Equity Bank wanahujumu uchumi wetu

Equity Bank wanahujumu uchumi wetu

Acha mambo yako wewe kwanza equity bank wako vizuri sana mie nina akaunti yangu pale ya dola tena wako vizuri sana kwenye rate zao sio kama mabenki yetu hapa wanatudhulumu sana sasa ukienda crdb, nmb au nbc utaambiwa dola1=1700tsh badala ya 2000tsh, lakini equity wanawazidi hata hizo bureau de change kwa rate. Watu wengi siku hz wanaenda kubadilishia fedha zao equity kwa sababu hizo, na mie risiti huwa napewa!

Mkuu hapa hakizungumzwi rate ya exchange zaidi bali kutoa receipt

Swali ni kwa nini watoe risiti kwa wengine (Kama madai yako kuwa unapewa risiti ni ya kweli) na wengine hawapewi risiti?

Twende Mbele turudi nyuma hii nchi ukusanyaji wa mapato (ukiachilia PAYE wanayoipata kilaini bila jasho kuwatoka) hauko vizuri na usimamizi wake unakosa umakini...utoaji wa risiti ni mtu/taasisi/firm akiamua atoe au asitoe na sio suala tena lazima na la kisheria
 
Toka mwanzo ungeuliza hivi mbona ungepata jibu mujarabu!, hakuna bank inayosajiliwa Bank kuu eti wanatoa huduma bure kama taasisi ya kidini hivo wasiwe wanalipa VAT.

Ukiangalia ukutani mwa Bureau de Change yoyote utaona cheti cha mlipa kodi, hicho kinauainisha kuwa wewe ni mlipa kodi unayetambulika.

Pia unanunua dollar (mfano) kwa shs 970 na unauziwa kwa shs 1050 ukitoa kuna shs 80 inakwenda wapi hapo kama si biashara ya faida?

Umefunguka au bado?

Bt kubadilisha hela kwan kuna mapato unalipia?!!cjaelewa coz zile rate zimequotiwa cdhani km kuna vat pale
 
Kama wako hivyo wanakosea sana
Maduka yote Ya pesa Ya Tanzania tangu nianze kubadirisha pesa sijawahi kupata risiti ..hongera sana muleta mada kwani Pia leo umenifundisha uzalendo.TRA ndo Ya kufanya hiyo research hii ni elimu Ya kuwapa raia wetu . Tatizo lipo Kwenye mifumo yetu na sisi raia wenyewe. Kusema ukweli wananchi wa tanzania kuanzia viongozi na sisi wa chini hatuna uchungu na ndo maana wageni wanachuma na kuondoka. Kenya kwa Mfano wakikaa sehemu utawakuta wanajazana Kwenye kisuper market na kuchambua bidhaa zinazotoka kwao . Jiulize watanzania spirit zetu tuna kasumba Ya kuchukia vitu vyetu wenyewe. Ndo maana tunahitaji kujengeana uzalendo kwanza na kujielewa kwani viongozi hawajitambui na raia hajitambui huku wageni wanaojitambua wako busy kupiga rasilimali zetu.
 
Mimi si mtaalam wa masuala ya sheria,lakini nakumbuka kuna sheria inayotutaka sisi wananchi kidai risiti kila tufanyapo manunuzi.nahisi sisi kama wananchi tuna sehemu pia ya kushiriki mzigo huu wa lawama,mlete uzi siyasemi haya kukelekea wewe.sisi kwa pamoja kama wananchi tuna tatizo!
 
Mimi si mtaalam wa masuala ya sheria,lakini nakumbuka kuna sheria inayotutaka sisi wananchi kidai risiti kila tufanyapo manunuzi.nahisi sisi kama wananchi tuna sehemu pia ya kushiriki mzigo huu wa lawama,mlete uzi siyasemi haya kukelekea wewe.sisi kwa pamoja kama wananchi tuna tatizo!

Kama sikosei Kuna EFD regulations ya 2012 lakini pia Income tax Act kwa ujumla wake bila Shaka vinaagiza kutoa na kupokea risiti kwa kila mauzo/transaction....

Wabobevu wa masuala ya kodi wanaweza saidia zaidi juu ya sheria zinazosimamia hili
 
Sasa hiyo risiti itakusaidia nini kwa mfano
laki si pesa tell me your joking or some kind of sarcasm ...

