Enzymes
JF-Expert Member
- Feb 14, 2013
- 4,332
- 3,020
Sasa hiyo risiti itakusaidia nini kwa mfano
Nilidhani una akili, kumbe umejaza makamasi tu kichwani!!
Sasa hiyo risiti itakusaidia nini kwa mfano
Ni kweli mkuu. Kwenye hili suala la forex tunashangaza. Utadhani tupo enzi zile za barter system. Hata mimi nisiye mchumi naona twapoteza kodi katika eneo hilo...Wadau,
Hata kama ni uwekezaji lazima ufuate sheria za nchi husika, lazima kuwe na win win situation.
Kwa bahati mbaya sivyo hivyo kwa haya mabenki ya nje yanayofurika nchini kila uchao, wanakuja kutuibia na kutuhujumu. Najiuliza, wanapata wapi ujasiri wa kukiuka masharti ya biashara na uwekezaji? Hivi ni kweli Benki Kuu haina mechanism ya kucheki kama haya mabenki yanafuata sheria za nchi.
Wiki tatu zilizopita nilienda Equity Bank pale Golden Jubilee kuchenji dola elfu mbili ili nipate shilingi niweze kufanya malipo mbali mbali ya kiofisi. Nilipofika Equity Bank nilielekezwa nipande ghorofani ambapo nilimpatia teller hizo dola ili anipe shilingi. Ajabu ni kuwa, nilipomwomba risiti akagoma ati hawatoagi risiti! Nikamwambia hicho kitu haiwezekani na hakipo, dada akasema ndivyo ilivyo na akamuuliza jirani yake ili nithibitishe, na mwenzake akanithibitishia! Ndipo nikawaambia wanirudishie dola zangu nikaenda kubadilishia Bureau de Change ambao baada ya kudai risiti walinipa.
Ijulikane kuwa hata hizo Bureau de Change nao ni hivyo hivyo, risiti ni hadi uidai. Wenzetu Uganda hata ukiwa unauza dola ili upate shilingi yao lazima wadai passport na wajaze fomu kadhaa na kukupa risiti yako, yaani huhitaji kuuliza.
Nachotaka kusema ni kuwa hawa Equity Bank wanahujumu uchumi wetu, wanatorosha dola zetu kupeleka kwako na hivyo kusababisha kushuka na kuporomoka kwa shilingi yetu.
Si Equity Bank tu,hapa Tanzania hakuna udhibiti wowote wa exchange ya pesa za Kigeni.Nchi za Wenzetu mfano Rwanda kuna udhibiti mkubwa wa Pesa za Kigeni,ni sehemu chache wanakopokea malipo kwa pesa yakigeni.Nenda India,ukienda India mwaka hadi Mwaka rupee 4 ni Dolar 1.Ukienda hata kwenye duka la kuuza pesa unahitaji Dolar lazima ujaze form yenye maelezo malefu kama una haraka ya Kitanzania Unaweza ukaondoka bila kuhudumiwa.Unaambiwa utoe Passi ya kusafiria, makusudi ya dola hizo labda niza matumizi ukiwa kwnye Transit nyumbani,lakini ukisema unahitaji kufanya shopping India utaambiwa utumie Rupee .
Risiti ina umuhimu sana. Kwanza kuiongezea mapato serikali kwa yule kukatwa ushuri. Pili kama hujaomba risiti wanachofanya wanakubadilishia kwa "Rate" tofauti ukiomba "Risiti" wanakubadilishia kwa "Rate' halali. Siku jaribu kwenda kubadilisha fedha fanya kama hutaki risiti akikupa zile hela mwambia naomba risiti utaona anapiga mahesabu upya na kukuongeza kile ambacho ungekiacha bila risiti.
Ambao hawaombi risiti wanacha change nyingi sana, ni faida kwa yule. Risiti kwa ofisini/mwajiri hazina nguvu sana kwa sababu hakuna popote zinapotunzwa akisoma, akiona rate akihakiksha fedha zipo sawa basi anaweza ichana.
