Elimu ni cheti au ni ujuzi?

Elimu ni cheti au ni ujuzi?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
37,156
Reaction score
55,653
Hapa nilipo nina vyeti vingi kweli, vinakaribia kujaa begi, lakini sina uwezo wa kuvumbua chochote kile kwa kutumia elimu niliyoipata kutokea chekechea mpaka uprofeseri. Nazidiwa ata na mafundi majiko walioishia darasa la saba, wanaweza kutengeneza kitu. Yaani nisipo ajiriwa na huu wingi wa vyeti nilivyonavyo, sitaweza kuishi kabisa. Sasa najiuliza swali, elimu ni kupata ujuzi au ni kupata cheti tu? Kwa sababu, ata huku mashuleni na vyuoni tunajifunza namna ya kujibu maswali tu, na tunafaulu vizuri kwa alama A; ila kiuhalisia hatuvumbui vitu, tunategemea kuajiriwa tu.​
 
Elimu ni maarifa. lakini kugundua kunatokana na vitu vingi mnooo na elimu ikiwa ndani yake...
Gunduzi nyingine zilianza kisha elimu ikafata.. maarifa yalitafutwa baada ya gunduzi, haswa gunduzi za kale.
 
Elimu ni maarifa. lakini kugundua kunatokana na vitu vingi mnooo na elimu ikiwa ndani yake...
Gunduzi nyingine zilianza kisha elimu ikafata.. maarifa yalitafutwa baada ya gunduzi, haswa gunduzi za kale.
Tukisema, chimbuko la elimu ni mawazo ya watu ambao hawakwenda shule ila walizaliwa na vipaji vyao, tutakuwa tunakosea?
 
Elimu ni ujuzi cheti ni nyaraka ya kisheria kuthibitisha elimu (sio ujuzi
Logic: Elimu ni ujuzi , cheti ni nyaraka ya kisheria kuthibitisha elimu = cheti ni nyaraka ya kisheria kuthibitisha ujuzi. Kwa hiyo, mwenye elimu lazima awe na ujuzi; kama hana ujuzi atakuwa hana elimu. Hapo nipo sahihi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom