Well, hapa unachanganya mambo. Hapa ni kama vile unamtetea Tibaijuka. Ukweli ni kwamba Tibaijuka amekula mlungula na anapaswa kuchukuliwa hatua. Vivyo hivyo, Chenge amekula mlungula na anapaswa kuchukuliwa hatua. Kutokujadiliwa kwa "Chenge huko CC aondoke kwenye CCM"[sic] hakufuti makosa ya Tibaijuka. Unachopaswa kufanya ni kushinikiza kusiwe na double standards na wote waliovunja sheria za nchi wachukuliwe hatua badala ya kutumia kutochukuliwa hatua kwa mkosaji mmoja kufuta au kuhalalisha makosa ya mwingine.
According to Oxford Dictionary, scapegoat means a person who is blamed for something bad that somebody else has done or for some failure. Sasa kwenye hili, Tibaijuka hawezi kuwa scapegoat. Ni kweli alihongwa shillingi 1.6 billion na lazima achukuliwe hatua za kisheria. Matumizi yako ya neno scapegoat hapa yanaonesha kuwa unashangaa kwa nini hawamlindi Tibaijuka kama wanavyomlinda Chenge? Kwa maneno mengine, unataka waendeleze utaratibu wao mchafu wa kulindana. Tusingependa walindane bali kila mtu abebe mzigo wake.