Enzi ulipokuwa boarding

Enzi ulipokuwa boarding

nakumbuka nlihamia shule Siku Ya kwanza darasani Nkaenda mbele ya Darasa nkauliza Nani namba moja akaja mshkaji nkamwambia mbele ya dara we kwanzia leo utakuwa number 2 wengne nyuma ha ha ha kumbe biti tu
 
nilikuwa sipendi kwenda 'PREPO' na nilikuwa nikilazimishwa kwenda basi darasani watu siku hiyo hawatasoma kwa raha (nilikuwa msumbufu sana) kwa hiyo ilipitishwa resolution kuwa ntakuwa nafungiwa bwenini nilale na taa zinazimwa. sasa kwa kuwa mwalimu wa zamu ilikuwa lazima aje akague ikabidi kitanda changu kiongezewe godoro(ambalo lilikuwa kubwa zaidi ya kitanda) na likazuia hata mwalimu akija hanioni anapita tu mi nakuwa nimezama katikati huko...

afu nilikuwa sipendi maharage kwa hiyo nikajiandikisha mi ni mgonjwa kwa hiyo nilikuwa nakula spesho dayati....dagaa na mchicha wa kuchemsha, nikitoka hapo naenda kugawana na marafiki zangu, tunakuwa tumekula maharage, mchicha na dagaa...
 
Kuna jamaa kibaha sec alikuwa ana tabia ukikatika umeme,anafungua kabati la mshikaji mmoja na kuiba maziwa ya unga kisha analamba kama glucose.Siku hiyo umeme umekata,kama kawa akaenda kwenye locker la mshikaji,akafungua kopo,akachota na kubugia yote mdomoni.Loh!kumbe jamaa mwenye locker alificha maziwa ya unga na badala yake akaacha kopo la sabuni ya unga.Acha jamaa asuuze ulimi bombani kama nguo!
 
Me niliambiwa nenda bweni(jina kapuni) ukwamuulizie jamaa anaitwa Bunsen burner!!! LOH! Nilipofika hapo bwenini jamaa wanistukia kuwa

nimeingizwa mkenge nao wakanambia ametoka nimsubiri kama dakika sita hivi atarudi!! ndugu niliuza chai mpaka nikakoma, baadae ndo

wakanielewesha.. nilimind we acha tu.
ahhaaaaaaaaaaaaaaaaaa yako kali sasa
 
Nakumbuka cku ikitokea sherehe au msiba mtaani,lazma tuvunje sheria tuzamie kitaa na tukifika huko utafikiri cc ndo wahusika,tunagonga menye then kingine tunabeba,so ikatokea cku moja tumezamia haruc m1 kat ya masela 2liokuwepo akawa ndo anagawa menyu,lo mara gafla anashangaa ticha yupo mbele yake,jamaa ikabidi amgawie na ticha ila tulivyorud xul mh
 
Nakumbuka Umbwe Sec siku ya kwanza kufika tu, walituita "njuka" jamaa mmoja alinifata nikiwa juu ya kitanda pale dom 4, akaniambia kuwa "oya dogo unanilipa hela yangu lini" nikamuambia ipi, akanijibu , si ya hizi ndala ulizovaa? au ni zako?

Kuanzia leo hizo ndala ni zangu na nimekuuzia tayari na unipe hela yangu haraka, kwanza nipe sabuni na taulo nikaoge (huku akinivua zile ndala mpya za Umoja - 1997) akazichukua na kutokomea nisikokujua, ila brother mmoja akaniambia kuwa usijali nitakuonesha anapolala utaenda kuzichukua, duh kaka mbona niliona shule chungu.....

Dah umenikumbusha mbali me nilisoma narumu ndo tulikuwa viburudisho vyenu
 
Nakumbuka cku ikitokea sherehe au msiba mtaani,lazma tuvunje sheria tuzamie kitaa na tukifika huko utafikiri cc ndo wahusika,tunagonga menye then kingine tunabeba,so ikatokea cku moja tumezamia haruc m1 kat ya masela 2liokuwepo akawa ndo anagawa menyu,lo mara gafla anashangaa ticha yupo mbele yake,jamaa ikabidi amgawie na ticha ila tulivyorud xul mh

Hehehehe yaaani kiongozi stori yako imenikumbusha mengi sana. Nakumbuka tulikua tunazamia
 
Nakumbuka cku ikitokea sherehe au msiba mtaani,l azma tuvunje sheria tuzamie kitaa na tukifika huko utafikiri cc ndo wahusika,tunagonga menye then kingine tunabeba,so ikatokea cku moja tumezamia haruc m1 kat ya masela 2liokuwepo akawa ndo anagawa menyu,lo mara gafla anashangaa ticha yupo mbele yake, jamaa ikabidi amgawie naticha ila tulivyorud xul mh
Tulikua tunavizia misiba na kama hamna basi tulitorokea kwenye bar za Mbege. Tulikua tuna chimbo letu lilikua linaitwa Ngiwara necha kule mwika Vunjo Sec.

