Escrow kumuumbua Rais Kikwete

Escrow kumuumbua Rais Kikwete

Uongo mtupu.

Mtamtafuta sana mwana wa mwenzenu hamumpati ng'oo. Mahasidi wakubwa.

Mmemtafuta miaka 9 hamjampata mtampata leo imebaki miezi 9? Mnanchekesha.

Nakuambia kikwete atakamatwa kabla hajavuka viwanja vya Jimukana.
 
Well, hapa unachanganya mambo. Hapa ni kama vile unamtetea Tibaijuka. Ukweli ni kwamba Tibaijuka amekula mlungula na anapaswa kuchukuliwa hatua. Vivyo hivyo, Chenge amekula mlungula na anapaswa kuchukuliwa hatua. Kutokujadiliwa kwa "Chenge huko CC aondoke kwenye CCM"[sic] hakufuti makosa ya Tibaijuka. Unachopaswa kufanya ni kushinikiza kusiwe na double standards na wote waliovunja sheria za nchi wachukuliwe hatua badala ya kutumia kutochukuliwa hatua kwa mkosaji mmoja kufuta au kuhalalisha makosa ya mwingine.

According to Oxford Dictionary, scapegoat means a person who is blamed for something bad that somebody else has done or for some failure. Sasa kwenye hili, Tibaijuka hawezi kuwa scapegoat. Ni kweli alihongwa shillingi 1.6 billion na lazima achukuliwe hatua za kisheria. Matumizi yako ya neno scapegoat hapa yanaonesha kuwa unashangaa kwa nini hawamlindi Tibaijuka kama wanavyomlinda Chenge? Kwa maneno mengine, unataka waendeleze utaratibu wao mchafu wa kulindana. Tusingependa walindane bali kila mtu abebe mzigo wake.



Zungu Pule Nadhani Umeisoma hiyo taarifa vizuri... Na Unajua ya kuwa Prof. Tibaijuka hakuwa kwenye hiyo campaign ya kuidhuru serikali ya nchi yetu kwa hiyo mikataba dhaifu; Ila alipewa pesa kama watu zaidi ya 40 kwenye Account zao, wako wa kila aina... lakini ni kwanini yeye kuchaguliwa kati ya hao 40 ndani ya serikali --- that's when SCAPEGOAT comes...

Yeah... sijasema hana Makosa kupokea hizo pesa kama kiongozi wa serikali bila kujua undani wake ni kuwa UNETHICAL --- na kuwa kiongozi wa serikali tukufu unatakiwa kuwa ETHICAL... kuondolewa Uwaziri ungetosha kabisa na kama watatumia njia za kutaka pesa zirudishwe ni kumuandama the main known culprit or culprits...

As you know...
There may be times when we are powerless to prevent injustice, but there must never be a time when we fail to protest.
 
RAIS Jakaya Mrisho Kikwete, anahaha kujiokoa na kashfa ya ukwapuaji wa mabilioni ya shilingi katika akaunti ya Escrow, ndani ya Benki Kuu (BoT).

Mpango wa sasa, ni kuwakamata baadhi ya waliopewa fedha na James Rugemalira, mmoja wa wamiliki wa IPTL ili kuzima mjadala.

Profesa Anna Tibaijuka, mbunge wa Muleba Kusini (CCM), yumo katika orodha ya wanaotakiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote wiki hii.


Tayari Prof. Tibaijuka amehojiwa zaidi ya mara moja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU), kuhusu Sh. 1.6 bilioni alizopewa na Rugemalira.


Mkakati wa kumfikisha mahakamani Prof. Tibaijuka, unasukwa kwa ustadi mkubwa na waziri mmoja mwandamizi katika serikali ya Rais Kikwete.


“Watanaka Prof. Tibaijuka apelekwe mahakamani kwa hoja kuwa, kwa hadhi aliyonayo kimataifa, sakata zima la Akaunti ya Tegeta Escrow litakuwa limezimwa,” anaeleza mtoa taarifa.


Anasema, “Lakini nataka nikuhakikishie, kitendo hicho kitasababisha tatizo kukua. Rais Kikwete anafahamu fika Harbinder Singh Sethi wa IPTL kuwa alitokea ikulu kabla ya kukwapua mabilioni ya shilingi kutoka akaunti ya Escrow.”


Anasema, “Ni vigumu kwa Rais Jakaya Kikwete kufanikiwa kujitenga na kashfa ya ukwapuaji wa zaidi ya Sh. 321 bilioni zilizochotwa katika akaunti ya Tegeta Escrow.”