Na mbwembwe zote unazoonesha humu kuijua na kuitetea system leo uniambie hujui faida ya kutoa na kupokea receipt kwa nchi, kwa anayetoa lakini pia kwa anayepokea???? My world.....
 
Last edited by a moderator:
Kama sikosei Kuna EFD regulations ya 2012 lakini pia Income tax Act kwa ujumla wake bila Shaka vinaagiza kutoa na kupokea risiti kwa kila mauzo/transaction....

Wabobevu wa masuala ya kodi wanaweza saidia zaidi juu ya sheria zinazosimamia hili
Ndio mkuu ,twapaswa kuchukua risiti kwa kila mchakato wa manunuzi,nadai risiti kila napoenda dukani,in so doing i am being responsible citizen!
 
hoja zuri lakini haitapata watu wa kuchangia kwa sababu wachangia wa forum hii wanapenda kujadili watu badala ya issue

Wadau,

Hata kama ni uwekezaji lazima ufuate sheria za nchi husika, lazima kuwe na win win situation.

Kwa bahati mbaya sivyo hivyo kwa haya mabenki ya nje yanayofurika nchini kila uchao, wanakuja kutuibia na kutuhujumu. Najiuliza, wanapata wapi ujasiri wa kukiuka masharti ya biashara na uwekezaji? Hivi ni kweli Benki Kuu haina mechanism ya kucheki kama haya mabenki yanafuata sheria za nchi.

Wiki tatu zilizopita nilienda Equity Bank pale Golden Jubilee kuchenji dola elfu mbili ili nipate shilingi niweze kufanya malipo mbali mbali ya kiofisi. Nilipofika Equity Bank nilielekezwa nipande ghorofani ambapo nilimpatia teller hizo dola ili anipe shilingi. Ajabu ni kuwa, nilipomwomba risiti akagoma ati hawatoagi risiti! Nikamwambia hicho kitu haiwezekani na hakipo, dada akasema ndivyo ilivyo na akamuuliza jirani yake ili nithibitishe, na mwenzake akanithibitishia! Ndipo nikawaambia wanirudishie dola zangu nikaenda kubadilishia Bureau de Change ambao baada ya kudai risiti walinipa.

Ijulikane kuwa hata hizo Bureau de Change nao ni hivyo hivyo, risiti ni hadi uidai. Wenzetu Uganda hata ukiwa unauza dola ili upate shilingi yao lazima wadai passport na wajaze fomu kadhaa na kukupa risiti yako, yaani huhitaji kuuliza.

Nachotaka kusema ni kuwa hawa Equity Bank wanahujumu uchumi wetu, wanatorosha dola zetu kupeleka kwako na hivyo kusababisha kushuka na kuporomoka kwa shilingi yetu.

Siku tutakapokuwa na task force (engine ya taifa) itakayoweka mbele maslahi ya nchi kwanza mambo mengi yatabadilika
 
Kwa nini una badlisha fedha za kigeni Bank, "Rate" zao ni ndogo sana. Nenda kwenye maduka ya kubadilisha fedha, "Rate" nzuri na hawana longo longo kwenye kutoa risiti.

Mkuu nisaidie,risiti ukipewa inakuwa na umuhimu gani hasa au ni ofisini au mwajiri huwa anahitaji?
 
Si Equity Bank tu,hapa Tanzania hakuna udhibiti wowote wa exchange ya pesa za Kigeni.Nchi za Wenzetu mfano Rwanda kuna udhibiti mkubwa wa Pesa za Kigeni,ni sehemu chache wanakopokea malipo kwa pesa yakigeni.Nenda India,ukienda India mwaka hadi Mwaka rupee 4 ni Dolar 1.Ukienda hata kwenye duka la kuuza pesa unahitaji Dolar lazima ujaze form yenye maelezo malefu kama una haraka ya Kitanzania Unaweza ukaondoka bila kuhudumiwa.Unaambiwa utoe Passi ya kusafiria, makusudi ya dola hizo labda niza matumizi ukiwa kwnye Transit nyumbani,lakini ukisema unahitaji kufanya shopping India utaambiwa utumie Rupee .