Basi siku iyo nilikua nina kiu kweli maana jumamosi ilikua zamu ya ticha mnoko hivo sikuweza kutoroka nikatumia siku ya jumapili kuomba gatepass ya kwenda kanisani.mbio mpaka counter nampigia kelele stanfodi anipe kubwa.

Bila kutazama pembeni: stanfod akanipa basi sikuweka chini nikapiga kama nguchu tatu ivi:kugeuka pembeni nagongana macho na Mr mwasha mwalimu mnoko kuliko wote na anasifika kwa kupiga viboko.

Kwa mshtuko nilioupata nikajikuta natabasamu huku mdomoni nina mustach wa mapovu ya mbege. Yaliyonikuta kesho yake ni balaa...
 
Musoma Tech, tulikua na mwalimu mmoja anaitwa mwl.J uju yeye siku zote akili yake ilikua dk10 mbele. Mara nyingi alikua yupo upande wa wanafunzi,walimu wenzake alikua hawapendi.

Basi siku moja kwenye siku baraza akawa anachangia hoja juu ya mwenendo mbaya wa shule kukoswa wafanyakazi na walimu wanaojituma, akasema zamani hii shule ilikua na ng'ombe wa mayai na kuku wa maziwa,aisee watu tulicheka kuliko maelezo maana alivyoipiga vice versa tena kwa kujiamini,hata headmaster hakuvumilia kicheko.
 
Kaka umenikumbusha wazee wa mara sec,bifu lenu na letu lilikua haliishi.
Kuna siku tumecheza fainali kwenye uwanja wenu,kati ya musoma day na musoma tech,tuliwafunga hao watoto wa musoma day.Kwa hasira musoma day na mara sec wakaungana ili kutupiga,aisee hilo gemu lilikua balaa.Tulikuja mitaa fulani ya nyasho kuvizia kila daladala iliyobeba watoto wa musoma day,tulipiga sana,hadi saa tatu usiku ndo tuliletewa FFU shuleni maana tulipasua magari vioo ile mbaya.


Nakumbuka enzi hizo nasoma Mara Sec.. yaan mnawaza kugombana na Musoma Tec. Sababu zenyewe za maana hakuna yaan mkikutana..ndo tuseme kwenye UMISSETA mazee yaan mnapeana kichapo cha mbwa mwizi..nakumbuka game ilipigwa Musoma Tec tukamvunja jamaa Yao mguu.Ebwanaee jamaa Hawakujua mambo ya 'fairplay' walitukimbiza Kama km6..kwa masela angalau ilikuwa poa..ila mademu wetu jamaa waliwapa taabu..sipati kusimulia..haya maisha tumetoka mbali!!
 
Kuna jamaa kibaha sec alikuwa ana tabia ukikatika umeme,anafungua kabati la mshikaji mmoja na kuiba maziwa ya unga kisha analamba kama glucose.Siku hiyo umeme umekata,kama kawa akaenda kwenye locker la mshikaji,akafungua kopo,akachota na kubugia yote mdomoni.Loh!kumbe jamaa mwenye locker alificha maziwa ya unga na badala yake akaacha kopo la sabuni ya unga.Acha jamaa asuuze ulimi bombani kama nguo!

ahahahaaah!!
 
Ni kweli bodi kuna utemi,nakumbuka mara ya kwanza kuripoti form one mwaka 1999 same boys,tulipewa dishi watu wa tano cha ajabu tuligombania wote tukakosa sb ulimwagika
 
Hizo zote stori tu,mwisho wa maelezo ni UMBWE BOYS,siku tunaingia shule tulikuta raia kibao wamevaa vyuti,wanapokea wazazi,kumbe ni madenti,ukiwapa tranka lako tu,imekula kwako,,,ukiingia domitory unakuta vitanda vyote havina chagga,inabidi uende dorm 6,kwa ma 4m six ukanunue chaga,chaga moja ni buku,kama hutakilala chini.....