Kiasi cha Sh. 321 bilioni zilikwapuliwa kutoka akanti ya Escrow ndani ya Benki Kuu (BoT), kati ya Septemba na Novemba 2013; na Prof. Tibaijuka alipewa Sh. 1.6 bilioni na mmoja wa waliokuwa wabia katika kampuni ya kufua umeme ya IPTL.


Taarifa zinasema, anayejiita na kuitwa na serikali kuwa ni “mmiliki mpya wa IPTL/PAP,” Harbinder Singh Sethi, aliletwa nchini na mmoja wa wanafamilia wa Rais Kikwete.


Taarifa zinasema, wanaoshinikiza Prof. Tibaijuka kufikishwa mahakamani wanajenga hoja mbili. Kwanza, kwamba hatua hiyo italegeza msimamo wa wahisani wa kuinyima misaada Tanzania; na kwamba kelele zote za ndani zitakuwa zimezimwa.


Pili, hatua ya kumfikisha mahakamani waziri huyo wa zamani wa ardhi, kutasaiidia kumkingia kifua waziri wa nishati na madini, Prof. Sospeter Muhongo na kuzima mjadala bungeni.


Rais Kikwete alimfuta kazi Prof. Tibaijuka katika mkutano wa “Wazee wa Dar es Salaam,” tarehe 23 Desemba 2014.


Inaelezwa kuwa singasinga alikutana na rais, ikulu jijini Dar es Salaam; na kutoka hapo alikwenda kukwapua mabilioni ya shilingi BoT hata bila kumfahamisha Rugemalira – mbia mwenzake.


Taarifa zinasema, sasa rais anashinikizwa kumfukuza Prof. Tibaijuka kutoka Kamati Kuu (CC) ya CCM na baadaye kumfikisha mahakamani kwa madai ya wizi na utakatishaji wa fedha.


Kupatikana kwa taarifa kuwa serikali ya Rais Kikwete inapanga njama za wizi kwa kupeleka baadhi ya waliochotewa fedha na Rugemalira, kumekuja wiki tatu baada ya Kikwete kudai kuwa fedha katika akaunti ya Escrow, hazikuwa za umma.


Akihutubia wanaoitwa, “Wazee wa Dar es Salaam,” katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Rais Kikwete alisema, mabilioni ya shilingi katika akaunti ya Escrow yalilipwa kwa PAP baada ya Mahakama Kuu kutoa “amri” tarehe 5 Septemba 2013.”


Akaunti ya Escrow ilifunguliwa ili kusubiri kumalizika kwa mgogoro kati ya Tanesco na IPTL, uliohusu madai ya udanganyifu katika uwekezaji; na hata gharama za kuweka mitambo – Capacity Charge – ambavyo vilifanywa na kampuni hiyo ya kigeni.


Kampuni ya IPTL ni muungano wa kampuni mbili – VIP Engineering and Marketing Limited ya James Rugemalira, iliyokuwa ikimiliki asilimia 30 ya hisa na MECHMAR ya Malaysia iliyokuwa na asilimia 70 za hisa.

uzombi huu utaisha lini??
 
Agenda kuu ktk uchaguzi 2015 nikuwa RAISI JK kutoka CCM kaiba pesa za wananchi, hili lazima liingie vizuri kwenye vichwa vya wananchi na lazima lihubiriwe kila kona na kila pembe ya nchi
 
Tibaijuaka kupelekwa mahakamani siyo tija tayari jk alisema siyo pesa ya umma sasa anapeleka watu mahakamani kwa lipi totally hii ni contradiction ya hali ya juu.
 
Ninavyojua mimi ni kwamba Anna Tibaijuka hakuiba hizo pesa bali alipewa zilizoibiwa. Sina uhakika kama alijua kuwa anapewa pesa zilizoibiwa au la. Swali langu ni hili: Kwa kuwa Tibaijuka alikuwa muwazi na akatwambia huyo aliyempa pesa (zilizoibiwa), kwa nini huyo aliyetoa hizo pesa za wizi asibebeshwe mzigo wa huo wizi? Kujaribu kumfanya Anna aonekane kuwa ndo mwizi ni kumfunya kuwa mbuzi wa kafara tu.
 
Tibaijuaka kupelekwa mahakamani siyo tija tayari jk alisema siyo pesa ya umma sasa anapeleka watu mahakamani kwa lipi totally hii ni contradiction ya hali ya juu.

Wewe umekuwa Jaji mkuu? Mtu amekula rushwa na hilo ni kosa kisheria. Unazungumzia tija gani? Na haki inapatikana mahakamani. Kwanini mnaogopa huyu Mama kufikishwa mahakamani? Kama kweli yeye ni safi kama anavyodai, kwanini anaogopa mahakama?
 