Kaka kwa India siyo yote hayo uliyoelezea yako practical.Nilikuwa Bangalore Mara tatu miaka tofauti na pale hospitali (HCG GLOBAL CARE)walilazimisha tulipe kwa dola badala ya rupee.
 
Queen Esther

Katika bank inayokuwa kwa kasi na kuenea nchini ni EQUITY na kwa Kenya ipo karibu kila mahali kama Mpesa

Ikumbukwe pia Commercial Bank of Africa (CBA) ilianzia Tz ila sasa headquarter ipo Nairobi.Tusipokuwa makini tutakuwa wasindikizaji wa wenzetu.
 
Last edited by a moderator:
Wadau,

Hata kama ni uwekezaji lazima ufuate sheria za nchi husika, lazima kuwe na win win situation.

Kwa bahati mbaya sivyo hivyo kwa haya mabenki ya nje yanayofurika nchini kila uchao, wanakuja kutuibia na kutuhujumu. Najiuliza, wanapata wapi ujasiri wa kukiuka masharti ya biashara na uwekezaji? Hivi ni kweli Benki Kuu haina mechanism ya kucheki kama haya mabenki yanafuata sheria za nchi.

Wiki tatu zilizopita nilienda Equity Bank pale Golden Jubilee kuchenji dola elfu mbili ili nipate shilingi niweze kufanya malipo mbali mbali ya kiofisi. Nilipofika Equity Bank nilielekezwa nipande ghorofani ambapo nilimpatia teller hizo dola ili anipe shilingi. Ajabu ni kuwa, nilipomwomba risiti akagoma ati hawatoagi risiti! Nikamwambia hicho kitu haiwezekani na hakipo, dada akasema ndivyo ilivyo na akamuuliza jirani yake ili nithibitishe, na mwenzake akanithibitishia! Ndipo nikawaambia wanirudishie dola zangu nikaenda kubadilishia Bureau de Change ambao baada ya kudai risiti walinipa.

Ijulikane kuwa hata hizo Bureau de Change nao ni hivyo hivyo, risiti ni hadi uidai. Wenzetu Uganda hata ukiwa unauza dola ili upate shilingi yao lazima wadai passport na wajaze fomu kadhaa na kukupa risiti yako, yaani huhitaji kuuliza.

Nachotaka kusema ni kuwa hawa Equity Bank wanahujumu uchumi wetu, wanatorosha dola zetu kupeleka kwako na hivyo kusababisha kushuka na kuporomoka kwa shilingi yetu.

Nenda crdb
 
Forex ni Black Market mpaka kwenye Mabenki. BOT wamecollapse kabisa.
 
Mkuu nisaidie,risiti ukipewa inakuwa na umuhimu gani hasa au ni ofisini au mwajiri huwa anahitaji?


Risiti ina umuhimu sana. Kwanza kuiongezea mapato serikali kwa yule kukatwa ushuri. Pili kama hujaomba risiti wanachofanya wanakubadilishia kwa "Rate" tofauti ukiomba "Risiti" wanakubadilishia kwa "Rate' halali. Siku jaribu kwenda kubadilisha fedha fanya kama hutaki risiti akikupa zile hela mwambia naomba risiti utaona anapiga mahesabu upya na kukuongeza kile ambacho ungekiacha bila risiti.

Ambao hawaombi risiti wanacha change nyingi sana, ni faida kwa yule. Risiti kwa ofisini/mwajiri hazina nguvu sana kwa sababu hakuna popote zinapotunzwa akisoma, akiona rate akihakiksha fedha zipo sawa basi anaweza ichana.
 
BOT ime ajiri hadi wasanii wamziki, unategemea nn?

BOT imejaa watoto wa akina Lowasa, Sumaye, Malecela, Sita, nk unategemea nn? Unadhani Beno Ndulu ana meno ya kuwa ng'ata hawa watoto kama hawaperform?
 
Katika bank inayokuwa kwa kasi na kuenea nchini ni EQUITY na kwa Kenya ipo karibu kila mahali kama Mpesa

Ikumbukwe pia Commercial Bank of Africa (CBA) ilianzia Tz ila sasa headquarter ipo Nairobi.Tusipokuwa makini tutakuwa wasindikizaji wa wenzetu.

Commercial bank of africa kitambo ilikuwa inaitwa UBA ni bank ya Kenyatta family.
 
Back
Top Bottom