jambo1
JF-Expert Member
- Jul 5, 2009
- 241
- 29
Kufuatia Maandamano yaliyofanywa na wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wiki hii ya kudai nyongeza ya pesa ya kujikimu kutoka Sh.5000/= hadi Sh.10000/=. Kumekuwa na kauli mbalimbali toka kwa wadau mbalimbali, lakini Mtangazaji wa Clouds FM Ephraim Kibonde amewadharau na kuwatukana wasomi kwa kiasi kikubwa. Amesema eti wanafunzi wanadai pesa kwa ajili ya anasa ya kwendea Disko, Milmani city na kununua vitu vya anasa.
Kama matangazaji mtu mzima mwenye ufahamu hakupaswa kuwa na kauli za kipuuzi kama hizi wakati watu wako kwenye madai ya msingi. Kauli hii si ya kiungwana naamini imewachukiza kwa kiasi kikubwa wanazuoni.
Hivyo Kibonde anapaswa kuwaomba radhi wasomi na pia achunge sana kauli zake za kudharau madai ya watu au mambo ya msingi kwani si mara ya kwanza kwa Kibonde kuwa na Kauli za ajabu, matusi na dharau katika mambo ya msingi.
Kama matangazaji mtu mzima mwenye ufahamu hakupaswa kuwa na kauli za kipuuzi kama hizi wakati watu wako kwenye madai ya msingi. Kauli hii si ya kiungwana naamini imewachukiza kwa kiasi kikubwa wanazuoni.
Hivyo Kibonde anapaswa kuwaomba radhi wasomi na pia achunge sana kauli zake za kudharau madai ya watu au mambo ya msingi kwani si mara ya kwanza kwa Kibonde kuwa na Kauli za ajabu, matusi na dharau katika mambo ya msingi.