Ninavyojua mimi ni kwamba Anna Tibaijuka hakuiba hizo pesa bali alipewa zilizoibiwa. Sina uhakika kama alijua kuwa anapewa pesa zilizoibiwa au la. Swali langu ni hili: Kwa kuwa Tibaijuka alikuwa muwazi na akatwambia huyo aliyempa pesa (zilizoibiwa), kwa nini huyo aliyetoa hizo pesa za wizi asibebeshwe mzigo wa huo wizi? Kujaribu kumfanya Anna aonekane kuwa ndo mwizi ni kumfunya kuwa mbuzi wa kafara tu.

Unachanganya. Tibaijuka amekula rushwa. Haijalishi kama pesa zimeibiwa au la. That is source ya hela za mtoa rushwa si hoja hapa. Jiulize, mbona hukupewa wewe hizo billion 1.6? Au wewe ulikuwa huhitaji?
 
Wewe umekuwa Jaji mkuu? Mtu amekula rushwa na hilo ni kosa kisheria. Unazungumzia tija gani? Na haki inapatikana mahakamani. Kwanini mnaogopa huyu Mama kufikishwa mahakamani? Kama kweli yeye ni safi kama anavyodai, kwanini anaogopa mahakama?
tunataka wahumiwa Wote kuanzia werema mpaka muhongo
 


Zungu Pule Nadhani Umeisoma hiyo taarifa vizuri... Na Unajua ya kuwa Prof. Tibaijuka hakuwa kwenye hiyo campaign ya kuidhuru serikali ya nchi yetu kwa hiyo mikataba dhaifu; Ila alipewa pesa kama watu zaidi ya 40 kwenye Account zao, wako wa kila aina... lakini ni kwanini yeye kuchaguliwa kati ya hao 40 ndani ya serikali --- that's when SCAPEGOAT comes...

Yeah... sijasema hana Makosa kupokea hizo pesa kama kiongozi wa serikali bila kujua undani wake ni kuwa UNETHICAL --- na kuwa kiongozi wa serikali tukufu unatakiwa kuwa ETHICAL... kuondolewa Uwaziri ungetosha kabisa na kama watatumia njia za kutaka pesa zirudishwe ni kumuandama the main known culprit or culprits...

As you know...
There may be times when we are powerless to prevent injustice, but there must never be a time when we fail to protest.

Tibaijuka alipokea rushwa, bila kujali "undani" wa fedha alizopokea. Watu wanachanganya kitendo cha kupokea rushwa na chanzo cha fedha zilizotumika. Hivi ni vitu viwili tofauti. Je unamaana kuwa kama fedha alizopokea Tibaijuka zisingekuwa zimetoka kwenye akaunti ya escrow, basi ingekuwa ethical kwake kupokea fedha hizo? Au TAKUKURU wasingenyanyua bendera kuashiria kuwa kiongozi kapokea mlungula kinyume cha sheria?
 
Unachanganya. Tibaijuka amekula rushwa. Haijalishi kama pesa zimeibiwa au la. That is source ya hela za mtoa rushwa si hoja hapa. Jiulize, mbona hukupewa wewe hizo billion 1.6? Au wewe ulikuwa huhitaji?

​Kama hiyo ni rushwa, kwa nini mtoa rushwa haguswi badala yake kosa lote anabebeshwa mpokeaji tu?
 
ot Lady;11724321]Kubenea anahangaika sana. Fedha za Reginald Mengi alizolamba kushinikiza Muhongo afukuzwe anaona kuwa zinataka kumtokea puani[/QUOTE]tupe facts
 
​Kama hiyo ni rushwa, kwa nini mtoa rushwa haguswi badala yake kosa lote anabebeshwa mpokeaji tu?

Hayo ndiyo maswali unayopaswa kuuliza. Na si kusema huyu mama hastahili kuchukuliwa hatua za kisheria. Kutokuchukuliwa hatua kwa mtoaji hakufuti makosa ya mpokeaji (They will not be tried jointly.). Makosa ya mtoa rushwa hawezi kubebeshwa mpokeaji. Haliko hivyo. Huyu mama, kama atashtakiwa, atashtakiwa kwa kosa la kupokea rushwa na si kutoa rushwa. Si umefuatilia mashtaka ya wale wengine yanavyosomeka? Kwamba, mnamo tarehe 2 February 2014 majira ya saa nne asubuhi kwenye maeneo ya Benki ya Mkombozi, Mshitakiwa Anna Tibaijuka alipokea rushwa ya Shillingi 1.6 billioni kutoka kwa James Rugemalira kinyume na Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
 
Back
Top Bottom