Kweli ujinga kipaji, nimejua kwanini waitetea sana CCM...Sasa hiyo risiti itakusaidia nini kwa mfano
Ninawasiwasi wewe ni kati ya wanaosaidia kushusha thamani ya fedha yetu au unafurahia pengine uraia wako pia ni utata. Naona kama uzalendo hakuna kabisa hapa. Maelezo yako tu yanaonesha. Kama hata account yako tu ni ya dolla na huna imani na benki za ndani. Pia unashangilia kubadirisha kwa 2000 badala ya 1700 yaani unatamani ishuke zaidi. I si.ply hate people of your kindAcha mambo yako wewe kwanza equity bank wako vizuri sana mie nina akaunti yangu pale ya dola tena wako vizuri sana kwenye rate zao sio kama mabenki yetu hapa wanatudhulumu sana sasa ukienda crdb, nmb au nbc utaambiwa dola1=1700tsh badala ya 2000tsh, lakini equity wanawazidi hata hizo bureau de change kwa rate. Watu wengi siku hz wanaenda kubadilishia fedha zao equity kwa sababu hizo, na mie risiti huwa napewa!
Acha mambo yako wewe kwanza equity bank wako vizuri sana mie nina akaunti yangu pale ya dola tena wako vizuri sana kwenye rate zao sio kama mabenki yetu hapa wanatudhulumu sana sasa ukienda crdb, nmb au nbc utaambiwa dola1=1700tsh badala ya 2000tsh, lakini equity wanawazidi hata hizo bureau de change kwa rate. Watu wengi siku hz wanaenda kubadilishia fedha zao equity kwa sababu hizo, na mie risiti huwa napewa!
Nilidhani una akili, kumbe umejaza makamasi tu kichwani!!
Wadau,
Hata kama ni uwekezaji lazima ufuate sheria za nchi husika, lazima kuwe na win win situation.
Kwa bahati mbaya sivyo hivyo kwa haya mabenki ya nje yanayofurika nchini kila uchao, wanakuja kutuibia na kutuhujumu. Najiuliza, wanapata wapi ujasiri wa kukiuka masharti ya biashara na uwekezaji? Hivi ni kweli Benki Kuu haina mechanism ya kucheki kama haya mabenki yanafuata sheria za nchi.
Wiki tatu zilizopita nilienda Equity Bank pale Golden Jubilee kuchenji dola elfu mbili ili nipate shilingi niweze kufanya malipo mbali mbali ya kiofisi. Nilipofika Equity Bank nilielekezwa nipande ghorofani ambapo nilimpatia teller hizo dola ili anipe shilingi. Ajabu ni kuwa, nilipomwomba risiti akagoma ati hawatoagi risiti! Nikamwambia hicho kitu haiwezekani na hakipo, dada akasema ndivyo ilivyo na akamuuliza jirani yake ili nithibitishe, na mwenzake akanithibitishia! Ndipo nikawaambia wanirudishie dola zangu nikaenda kubadilishia Bureau de Change ambao baada ya kudai risiti walinipa.
Ijulikane kuwa hata hizo Bureau de Change nao ni hivyo hivyo, risiti ni hadi uidai. Wenzetu Uganda hata ukiwa unauza dola ili upate shilingi yao lazima wadai passport na wajaze fomu kadhaa na kukupa risiti yako, yaani huhitaji kuuliza.
Nachotaka kusema ni kuwa hawa Equity Bank wanahujumu uchumi wetu, wanatorosha dola zetu kupeleka kwako na hivyo kusababisha kushuka na kuporomoka kwa shilingi yetu.
Kama wako hivyo wanakosea sana
Mtoa maada umesema mwenyewe kuwa hata huko Bureau De Change ni mpaka uombe risit ndo unapewa vinginevyo hupewi....sasa hapa ni kuwaonea Equity Bank bila sababu yeyote. BOT ndo tatizo usig=dhani kwamba hawajui...wanjua kwa undani kuliko wewe ufikiriavyo na hii sio jambo jipya. Kila mradi ama bank hapa nchini vigogo na wtawala wana share zao humo kwahiyo tuwalaumu viongozi wetu kabla ya kuwalaumu Equity Bank.
Bt kubadilisha hela kwan kuna mapato unalipia?!!cjaelewa coz zile rate zimequotiwa cdhani km kuna vat pale