwa kuangalia uchafu wa mwingine.
 
JK alisema huwezi kuamka tu asubuhi ukakuta fedha zimejaa kwenye akaunti yako. Zimetoka wapi? Zimeshuka kutoka mbinguni? Na JK aliyasema haya baada ya kuzungumza na Bodi ya Shule anayoingoza (anayoimiliki?) Tibaijuka, akiwemo Mzee Rupia. Mazingira ya rushwa ni dhahiri, na kukiukwa kwa maadili ya viongozi ni dhahiri. Sasa, anayeweza kuamua kama huyu mama ana hatia au la ni mahakama. Si wewe, wala mimi. Alipewa rushwa kwa kazi ipi, huyu mama ataileza mahakama wakati ukifika. Ripoti ya CAG haijamtaja popote haina maana kuwa Mama Tibaijuka hakupokea rushwa. Na wala si kazi ya CAG kuchunguza mashauri ya rushwa. Ripoti ya TAKUKURU unayosema haimtaji huyu mama kupokea rushwa umeiona? Unaweza kuiweka hapa?

Na kumbuka, anayetuhumiwa hapa ni Mama Anna Tibaijuka. Si wewe. Si Wizara ya Ardhi. Aliyepokea fedha kutoka kwa James Rugemalira ni Anna Tibaijuka. Si wewe. Si Wizara ya Ardhi. Kama ni kosa, limefanywa na mtu aitwaye Anna Tibaijuka. Kosa halikufanywa na Wizara ya Ardhi au Waziri wa Ardhi. Na kama ni kushtakiwa, atashtakiwa Anna Tibaijuka. Hatoshtakiwa Waziri wa Ardhi au Wizara ya Ardhi.

Ni nini kinakufanya uhusishe maovu ya huyu mama na Wizara ya Ardhi? Wizara ya Ardhi ni taasisi. Anna Tibaijuka ni individual.

Na kosa hapa ni rushwa, bila kujali hizo pesa zilitoka kwenye akaunti ya escrow au la. Je kama pesa hazikutoka kwenye akaunti ya escrow, ina maana tuhuma za rushwa zinalomkabili zitafutika? Je, mimi nikutuhumiwa kukupa rushwa wewe, tuhuma hizo zitafutika ikigundulika kuwa pesa nilizokuhonga nilizipata kwa njia halali?
Mkuu,
Aliyempa rushwa huyu mama ni nani? nae tunataka kuona akihojiwa na kufikishwa mahakamani.
Haki bin Haki.........blah blah za CCM na serikali yake hazitaifikisha nchi hii popote.

Aliyetoa, na aliyepokea wote wanamakosa..........Sasa Rugemalira tunataka kumuona kizimbani pia.

Thats one, pili, fedha zilizotolewa cash Stanbic bank zilikwenda wapi, nani alipewa mgao? inamaana Ruge ndiye aliyegawa fedha peke yake? Singasinga aliyechota 70% ya fedha zote alizipeleka nje bila kumgawia swahiba wake?
 
so agenda ya kutafutia kura ni kupakazia watu wizi?
nayo itagonga mwamba vilevile

Acha mapenz ya kijinga......Nchi hii ni ya wa Tanzania sio ya CCM wala ya CHADEMA Kikwete na wenzake ni wezi.......serikali yake tumeshuhudia kashfa ngapi za wizi ambazo zinzfanywa na wanaoitwa wasaidiz wake?,hakwepi haya huo ndo ukweli......mapenz ya kijinga hadi kupotosha ukweli hauna nafas dunia ya sasa,hiki ni kipindi cha kujua na kuona nyeupe hii na nyeusi ni hii hamna kuzuga....
 
Mimi nilichosema ni kua kama haya madudu yangefanyika kwenye taasisi iliyo chini ya wizara ya aridhi nisingemtoa moja kwa moja katika hili. Kinacholeta wasi wasi ni waziri mwenye dhamana na nishati kubaki msafi kwenye escrow na waziri wa aridhi akawa mchafu kwenye escrow hiyo hiyo labda kama Tanesco watakua chini ya wizara ya aridhi. Watanzania hatuwezi kuwa wajinga kiasi hicho cha kuangalia usafi wa mtu kwa kuangalia uchafu wa mwingine.

With or without escrow, huyu mama alipokea rushwa kutoka kwa James Rugemalira. Hili ni kosa bila kujali kuwa Waziri mwenye dhamana na nishati amechukuliwa hatua au la. Huwezi kupokea rushwa halafu utetezi wako ukawa mbona fulani naye alipokea rushwa lakini hajachukuliwa hatua.

Waziri wa Nishati ambaye ni Prof. Muhongo, kama ilivyo kwenye maazimio ya Bunge, anahusika na utoaji wa fedha kwenye akaunti ya escrow kwa njia za kutatanisha. Alishiriki pia kuficha maovu around utoaji wa fedha hizo. Sasa,naamini na yeye anapaswa kuwajibika na anastahili kuchunguzwa na kuchukuliwa hatua stahili. Hata asipochukuliwa hatua, haina maana kuwa Tibaijuka hakupokea rushwa.

Unachopaswa kuelewa ni kuwa kutoa na kupokea rushwa ni kosa, bila kujali kama pesa zilizotumika ni za escrow au la. Again, anayetuhumiwa ni Anna Tibaijuka. Si Waziri wa Ardhi kwa nafasi yake. Hizi ni tuhuma dhidi ya mtu na si taasisi inayoitwa Wizara ya Ardhi.
 
Unajua wahaya ni wasomi wastaarabu,pia wakwele ni kama ka kijiji kachovu huko huayani,hapo ni sawa na mende kuangusha kabati.
Lakini kwa kashifa ya huyu mama na maneno yake ya nyodo wahaya wamemwacha azame dimbwini.

Mmh.! Tunazugwa sie..
 
Kwani anayewapeleka Mahakamani ni JK? Na je wanaopelekwa mahakamani ni wanufaika wote wa escrow au wale maafisa wa serikali walioenda kinyume na maadili ya kazi zao?
kwani tiba katolewa kwa nini.? Suala la escrow au kwenda kinyume na maadili ya kazi.?
 
sisi kina gogo la shamba tulishasema kwamba,maadam Kikwete alipuuza mawazo tuliyompa hawezi tena kuepuka kikombe hicho,yeye na familia yake yote,aelewe kwamba mwisho wa maisha yake hayato kuwa tofauti na Sadam au Gadafi karata yake moja iliyobaki ni
1. kuamuru kutoka kinywani kwake kwamba wale wote waliotoa na waliopewa fedha za Escrow wazirudishe na baadae mahakamani
2.Nyumba zote za uma zirudishe
3.shule bure
..za alinacha hizo....
 
Alijiweka mbali nao vipi wakati alifanya nao kazi. Shida yako ni kuwa unaugua ugonjwa wa ukabila ambao kwa kitaalamu unafahamika kama ufashisiti kama aliokuwa nao Hitler na Mussolini. Wahi Milembe upate tiba haraka kwani wewe ni Interahamwe!

Na wakwere je.?!
 
Back
Top Bottom