Mambo ya toilet tulikuta choo kimoja tu kizima,,,kama atm ya crdb saa 12 jioni...mtu nyomiiiii, ukiwa f5 au f1 ukiingia tu lazima "ukatwe mkia", yaani hiyo siku ni fimbo kwa kwenda mbelee, mtarushiwa mawe chumbani, immagine mtu anakuja kunoa panga dirishani kwako usiku wa manane,,,,,,,,,

uji tulikua tunauita fongo, watoto wanaojiweza ndo waliweza kununua sugar, sisi tulikuwa tunapiga fongo chuma-yaani bila sukari au tunachanganya super-deep(jussi kola) tunapata mafleva, uji wenyewe umechanganywa na pumba yaani full kutematema,.

Siku ya nyama au wali ni vita balaa,yaani ukuifanya utafiti,watu wengi sana wanarudi kwao na ngeu za wali....mwisho kabisa ni kwenye vita kati ya sisi na lyamungo boys,,,tulikuwa tunapigania uwanja flani mkuuuubwa tulikua tunapaita desert,tulikua na division of labour ya kutosha,form six walikuwa wapiganaji wakuu,form five kuvunja stoo na kuchukua zana kama majembe, shoka,panga etc....

Form four walikua warusha mawe na kuleta noma,form three walibeba viti,kuni,kuwavunjia wenzetu vioo,kama tungeshinda viti,,form two na one ni waokota mawe na kuwapa wakubwa ili wawarushie maadui na wasindikizaji cz hamna mtu kubaki nyuma.

UMBWE was something else,,,,,siku ya graduation wababe wanabeba mabench na wanaweka kambi kwenye familia yoyote waliokuja kumpongeza mwanao,wanagonga diko then wanahamia familia nyingine.....siku za kwenda shule za girls ni full kuanua nguo za watu na kupiga "butterfly" matranka ya watu ili kupata pamba,,,,,,,

Migomo ya ndani ,watu wanaenda kukata umeme kwenye transformer,,,,,,,,,wezi walikuwa ni wakali mithili ya carlos,watu wanaiba hadi bendera na bunduki ya mlinzi,kuiba ndizi kijijini,,,kuvamia soko la pale kijijini,,,,duuuh,,,,,,embu mwanaUMBWE mmoja aendeleze zile swagg zetu,maana nadhani hamna kambi kama lile
 
TE TE TEH TEH TEH,unanivunja mbavu kaka asee ningekuwepo ningekuwa nacheka kila nikikuona!!
 
Kuna stori imenichekesha sana ya kula na kuvimbewa, JF full maraha.

Shybush kulikuwa na kundi la watu hawanyi chooni ili wasifanye usafi, walienda kuchimba vyoo vyao porini kila mtu na chake. Halafu kulikuwa na Headmaster mkali huyo usiku saa nane anzuga kuja kutuchapa kumbe anatafuta mbinu ya kwenda kwa demu wake (ticha wa hapohapo skuli) kwa hiyo anaanzia mabwenini kutembeza viboko.
 
Tulikuwa na katabia kakuzamia misosi ya sherehe tukiwa pale kibaha sec.Siku hiyo tumezamia sherehe moja,kumbe sherehe yenyewe ilikuwa ni mjeda anaoa.Mshikaji mmoja akaamua kutuiga,akapanga foleni,alipofika kwa wahudumu,badala ya kuomba apewe kuponi yeye akasema anataka koni,hapo ndipo alipostukiwa kwamba ni mzamiaji,ee bwana jamaa alipewa mbata za mgongo na makonzi ya kutosha kutoka kwa kamati ya ulinzi ya wanajeshi watupu.
 
Mbeya sec. School shule yetu ilikuwa yakistaarab had rahaa we acha 2.
 
Tulikua tunavizia misiba na kama hamna basi tulitorokea kwenye bar za Mbege. Tulikua tuna chimbo letu lilikua linaitwa Ngiwara necha kule mwika Vunjo Sec.

Basi siku iyo nilikua nina kiu kweli maana jumamosi ilikua zamu ya ticha mnoko hivo sikuweza kutoroka nikatumia siku ya jumapili kuomba gatepass ya kwenda kanisani.mbio mpaka counter nampigia kelele stanfodi anipe kubwa.

Bila kutazama pembeni: stanfod akanipa basi sikuweka chini nikapiga kama nguchu tatu ivi:kugeuka pembeni nagongana macho na Mr mwasha mwalimu mnoko kuliko wote na anasifika kwa kupiga viboko.

Kwa mshtuko nilioupata nikajikuta natabasamu huku mdomoni nina mustach wa mapovu ya mbege. Yaliyonikuta kesho yake ni balaa...

hehehehe haika mangi
 
Back
Top Bottom